Uchafu wa Uwanja wa Mkapa: Kusingizia Kongamano la Mwamposa ni uongo wa kijinga sana

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,377
217,440
Mamlaka husika isijaribu kumkufuru Mungu kwa kutengeneza hadithi ya kutunga kuhusiana na Uchafu uliokubuhu ndani ya Uwanja wa soka wa Mkapa.

Ukweli ni kwamba Wizara husika imeshindwa kabisa kusafisha uwanja huo wenye uwezo wa kuchukua watu elfu 60, kutokana na ubahili, uwezo mdogo wa viongozi, hulka tu ya uchafu ambayo imewajaa viongozi wa uwanja huo au Ushamba.

Wakati wa Kongamano la Mwamposa la VUKA KABLA YA KUVUKA, kulikuwa na kikosi kazi cha waumini waliojitolea kufanya usafi kwenye maeneo yote pamoja na Chooni, baadhi ya Waliojitolea kufanya usafi kwenye vyoo kwa usiku ule WALIBARIKIWA na kufanikiwa mambo yao baada ya Mungu kuwatendea, nimeona Ushuhuda wa Msafisha choo wa kujitolea kwenye kongamano lile, akidai kulipwa fedha alizokuwa anadai kwa muda mrefu, ambapo alidai Mungu alimfungulia milango baada ya kujitolea kusafisha vyoo.

Hii maana yake ni kwamba Mwamposa na kundi lake walikwishajipanga kwenye maswala yaliyohusu Usafi wa eneo lile na walifanikiwa.

Kwahiyo kushindwa kwa mamlaka husika kwenye usafi wa uwanja huo, wasimwangushie jumba bovu Mwamposa.
 
Karibu viwanja vyote vya soka ni vichafu, je huko nako Mwamposa alifanya kongamano? Tuache kujificha kwenye vichaka vifupi
 
Mamlaka husika isijaribu kumkufuru Mungu kwa kutengeneza hadithi ya kutunga kuhusiana na Uchafu uliokubuhu ndani ya Uwanja wa soka wa Mkapa...
Kweli kabisa. Hata pitch kuwa na vipara namna ile ni aibu tu. Kwanini kila tukio ni uwanja wa Mkapa? Mfano ile game ya jana watu wachache si wangecheza Chamazi au uhuru?

Waupumzishe ili nyasi ziote vizuri

Sent from my SM-A315F using JamiiForums mobile app
 
Mimi hoja yangu ni kwamba Watanzania kwa ujumla wetu tuna tatizo la usafi au kutunza mazingira yetu yawe Safi kama tulivyoyakuta, hasa hasa maeneo ya umma kama viwanja vya mpira, maeneo ya burudani, barabarani, kwenye vyombo vya usafiri nk. Hili kwangu mimi ni tatizo kubwa sana la kijamii lenye chanzo kwenye malezi, makuzi na hata vijana wetu wakiwa mashuleni na vyuoni.

Yaani ni kawaida sanaa kuona mtu mzima kabisa anakunywa maji, juice au anakula machungwa kutupa hovyo chupa au maganda ya matunda. Mtu anaendesha Harrier au BMW lakini anatupa chupa ya maji nje ya gari eti kuna mtu wa usafi atafanya, really?

Mtu yuko kwenye Bus amekula anachokula halafu mabaki yake badala ayatunze mpaka afike sehemu ya kuchimba dawa atupe, yeye anarusha tuu uchafu barabarani just like that!!Kwa hiyo nikirudi kwenye hoja yako hili ni tatizo kubwa sana la kijamii tulilonalo, unapoona Wajapani kwenye World cup kama kule Qatar na kwingineko mashabiki wanabaki uwanjani kuokota takataka kwenye kila mechi, hata pale wanapofungwa ni kwamba hiyo ni tabia yao iliyojengeka kuanzia nyumbani kwao, mashuleni kwao, vyuoni kwao, ma kazini na kwingineko.
 
Na wewe ni mjinga kiasi hiki!??..sikutaraji Ila sishangai,maana watenda maajabu wote ni WA huko kwenu nyanda za juu kusini,siku hizi huko hamtoi Tena wachezaji Waziri Kama zamani Bali manabii feki
Shambulia mada , usimshambulie mtoa mada .
 
Bora hata uwanja kuliko uchafu wa hizi ofisi
Geti lina kutu,madirisha vumbi, vyoo vichafu vimeziba, corrido zina buibui
20230201_132412.jpg
 
Back
Top Bottom