Uchaguzi 2020 Hizi si dalili njema kuelekea Oktoba 28

Subira the princess

JF-Expert Member
Mar 3, 2018
2,474
2,646
Wasalaam,

Kitendo cha tume ya Taifa ya Uchaguzi kutoka haraka kukemea makusudio ya vyama vya upinzani kushirikiana katika uchaguzi huu ni cha kibaguzi hakikubaliki. Sababu iliotolewa na NEC ni dhaifu na ni dhahiri ni kuitetea CCM, eti wananchi watachanganyikiwa siku ya uchaguzi na eti watashindwa wampige kura nani.

Hapa najiuliza hawa wananchi NEC inaowasemea ni mbumbumbu kiasi gani hata wasijue wamchague nani? Ina maana watanzania ni vilaza na kwamba vyama vya upinzani vikiungana tutachanganyikiwa tusijue tumchague nani!

Kuna dalili na hisia mbaya kwamba tume ya taifa ya uchaguzi IPO pale kwa maslahi ya CCM na inapokea maelekezo kutoka kwa mwenyekiti wa CCM ambae ndio muajiri wao, kwa kifupi watumishi wa NEC ni makada wa CCM.

Hitimisho: Kila mpenda haki na Amani ya taifa hili aikemee Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuacha uCCM ili uchaguzi uwe kwenye sanduku la kura kwa Uhuru na uwazi wenye nia ya kushirikiana waachwe washirikiane, wananchi wakichanganyiwa itakua vyema maana watampigia kura Mh. Magufuli hivyo kuwa faida kwa NEC yenyewe, CCM, TLP na UDP.

Maendeleo yana vyama.
 
Watakavyoweka ugumu ndipo wanasaidia kumtangaza Lissu pasipo kujua kwani wananchi wameishafahamu ni kwa nini wanazuia ushirikiano hivyo watakwenda kumpigia kura Lissu.

Hata wale wa vyama vidogo ambavyo wanaelewa kuwa ni wasindikizaji wa msimu wa uchaguzi nao watapiga kura kwa Lissu.
 
Watakavyoweka ugumu ndipo wanasaidia kumtangaza Lissu pasipo kujua kwani wananchi wameishafahamu ni kwa nini wanazuia ushirikiano hivyo watakwenda kumpigia kura Lissu. Hata wale wa vyama vidogo ambavyo wanaelewa kuwa ni wasindikizaji wa msimu wa uchaguzi nao watapiga kura kwa Lissu.
Nguvu ya umma? Sidhani maana tume ni ccm mapolice ni ccm
 
Huu nao ni ubabaishaji kama ilivyo kawaida. Mlezi wa vyama sio Tume ni Msajili. Pigeni kampeni kutafuta kura, sio kutuletea taarabu zenu. hizi ni dalili za kushindwa na kuishiwa sera. Kama mlijua mtashirikiana mbona hamkujipanga mapema??
 
"Kwa mujibu wa ibara ya 74(7) ya katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, Tume ya taifa ya uchaguzi ni idara huru inayojitegemea. Aidha, ibara ya 74(11) ya katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania inaeleza kuwa Tume katika kutekeleza majukumu yake ya kikatiba haitalazimika kupokea maelekezo au amri kutoka kwa mtu yoyote au idara yoyoye ya serikali au kufuata maoni ya chama chochote Cha siasa" kwa maelezo hayo Tume Haina woga wowote katika kutekeleza majukumu yake Hadi uje upotoshe watu kuwa inapendelea chama fulani
 
Ukisikia kupigwa pin mpaka kuchanganyikiwa ndio huku,na bado amjasema dadeki,mtulie dawa iwaingie vizuri.Nyinyi amjielewi ni kukurupuka bila break hao NEC wamekemea lini hayo makusudio ya kushirikiana kati ya CDM na ACT.Usipotoshe umma ,uache kuweweseka.kumbe msajili wa vyama vya siasa anaitwa NEC?
 
"Kwa mujibu wa ibara ya 74(7) ya katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, Tume ya taifa ya uchaguzi ni idara huru inayojitegemea. Aidha, ibara ya 74(11) ya katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania inaeleza kuwa Tume katika kutekeleza majukumu yake ya kikatiba haitalazimika kupokea maelekezo au amri kutoka kwa mtu yoyote au idara yoyoye ya serikali au kufuata maoni ya chama chochote Cha siasa" kwa maelezo hayo Tume Haina woga wowote katika kutekeleza majukumu yake Hadi uje upotoshe watu kuwa inapendelea chama fulani
Sio kwamba hawajui. Ila wanajitoaga ufahamu tu!!
Hawataki kabisa kusikia kitu kinachoitwa katiba, Sheria au Kanuni!
WAO NI KULALAMA TU
 
"Kwa mujibu wa ibara ya 74(7) ya katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, Tume ya taifa ya uchaguzi ni idara huru inayojitegemea. Aidha, ibara ya 74(11) ya katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania inaeleza kuwa Tume katika kutekeleza majukumu yake ya kikatiba haitalazimika kupokea maelekezo au amri kutoka kwa mtu yoyote au idara yoyoye ya serikali au kufuata maoni ya chama chochote Cha siasa" kwa maelezo hayo Tume Haina woga wowote katika kutekeleza majukumu yake Hadi uje upotoshe watu kuwa inapendelea chama fulani
Utakuwa kichaa au kipofu wa akili, unakumbuka kauli "nikuteue mimi, nikupe gari na posho halafu umtangaze mpinzani"
 
INAONESHA jinsi gani wapinzani wa Nchi hii hamko makini kabisa na mnajazana upepo usio na maana hata kidogo na kutiana ujinga.

Hivi ndivyo hata fomu za wagombea wengi zilikosewa kujazwa kwa ujinga Kama huu.

Siamini Kama kweli tu ashindwa kutofautisha MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA na TUME YA TAIFA YUCHAGUZI.

Hapo ndio watu hutuona hatujielewi. Hilo la ACT na Chadema limetolewa taarifa na Msajili wa Vyama vya Siasa na sio time. Tatizo tumekariri.
IMG_20200924_122134.jpg
 
Tangu NEC ilipopewa jukumu la kujaza form za wagombea wa CCM na ikazijaza zote, imani yangu ndogo iliyo kuwa imebaki kwao nayo ilipotea kabisa.
 
NAOMBA TUKUKEMEE WEWE KWA KUTOKUJUA KUSOMA KISWAHILI KWA UFASAHA. NAAMBATANISHA BARUA HII UISOME HALAFU UTULETEE BARUA YA TUME ILIYOKEMEA HAO ACT NA CHADEMA.
PSX_20200924_122215.jpg
 
Wasalaam,

Kitendo cha tume ya taifa ya uchaguzi kutoka haraka kukemea makusudio ya vyama vya upinzani kushirikiana katika uchaguzi huu ni cha kibaguzi hakikubaliki. Sababu iliotolewa na NEC ni dhaifu na ni dhahiri ni kuitetea CCM, eti wananchi watachanganyikiwa siku ya uchaguzi na eti watashindwa wampige kura nani.

Hapa najiuliza hawa wananchi NEC inaowasemea ni mbumbumbu kiasi gani hata wasijue wamchague nani? Ina maana watanzania ni vilaza na kwamba vyama vya upinzani vikiungana tutachanganyikiwa tusijue tumchague nani!

Kuna dalili na hisia mbaya kwamba tume ya taifa ya uchaguzi IPO pale kwa maslahi ya CCM na inapokea maelekezo kutoka kwa mwenyekiti wa CCM ambae ndio muajiri wao, kwa kifupi watumishi wa NEC ni makada wa CCM.

Hitimisho: Kila mpenda haki na Amani ya taifa hili aikemee Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuacha uCCM ili uchaguzi uwe kwenye sanduku la kura kwa Uhuru na uwazi wenye nia ya kushirikiana waachwe washirikiane, wananchi wakichanganyiwa itakua vyema maana watampigia kura Mh. Magufuli hivyo kuwa faida kwa NEC yenyewe, CCM, TLP na UDP.

Maendeleo yana vyama.
NEC iliyopo CCM na hii NEC ni mtu na dada ake
 
Back
Top Bottom