Uchafu mitaani Dar: Nani alaumiwe?

Rev. Kishoka

JF-Expert Member
Mar 7, 2006
4,526
1,529
Chicken has come home to roost!

Hivi tutamlaumu nani? Mwenye nyumba, diwani, katibu kata, meya, halmashauri, mbunge, DC, mkuu wa mkoa Waziri wa afya, Nyumba, Tamisemi, Mazingira, miundombinu, Waziri Mkuu au Raisi?

Hivi tukipata mlipuko wa kipindupindu tutapona?

y1pIjS-ngexYeXV7nwaWZP_N-0VFv7ffipmATXHC1zBYkUmXFkz3GvJDJy988Egmko7pKf_-_nVDJc
 
Mimi nawalaumu wote maana ukichunguza kwa undani au hata kwa juu juu tu utagundua kwamba kila mmoja wa hao uliowataja wanahusika kwa namna moja au nyingine.
 
Mimi nadhani mwenye nyumba, kisha serikali za mitaa. Maana kama tatizo ni dimbwi basi wananchi wanaweza kujitokeza na kulijaza kifu, lakini kama tatizo ni mfumo wa maji machafu, then serikali ya mitaa ndio inanguvu na swala hilo.

Rev au tuwalaumi mafisadi nini?
 
Mimi nawalaumu wote maana ukichunguza kwa undani au hata kwa juu juu tu utagundua kwamba kila mmoja wa hao uliowataja wanahusika kwa namna moja au nyingine.
ASANTE NYANI....! WAKATI NAANZA KUSOMA HUKU NIKITAFAKARI JIBU MUAFAKA......NILIPITA ULIMOPITA....! HAKUNA WA KUBAKI.....WOTE HAWAJA-PLAY ENOUGH KTK HILI.....LAWAMA ZIWAANGUKIE WOTE NA WOTE WAFANYE YANAYOWAPASA KUFANYA......NA SI KULAUMIANA KAMA ILIVYO JADI YETU....!
 
Kama kawaida yetu tunatafuta wa kulaumu badala ya kutafuta suluhisho, kwa mtindo huu basi mimi nasema tuwalaumu mafisadi wa Buzwagi, Richmond na waliokwiba pesa za EPA na waliokopa NSSF na hawajalipa hadi leo!:mad::(
 
Mimi natupia lawama viongozi. Nchi zote ambazo sasa hivi tunaona kuwa ni kioo cha usafi, hazikuwa siku zote hivi. Singapore ilikuwa bandari masikini na chafu kwa kila jinsi walipopata uhuru.

Ni uongozi wao waliochukizwa na hali hiyo na kuweka sheria ambazo zilimwadhibu raia yeyote atakayeendekeza uchafu. Miji ya uingereza, ufaransa yote nayo ilikithiri kwa uchafu mpaka utawala ulipopitisha sheria ili kukabiliana na milipuko ya magonjwa iliyokuwa kama tija wakati ule.

Ni mlipuko wa mara kwa mara wa Cholera ndiko kuliwafanya wenzetu wapitishe sheria ambazo kwanza zililazimishe local authorities wajenge sewer systems na wakazi wote wa mjini kuunganisha kwenye hizo sewers! Wananchi walipinga sana wakiona kuwa ni utawala wa ubabe lakini utawala ulishinikiza mpaka hali ikakubalika. Bila uongozi ulioamka hamna kitakachofanyika.

Hali hii ya uchafu kukithiri mara nyingi ni mijini na sio vijijini. Vijijini kila mwenye nyumba anawajibika katika sehemu yake na hapo awali sehemu kubwa ya uchafu uliokuwa ukizalishwa ulikuwa ni bio-degradable. Hapa mjini hakuna mwenye mji na bila uongozi kuweka sehemu na taratibu za kukabiliana na hali hii hakuna ambacho mwananchi wa kawaida anachoweza kufanya.

Kama hakuna taratibu za kukusanya taka, mwananchi aishie katikati ya mji ni vigumu kuchimba shimo la kutupia taka zake. Ziwekwe taratibu na kuhakikisha kuwa zinafuatwa. Bahati mbaya taratibu hizo zinafanywa dili kiasi cha kumuondolea mwananchi hamu ya kuzitumia!
 
Rev. Kishoka,

Hapo sisi wote tunawajibika na matatizo ya TZ. Kila mmoja wetu au wengi wetu tukitimiza wajibu wetu, Tanzania itasonga mbele.

Watu hapa wajuzi wa kuandika makala ndefu kulaumu wengine lakini ukifuatilia unagundua wengi hatuna tofauti na hao tunaowalaumu.

Sirikali ikitimiza wajibu wake, ni kweli maendeleo yatakuja haraka. Lakini je serikali ikilala, kwanini na sisi wananchi tulale?

Kwa kushirikiana mmoja mmoja, wawili wawili, tunaweza kabisa kuondoa hilo tatizo.

Huko nyuma niliwahi kuandika jinsi jamaa mmoja alivyoweza kuondoa tatizo sugu kwa solution rahisi sana huko kwao baada ya kutoka Ulaya. Alichoshwa na uchafu uliokuwa unazunguka maeneo yao pamoja na kwamba watu wote waliokuwa wanaishi huko walikuwa watu wenye kipato na nyumba za maana. Yeye alianza kwa kuwashawishi watu wachache ili watumie vijana waliokuwa wanakaa bure kukusanya takataka na kwenda kuzitupa mbali. Baada ya muda watu karibu wote wa eneo hilo wakajiunga na vijana pia wakaanzisha kikundi chao cha kukusanya takataka kwa mikokoteni.

Sio optimum solution lakini ilifanya kazi na kila mtu akawa happy. Wangeendelea kusubiri serikali, mpaka leo wangekuwa wanasota na uchafu.

Wakati mwingine mukiiumbua serikali hivyo, inaweza kushutuka na kufanaya kweli.

Mbona kwenye elimu hatuisubiri serikali? Mbona tunapeleka watoto wetu kwenye mashule ya bei mbaya wakati ni wajibu wa serikali kutoa elimu kwa raia wake? Hivyo hivyo hata kwenye afya. Kwanini tunashindwa kwenye mambo mengine?

Watu wakitoa pesa zao, itafika mahali watasema hapana, na kuamua kuwabwaga wanasiasa ambao hawafanyi kitu. Uchafu unaua ndugu zetu, kulalamika peke yake sio solution kabisa.
 
Wakati mwingine mukiiumbua serikali hivyo, inaweza kushutuka na kufanaya kweli.

Mbona kwenye elimu hatuisubiri serikali? Mbona tunapeleka watoto wetu kwenye mashule ya bei mbaya wakati ni wajibu wa serikali kutoa elimu kwa raia wake? Hivyo hivyo hata kwenye afya. Kwanini tunashindwa kwenye mambo mengine?

Serikali yetu kwa muda mrefu imekuwa ikipata free ride kutoka kwa wananchi. Hakuna sehemu ya huduma ambayo imeona inawajibika kuanzia usalama wa raia(sungusungu), kinga za moto(imekuwa biashara ya machinga kwa wenye uwezo), shule ( private) hospitali (private) na mengineyo. Hao wananchi wakikusanya huo uchafu watautupa wapi maana dampo zimegeuzwa makazi? Kwa wenye uwezo kuwatoa watoto wao kwenye shule za serikali ndiko kulikochangia kwa kiasi kikubwa kudumaa kwa sekta ya elimu.

Kwa wenye uwezo kupelekwa India, Uingereza na Marekani ukiachilia Hindu Mandal n.k. kumechangia kushuka kwa huduma za hospitali za serikali. Kwa wenye uwezo kuweza kuweka walinzi private kumechangia hali iliyopo katika vyombo vyetu vya usalama ambako huko mitaani mwananchi anaambiwa nenda kamlete mbaya wako hapa poli post. Kwa wenye uwezo kuweza kununua mashangingi kumefanya hali za barabara zetu kuwa kama zilivyo.

Kwa wenye uwezo kuweza kujiwekea self konteina kwenye maofisi kumefanya hali ya vyoo vya wafanyakazi wa kawaida kuwa haisemeki. Inabidi wanachi waanze kudai huduma stahili kutoka kwa hao wanaowachagua kuwaongoza maana ni kodi yao itakayotumika.
 
BBC News Online: World: Africa

--------------------------------------------------------------------------------
Wednesday, 23 May, 2001, 15:08 GMT 16:08 UK
Tanzania's private fire fight


By Roger Dean in Tanzania
Dar es Salaam, Tanzania, now has four new fire engines standing by for emergencies.



--------------------------------------------------------------------------------

--------------------------------------------------------------------------------
If the person will not sign we may watch a building burn
Knight Support spokesman

--------------------------------------------------------------------------------
But these vehicles are not owned by the Tanzanian Government, and represent a new approach to public services in the city.
They belong to Knight Support, a private security firm which now has the first privately-owned fire service in the country.

They have just shipped in four fire engines from the UK, trained their staff, and now say they have the most efficient fire service in East Africa.

Subscription only

Customers pay a monthly subscription of just over $100, so the service is accessible on to businesses and the well-heeled.

Everyone else either has to stump up a huge call-out fee, or rely on the government fire service.

Knight Support spokesman John Kagaruki insists that lives will not be put at risk due to their business tactics.

"Human lives come first," he says, "but otherwise, if the person will not sign we may watch a building burn."

The new service is also to provide backup to the state fire brigade when requested, but again bills will be in the post.

"We have the equipment to assist and will help," Mr Kagaruki says, "but, like the Dar es Salaam airport's fire team, we will charge for our assistance."

The Tanzanian government's free-wheeling economic liberalisation has only recently made this sort of private enterprise possible.

Over the past decade the policy of belt-tightening has saved Tanzania from bankruptcy, but the resulting lack of cash took its toll on public services.

Free market

Now the task of providing these services, until now the sole preserve of the state, is increasingly opening up to the free market.

Private hospitals have sprung up, in which patients have to pay for their treatment but at least know the medicines will be available.

Public utilities are being privatised left, right and centre.

A share in the telephone operator was sold recently. The railways and the beleaguered Dar es Salaam water authority are next. The hope is that private cash and business know-how can solve some of the problems.

Knight Support's relationship with the Dar fire brigade will be important to both parties.

The private company sees its role very much as a service to its customers first, and a backup to the official fire brigade second.

For its part the government service has pulled its socks up and is now arriving at fires quicker, conscious of Knight Support's presence.

Also, with the current rash of privatisations in Tanzania, it's possible that the contract to run the city fire service itself may be up for grabs, and a company like Knight Support could be well placed to apply.
Tanzania's free-enterprise revolution takes another small step.

Umachinga ninaouzungumzia kwenye biashara ya moto ni huu! Hawa wanapaki chini ya mwembe kungoja biashara. Nchi gani inayojiheshimu umeona hilo?
 
Fundi Mchundo

Unachoongelea ni chicken and egg scenario, nini kilianza kwanza? Shule zilikuwa mbovu kwanza na ndio watu wakahamisha watoto wao au watu walianza kuhamisha watoto wao kwasababu shule zilikuwa mbovu? Mimi nafikiri
shule zilianza kuwa mbovu.

Watu wakitaka kutafuta solution wataipata tu, kibaya ni hii tabia ya kukaa na tatizo bila kuhangaika na kufikiri. Hicho ndio kinatokea TZ kwenye mambo mengi ikiwemo suala la uchafu.

Hata suala la maji, kuna solutions ambazo watu 20 wakikaa pamoja wanaweza kugundua ni bora kuliko kusubiri shirika la maji lisilojali wateja.

Kitu ninachoongelea mimi ni kwamba, hakuna tatizo lisilo na jawabu. Mtu ukikaa kimya na kusubiri mtu mwingine aje akutatulie matatizo yako, jua umeshashindwa. Kama ni wajibu wa serikali sawa, lakini fanyeni jambo ili hiyo serikali iamke, au iangushwe. Vinginevyo utakaa na uchafu mpaka miaka mingapi?
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Mtanzania,

Mimi bado natofautiana na wewe. Solution za kutegemea wananchi zinafaa vijijini lakini si mijini. Vijijini wana njia zao za kuhakikisha kuwa kila mtu anawajibika. Mama mwenye nyumba chafu kwa mfano binti yake hapati mchumba. Huko ndiko solution kama kuchimba visima ili wakabiliane na shida ya maji kunawezekana. Solution hizi hazitafanya kazi mijini kwa sababu kuu mbili:

1. Miji haina wenyewe kwa hiyo zile taratibu za kuwekana sawa kijijini hazifanyi kazi. Mama mchafu anaweza kumpatia mchumba mwanae bila shida yeyote kama vigezo vingine vinavyothaminiwa mjini (pesa, uzuri n.k.) atakuwa navyo. Vile vile mjini anaweza kukuta watu ambao hawaoni uchafu kuwa ni tatizo.

2. Mlundikano wa watu mjini unahitaji usimamizi na utaalamu ambao mtu binafsi hatokuwa nao. Mahali kama Manzese hata wajioganaiz vipi tatizo la maji litahitaji mamlaka husika kushirikishwa. Hauwezi kuchimba kisima maana kila sehemu ina mwenyewe na upatikanaji wa maji safi utahitaji matumizi ya mashine ambazo ziko nje ya uwezo wa wananchi wengi.

Tukitazama hili la uchafu, hata wananchi wa Manzese wafanye nini bila kuwa na chombo kitakachoweza kuukusanya huo uchafu na kwenda kuutupa mahali panapostahili, juhudi zao zitakuwa bure. Mfano angalia vile vitrela vya kuchukua uchafu vinavyo overflow. In desperation wananchi wamefikia hatua ya kuchoma bila kuangalia madhara ya moshi ulio na sumu! Wengine wanawalipa watoto wa mjini kuchukua na kwenda kutupa taka hizo sehemu wanazojua wao.

Hii ndiyo inayonipelekea kusema kuwa katika mazingira ya miji ni lazima utawal uwajibike kwa kuweka nyenzo na system za kushughulikia suala la uchafu. Wakishafanya hivyo, ndiyo waweke bye-laws zitakazomwadhibu yeyote ambaye atasababisha uchafu maana hatokuwa na sababu. Singapore unalipa faini kama unatupa Big G chini, kama hauflush public toilet kwa sababu mapipa na vyoo havikosi maji kwa hiyo hauna sababu ya kufanya vinginevyo. Sehemu nyingi Ulaya wenye mbwa wana wajibika kukusanya choo cha mbwa wao kwa sababu sehemu ya kukitupia kiko kila sehemu. Mtu anayeacha kinyesi cha mbwa wake bila kukikusanya anaadhibiwa!

Utamlaumu vipi mtu kujisaidia nyuma ya mti kama hamna huduma ya vyoo vya umma? Utamlaumu vipi mtu kutupa maganda ya ndizi chini kama hamna sehemu ya kutupia? Na zaidi ya haya, utawalaumu vipi wote hawa kama hauwaadhibu wakifanya hivyo wakati vyoo vipo na vipipa vipo?

Miji inahitaji utawala unaowajibika ili ifanye kazi. Hili sidhani kama tunaweza kukwepa.
 
Last edited by a moderator:
Takataka barabarani....
y1pIjS-ngexYeXV7nwaWZP_N-0VFv7ffipmATXHC1zBYkUmXFkz3GvJDJy988Egmko7pKf_-_nVDJc


y1pIjS-ngexYeXeT80Md8FC0NvVc0ieIIpxAEi0RToNxdkWDvPLvOyrxM47O0xxs3nA21odvPzFQ6k


Wengine hupenda kutupa takataka kwenye mito...sijui pengine ni rahisi kwao..
y1pIjS-ngexYeWGeKlMqA_EOWltSNXjWMcDcY8rJypqE3w6vv1G4N6Ac2YjCIUd5C-PFLygBn7oEyE

Hata hivyo Usahau kuwa takataka wanazutupa kwenye mito huishia baharini au ziwani,ambako tunapata vitoweo vyetu
y1pIjS-ngexYeV3BDUd_AV8Zrdi3-wydjaSYexnYC1QY2TekhnAkc_F7qzZHimvKGlKY88v46NLJl0


y1pIjS-ngexYeUNBwt8FDlLCQWCR9dCTMJEPk9aaGCJSnEw6OfNdUcVcQkiS7K0TSwmWCt-JIYdS2A


Pamoja na juhudi za ujezi wa miundo mbinu... lakini sio wote wapendao kutupa taka zao katika sehemu zilizotengwa kwa ajili hiyo, badala yake....
y1pIjS-ngexYeXZcaGc6EmJ0Wn7iKb0XpLQwSrpGFGf61jTW-gVd8V1DVBA_ALx4MS_8o1HW8P1mEM


y1pIjS-ngexYeWoTMPLZUfaBBudiLUqjEBts5BaIZkyp_rHaDiNgd1lKcs39MC5LjnEAfsh4KdbIEc


Kwa wanaokerwa na tatizo la uchafu ni swala la uwamuzi tu, bila kusubiri serikali, kwani tatizo bado lipo kwenye elimu ya usafi..
y1pIjS-ngexYeUvnhLw6cu_IzrZAYyXpy6ATPoYRPXtQU_yj9IeJtDn7IZg2C0880j6h_yi6XiX-Hk


y1pIjS-ngexYeUR_DI1bSYAuJ2kknKvGGMPCupbVvIb3XA-9CT0WKBbHC51jDf9nZkSpCiT41T7fDo


y1pIjS-ngexYeX643ofpKsnqxDppLKFAGkxRfHpCfoBsv_o7K9fQxFJ2MwW3fUjgMaM2Pe9sOGILDk


Baada ya wananchi kuelewa ni wepesi kushiriki katika usafi..
y1pIjS-ngexYeXuxDIXUyCPpVnmvwLo8LQCWL0XurwzZVpO5HnhjKnFWB0RGUUyzXDbU65AKtq29nA


y1pIjS-ngexYeXM-vLxvHCzJinSg3n9AzHNhxiZ5NBvkb6D0qoPOOrLR97k3X7pceJD4amwhAdgd_8



Lengo ni kuwa na miji safi kwa Afya zetu na Mazingira kwa ujumla..
y1pIjS-ngexYeXpUMyzOXSdd3qpyOSAoWxLaLQz4dqKYM1Erf9Tg_T_y-WXHYUczYgXqOfsIC8j8ho


y1pIjS-ngexYeVHKfMB8FzEkLF4KF06CdXcWRpGkEtdCyLq6wdQDLBCnoHQsufbbKmBvRZI_6Y8Aik


y1pIjS-ngexYeXnD6n_DRfbOKQFjWrSyTcuaGmJZqlIVvrSuRXkNGhDC2ePdosKBu3tadZcVFlh5bc


y1pIjS-ngexYeVury11huKqrrtvPV4tytQ6f-Qc6UnJuzww770XR1mALXA1EtBCmE4o5hCZGjfqfS8


y1pIjS-ngexYeXZtrVQ9Ys17LQmlE_3sGaSRfSPq2jZFlMOJnWP1ZZtkx1o_4b3_e0U1PPRjWnA-yE
 
Ukiangalia hiyo picha ya nyumba na maji machafu utagundua kuwa si mvua ya siku moja tu ambayo imeleta uchafu mkubwa namna hiyo.

Kwa rangi ya tope, ni rahisi kubaini kuwa maji machafu ni kawaida kuizunguka hii nyumba mpaka kuna kuwa na algae. Angalia ule ukuta wa uzio, tayari umepata algae, angalia nyasi kubwa za kuzalisha mbu, si mvua ya siku moja inatosha kurutubisha nyasi hizo kwa kiwango kikubwa hivyo!

Jiulize, kipindupindu na malaria ambazo zitaikabili familia iliyoko kwenye nyumba hii, ni lawama kwa Serikali pekee?

Ni kweli killa mtu niliyemtaja anastahili lawama. Mwenye nyumba kwa kuendelea kuacha uchafu na maji machafu ya bafuni na chhoni yaendelee kumwagika mtaani, Diwani, kata na meya, kwa kukosa kutembelea maeneo yao na kuhamasisha usfai wa mazingira ama kutunga sheria, DC na Waziri kwa kushindwa kuhakikisha kuwa kuna mfumo bora wa miundombinu ambayo utajenga mabomba na mifereji ya chini ya ardhi ya kuondoa maji machafu, kushindwa kudhibiti ujenzi holela wa nyumba bila kufuata mipango miji kuhakikisha nyenzo na huduma muhimu zinapatikana katika maeneo haya, kushindwa kupitisha sheria kudhibiti uholela wa majumba na uchafu, kukosekana kwa utashi wa kupata maisha na afya bora.

Ni vigumu kupiga vita maradhi kama tutaendelea kuwa maskini wa mawazo na vitendo na kuachilia uchafu kama huu au hizi picha alizoonyesha Kibunango uendelee na kuzagaa.

Mbaya zaidi ni kujengwa kwa lile tabaka la wenye kustahili kuishi mahali safi (matajiri na wageni) ambapo Halmashauri za jiji hata Serikali huhakikisha usafi wa mitaa, mifereji, barabara unafanyika.

Ni jukumu letu sote kutaka kuishi mahali safi, pasipo na uchafu au harufu ya uozo. Mfano huu wa mtaani ni mdogo sana. Nenda masokoni, Tandale, Kisutu, Kariakoo na magenge mengine ambako ndipo unajinunulia chakula, hali za masoko haya ni taabani na hakuna mfumo bora wa uchukuzi wa takataka au kuwepo kwa maji safi na mifereji ya kuondoa maji machafu.

Si ufisadi au Comoro ambako tutalaumu Serikali kwa kushindwa kulazimisha usafi uwe kipaumbele. Ni lazima tuwe na utashi na kutaka mahali bora. Ni lazima tuwajibike kama familia, kata na jamii. Ikiwa wawakilishi na viongozi hawafanyi kazi zao, si kuna njia za kuwawajibisha kama kura?

Ni ajabu sana kuwa vijijini ambako tunadhani hakuna maendeleo au wako nyuma kwa kuwa wanakwenda kuteka maji maili moja na vyoo vyao vya shimo, wana usafi wa hali ya juu mara elfu kuliko ndugu huyu wa Mwananyamala au hizo picha nyingine.

Swali ni hili, ikiwa Vijijini tunakuona shamba na kuna utaratibu na uratibu bora, kwa nini basi tusimrudishe huyu ndugu na wengine wa mijini huko vijijini wakajifunze Usafi kwa nyenzo nyepesi?
 
Mkuu Kibunago,

Pamoja na kuniondolea appetite ni lazima nikushukuru kwa hizo picha na hasa kwa kuweka contrasts humu humu nchini kwetu.

Ukiangalia kwa makini utaona kuwa uchafu unalundikwa kwenye no man's land, kuanzia mini dampos hadi open drains. Hivi kama kweli hao waliopewa mandate ( wako jamani) ya public health wangewajibishwa hii hali ingekuwepo? Wangewajibishwa si kwa kushindwa kuondoa uchafu bali kutokua na mipango ya kukabiliana nao! Hao askari wa jiji ambao wanafukuzana na machinga wangemwagwa katika maeneo yenye open drains permanently na kuwajibika kuhakikisha hakuna taka inayoingia humo.

Hizo operesheni usafi ziwe za kudumu na si kwa kuleta watu kutoka nje kufanya usafi bali kuwalazimisha wakazi na watumiaji wa maeneo husika kuwajibika!

Iko kazi kweli.

P.S. Hivi huo mji wa pili ni Mwanza au Dodoma?
 
Rev. Kishoka

Kweli tupu, Mkuu.

Lakini huyo anayeishi karibu na hayo maji angefanya nini? Ajaze kifusi au ahame? Hapo zamani palikuwa na kamto kanapeleka maji ya mvua naturally kutoka sehemu za msasani, kijitonyama kupitia bwawa lachumvi na kuendelea msasani mikoroshini hadi baharini. Wakubwa wakajaza kifusi bwawa la chumvi na kugawana viwanja. Pale ambapo maji yalijitahidi kupita nakwenyewe waliziba wakagawana viwanja. Wenye mamlaka wakawapa ofa na building permits. Kazi imebaki kwa hao walalahoi ambao maji kwao sasa yana simama hayana mahali pa kwenda. Katika vitongoji palikuwa na sehemu za wazi ambazo wananchi waliweza kutupa taka ( si hygienic lakini aheri kuliko hii ya sasa) lakini hao hao wenye mamlaka wamegawa sehemu hizi kwa wenye nazo. Hizi sehemu zingefaa kuwa collection points, sasa hazipo. Mimi ndiyo maana sehemu kubwa ya lawama nawatupia wao. wao ndiyo wanaotakiwa kuongoza development ya miji yetu bila kuathiri afya za wakazi wake na hawafanyi hivyo. Hao health inpektas kwa nini wasifunge hayo masoko mpaka hali iwe ya kuridhisha? Haya ya siku moja katika mwaka kugawana T-shirt, kuimba ngonjera na kugawana vijibahasha na kufagia vijisehemu hakuta tufikisha mbali!

Niliwahi kusimuliwa kuwa kuna wakati huko Makutupora JKT kuna kijana alijisaidia nje ya bweni kwa kuogopa kwenda kwenye vyoo vilivyokuwa mbali. walipoulizwa hakuna aliyekiri kufanya kitendo hicho. basi afande akawaagiza wote waishio kwenye bwalo hilo kuwa ikifika wakati wa disko jioni kila mmoja amuonyeshe kipande cha ule mzigo kwenye kiganja chake ama sivyo wataipata. Kwa vile afande yule alikuwa anajulikana kwa suluba, watu ilibidi wamegeane ule mzigo. Toka hapo hakuna aliyerudia tena mchezo huo wakijinga!
 
Last edited by a moderator:
Pamoja na udahifu wa serikali zetu za mitaa na ungozi usafi uchafu pia ni hulka na silka za mtu!
 
Fundi,

Nimejiuliza, hivi Mkubwa wa nchi akiziona hizi picha zimechapisha kwenye magazeti na wakati wa kikao cha baraza la mawaziri akasema "I do not want to see this again" will the reaction be to stop publication and taking more pictures by Waziri wa Habari or efforts to clean the area?

Msichape hizi picha zimemkasirisha Rais na kuliaibisha Taifa, I believe will be the reaction top down kutoka kwa viongozi na si kuhakikisha kuna mipango bora ya kuondoa takataka!
 
Fundi,

Nimejiuliza, hivi Mkubwa wa nchi akiziona hizi picha zimechapisha kwenye magazeti na wakati wa kikao cha baraza la mawaziri akasema "I do not want to see this again" will the reaction be to stop publication and taking more pictures by Waziri wa Habari or efforts to clean the area?

Msichape hizi picha zimemkasirisha Rais na kuliaibisha Taifa, I believe will be the reaction top down kutoka kwa viongozi na si kuhakikisha kuna mipango bora ya kuondoa takataka!

Touche, Mkuu! Inawezekana kabisa na wale waliopiga wakachukuliwa hatua!!!
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom