Uchaguzi 2020 Baridi Tanzania. Kenya 2022 tayari Moto

Msulibasi

JF-Expert Member
Dec 2, 2014
5,836
7,492
Natazama uchaguzi wa Tanzania 2020 naona upo baridi kupitiliza. Hakuna vuguvugu kuanzia kwenye media mpaka mitaani. Kenya uchaguzi mkuu ni 2o22 lakini mijadala imeshika kasi. Mihemko ni ya kiwango cha juu kuliko Tanzania utadhani Tanzania ndio 2022.

Hali hii si yenye afya kwa mustakabali wa maendeleo ya nchi kwani uchaguzi huibua mijadala mingi miongoni mwa jamii na mawazo mbadala.

Ni wakati muafaka kwa taasisi mbalimbali kutoka hadharani kuweza kuusisimua uchaguzi wetu vinginevyo natabiri utakuwa uchaguzi wa UVCCM, BAVICHA, JUVICUF ,NGOME nk raia wasio wanachama wa vyama hawaelekei kuguswa.

Kenya mijadala ipo huru sana ,vijembe vya kisiasa, burudani vichekesho vya kisiasa na mashambulizi ya ana kwa ana ya kisiasa yametamalaki na watu wa Kenya wanaonekana kuzoea na kuchukulia positive. Kambi zinajengwa na kubomolewa kila uchao na maisha yanendelea.

Mazingira ya Kenya ya kisiasa ndio yalikuwapo Tanzania kabla ya Hapa kazi tu. Uchaguzi ulikua na sura ya elimu uchumi na burudani. Nani Katuloga?
 
Umezoea vurugu zako na mmeo unataka kuharibi nchi
Natazama uchaguzi wa Tanzania 2020 naona upo baridi kupitiliza. Hakuna vuguvugu kuanzia kwenye media mpaka mitaani. Kenya uchaguzi mkuu ni 2o22 lakini mijadala imeshika kasi. Mihemko ni ya kiwango cha juu kuliko Tanzania utadhani Tanzania ndio 2022.

Hali hii si yenye afya kwa mustakabali wa maendeleo ya nchi kwani uchaguzi huibua mijadala mingi miongoni mwa jamii na mawazo mbadala.

Ni wakati muafaka kwa taasisi mbalimbali kutoka hadharani kuweza kuusisimua uchaguzi wetu vinginevyo natabiri utakuwa uchaguzi wa UVCCM, BAVICHA, JUVICUF ,NGOME nk raia wasio wanachama wa vyama hawaelekei kuguswa.

Kenya mijadala ipo huru sana ,vijembe vya kisiasa, burudani vichekesho vya kisiasa na mashambulizi ya ana kwa ana ya kisiasa yametamalaki na watu wa Kenya wanaonekana kuzoea na kuchukulia positive. Kambi zinajengwa na kubomolewa kila uchao na maisha yanendelea.

Mazingira ya Kenya ya kisiasa ndio yalikuwapo Tanzania kabla ya Hapa kazi tu. Uchaguzi ulikua na sura ya elimu uchumi na burudani. Nani Katuloga?
 
Natazama uchaguzi wa Tanzania 2020 naona upo baridi kupitiliza. Hakuna vuguvugu kuanzia kwenye media mpaka mitaani. Kenya uchaguzi mkuu ni 2o22 lakini mijadala imeshika kasi. Mihemko ni ya kiwango cha juu kuliko Tanzania utadhani Tanzania ndio 2022.

Hali hii si yenye afya kwa mustakabali wa maendeleo ya nchi kwani uchaguzi huibua mijadala mingi miongoni mwa jamii na mawazo mbadala.

Ni wakati muafaka kwa taasisi mbalimbali kutoka hadharani kuweza kuusisimua uchaguzi wetu vinginevyo natabiri utakuwa uchaguzi wa UVCCM, BAVICHA, JUVICUF ,NGOME nk raia wasio wanachama wa vyama hawaelekei kuguswa.

Kenya mijadala ipo huru sana ,vijembe vya kisiasa, burudani vichekesho vya kisiasa na mashambulizi ya ana kwa ana ya kisiasa yametamalaki na watu wa Kenya wanaonekana kuzoea na kuchukulia positive. Kambi zinajengwa na kubomolewa kila uchao na maisha yanendelea.

Mazingira ya Kenya ya kisiasa ndio yalikuwapo Tanzania kabla ya Hapa kazi tu. Uchaguzi ulikua na sura ya elimu uchumi na burudani. Nani Katuloga?
Wakianza kuchinjana pia njoo hapa uwasifie.
 
Tz wagombea wengi walitegemea kupita kwa kununua wapiga kura za maoni.. Tangu waambiwe kuwa mchujo utaanzia Dom na majina matatu kurudishwa jimboni, wagombea wamechanganyikiwa.. Hapa kila mmoja anangojea jina lirudi ndio mbwembwe zianze!
 
Wapiga kura bwana....ni sawa tu na wanasiasa mnawapigia kelele.

Juzi tu 2014 mlikuwa mnatuaminisha hakuna utawala wa hovyo kama wa JK.

Leo eti utawala wa JK umekuwa wa mfano. Na nawahakikishia JPM akimaliza muda wake ndani ya miaka miwili mraanza kusema alikuwa Rais bora kuliko atakayekuwepo.
 
Tz wagombea wengi walitegemea kupita kwa kununua wapiga kura za maoni.. Tangu waambiwe kuwa mchujo utaanzia Dom na majina matatu kurudishwa jimboni, wagombea wamechanganyikiwa.. Hapa kila mmoja anangojea jina lirudi ndio mbwembwe zianze!
Kumbe ndio utaratibu wa sasa, aisee.

Pia inawezekana wapinzani hawajapata mgombea mwenye ushawishi mkubwa. Hawa kina Nyalandu baridi sama
 
Natazama uchaguzi wa Tanzania 2020 naona upo baridi kupitiliza. Hakuna vuguvugu kuanzia kwenye media mpaka mitaani. Kenya uchaguzi mkuu ni 2o22 lakini mijadala imeshika kasi. Mihemko ni ya kiwango cha juu kuliko Tanzania utadhani Tanzania ndio 2022.

Hali hii si yenye afya kwa mustakabali wa maendeleo ya nchi kwani uchaguzi huibua mijadala mingi miongoni mwa jamii na mawazo mbadala.

Ni wakati muafaka kwa taasisi mbalimbali kutoka hadharani kuweza kuusisimua uchaguzi wetu vinginevyo natabiri utakuwa uchaguzi wa UVCCM, BAVICHA, JUVICUF ,NGOME nk raia wasio wanachama wa vyama hawaelekei kuguswa.

Kenya mijadala ipo huru sana ,vijembe vya kisiasa, burudani vichekesho vya kisiasa na mashambulizi ya ana kwa ana ya kisiasa yametamalaki na watu wa Kenya wanaonekana kuzoea na kuchukulia positive. Kambi zinajengwa na kubomolewa kila uchao na maisha yanendelea.

Mazingira ya Kenya ya kisiasa ndio yalikuwapo Tanzania kabla ya Hapa kazi tu. Uchaguzi ulikua na sura ya elimu uchumi na burudani. Nani Katuloga?
Udikteta unatuangamiza tuupinge kwa nguvu zetu zote.
 
Back
Top Bottom