Mag3
Platinum Member
- May 31, 2008
- 13,064
- 22,757
Waziri awatahadharisha wapiga kura wa Busanda kuwa wasipomchagua mgombea wa CCM watabambikiwa kodi na kunyang'anywa leseni -
Makame kimya !
Katibu Mkuu wa CCM amtisha msimamizi wa uchaguzi Biharamulo kuwa akithubutu kutangaza CCM kushindwa ajue hana kazi -
Makame kimya !
Viongozi wa CCM wanakamatwa na raia wema wakinunua shahada za uchaguzi na kufikishwa kwenye vyombo vya dola -
Makame kimya !
Makame kimya !
Katibu Mkuu wa CCM amtisha msimamizi wa uchaguzi Biharamulo kuwa akithubutu kutangaza CCM kushindwa ajue hana kazi -
Makame kimya !
Viongozi wa CCM wanakamatwa na raia wema wakinunua shahada za uchaguzi na kufikishwa kwenye vyombo vya dola -
Makame kimya !
Hii mifano mitatu tu inatoa ishara ya hali ya hatari inayotunyemelea kuelekea kwenye uchaguzi mkuu 2010. Inatisha haya mambo yanapofanyika wazi wazi bila kukemewa na mamlaka husika wala hatua madhubuti kuchukuliwa. Sheria za uchaguzi zinavunjwa lakini Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi, Jaji Lewis Makame ameamua kwa makusudi mazima kufumbia macho vitendo hivyo.
Jaji, sisi wapenda amani tukueleweje ?
Unataka kutupeleka pabaya ili iweje ?
Yakitokea japo machafuko utasemaje ?
Ya Kivuitu Kenya tupishie mbali ewe Jaji
Tuwe na amani Tarime, Mbeya hadi Ujiji
Tuishi bila hofu Rukwa, Geita hadi Rufiji.
Unataka kutupeleka pabaya ili iweje ?
Yakitokea japo machafuko utasemaje ?
Ya Kivuitu Kenya tupishie mbali ewe Jaji
Tuwe na amani Tarime, Mbeya hadi Ujiji
Tuishi bila hofu Rukwa, Geita hadi Rufiji.