Elections 2010 Uchaguzi 2010. mialiko ya kuchangia kampeni kwa kadi kama harusi

Chimunguru

JF-Expert Member
May 3, 2009
10,678
4,350
Ukiwa na ndugu yako au mtu wako wa karibu ana nia ya kugombea uheshimiwa andika maumivu. Jana mamsap alipokea simu toka kwa kaka yake wa baba mkubwa akamwambia ana kadi yake. alipoulizwa kadi ya nini shemeji yangu akasema nakuja kukuletea utaiona hapo hapo, tukabaki tunajiuliza hii sasa itakuwa kadi ya kumi ya mchango wa harusi mpaka jana. Basi shem akaja salamu kama kawaida story nyingi, baadaye akaanza kumnadi dada yake ambaye ni diwani maaeneo flani hapa town. Shemeji unajua dada yangu amekuwa diwani muda mrefu sasa anataka kugombea uheshimiwa sana pale mjengoni DODOMA, wewe ni ndugu wa karibu kwa hiyo ni vema ukajumuika nasi katika hili jambo jema la kumsapoti shemeji yako katika kampeni zake za kuwania kiti cha UBUNGE wa viti maalum pale Coast Region, akatoa kadi maalum kama ya harusi imechapishwa swafi kabisa na maelezo yake, wapi kikao kitafanyika na mbiu ya Mchango wenu unahitajika ili kufanikisha hilo zoezi. leo mwezi wa nne watarajiwa washaanza maandalizi chini chini kusaka pesa kwa vikao. Cant wait kwenda kuona manjonjo na strategies za kugombea ubunge viti maalum unakuwaje. mtapata newz wadau msikonde!!!!!!!
 
mkeo alipokea kad?
msaidieni huyo, mbinu zipo nying sana mojawapo ni hiyo,
maana wengine si wana fungua makampun hewa (deep green) na kuchota pesa,
 
Aliipokea asingeweza kataa mkuu, ngoja tuone hiyo fund raising itakuwaje
 
Back
Top Bottom