iparamasa
JF-Expert Member
- Nov 14, 2013
- 13,438
- 14,916
Ni wazi CCM hivi sasa ni chama dhaifu kisiasa kuliko wakati wowote katika historia yake. Ni wakati huu kikiwa dhaifu hakina hazina ya viongozi wenye nguvu katika jamii ambao wana uwezo wa kukisemea na kukirudishia uhai kama alivyofanya nyerere baada ya mwinyi kuachia madaraka. Ni chama ambacho kiongozi wake mkuu yeye binafsi na familia yake wanatuhumiwa kuifisadi nchi na takribani wagombea urais wote wana tuhuma za ufisadi.
Chama kimepasuka kila kona na ni kama magenge ya mafia yanapigana ili kuchukua nafasi ikulu ili yapate kuiba tena na tena. CCM hii ndiyo inatuma vijana wake kuwapiga wazee wa chama ambao pengine wangeweza kuubadilisha umma kifikra na kuifikiria ccm kama chama na kwamba waovu wasihusishwe nao na kutoa ahadi ya kuwaondoa katika mbio za urais kama nyerere alivyofanya kwa malecela.
Warioba kapigwa,salim ahmed salim yuko kimya,mkapa yuko kimya,nchi inafanana na kuku aliyekatwa kichwa,haina mtu wa kutolea majibu masuala ya kitaifa.Safari hii wapinzani washindwe wenyewe kwa kuwa ni CCM ambayo imetoa mwaka mzima wa kampeni na elimu kwa umma kwa kuanzia sasa kwenye chaguzi za mitaa,kampeni za bunge la katiba,kura ya maoni,escrow,operesheni tokomeza,mchakato wa uchaguzi na mengine mengi yatasaidia wapinzani kuibana vilivyo CCM na kuinyanganya kura nyingi,
Chama kimepasuka kila kona na ni kama magenge ya mafia yanapigana ili kuchukua nafasi ikulu ili yapate kuiba tena na tena. CCM hii ndiyo inatuma vijana wake kuwapiga wazee wa chama ambao pengine wangeweza kuubadilisha umma kifikra na kuifikiria ccm kama chama na kwamba waovu wasihusishwe nao na kutoa ahadi ya kuwaondoa katika mbio za urais kama nyerere alivyofanya kwa malecela.
Warioba kapigwa,salim ahmed salim yuko kimya,mkapa yuko kimya,nchi inafanana na kuku aliyekatwa kichwa,haina mtu wa kutolea majibu masuala ya kitaifa.Safari hii wapinzani washindwe wenyewe kwa kuwa ni CCM ambayo imetoa mwaka mzima wa kampeni na elimu kwa umma kwa kuanzia sasa kwenye chaguzi za mitaa,kampeni za bunge la katiba,kura ya maoni,escrow,operesheni tokomeza,mchakato wa uchaguzi na mengine mengi yatasaidia wapinzani kuibana vilivyo CCM na kuinyanganya kura nyingi,