Uchafu mitaani Dar: Nani alaumiwe?

Nipo dar kwa siku yatano sasa nilichogundua hapa ni
1)Uchafu kuna uchafu wa kutisha lakini cha ajabu wakazi wake hawaushangai manake kama ni sehemu ya maisha yao. usishangae dar ukaona sufuria la supu katikati ya maji machafu ila watu wanakunywa na hawahofu.
2) Tatizo la usafiri hadi inakera hili lipo na litaendelea kuwepo.
3)Joto kama kawa.
Mkuu hujakamilisha orodha yako....jiji LINANUKA. Ukipita mitaani unasikia harufu ya inya kutokana na mifereji ya maji machafu ya choo kuelekezwa kwenye mifereji ya barabara. Kwa kweli ni aibu kubwa.
 
Mkuu ni kweli pita ferry ujionee kuna inzi wengi sana wanatishia afya za binadam hii ni kutokana na kitengo cha afya jiji kutokuwa makini kwa kupuliza dawa za kuua mazalia ya inzi ,pili mizoga ya samaki imeegeshwa getini hapo na kutoa maji yenye harufu kali .ukizingatia mabomba havatoi maji siku ya nne sasa ,pamoja na idadi kubwa ya wakaz bado wanaweza kutii taratib na sheria za usafi walizojiwekea hii inanipa picha kuwa mazingira haya wameyazoea
 
dar pana raha yake kuishi,
huko uswazi kwetu ukiwa sebuleni ni kama uko uwani
lakini maisha raha mustarehe,
 
Dar inanichefua kwelikweli. Natafuta kila njia nisiishi Dar. Nikisema Dar ni kuanzia Mlandizi hadi Ferry. Kute kunanuka.
 
kiukweli dar inanukaga, huo mji wameuzoea wenyewe, cc wa mikoani kama wanavyotuita hatupawezi
Dar inanichefua kwelikweli.
Natafuta kila njia nisiishi Dar. Nikisema Dar ni kuanzia Mlandizi hadi
Ferry. Kute kunanuka.
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom