Ubunifu zaidi unahitajika katika bidhaa zetu za ngozi

Sky Eclat

JF-Expert Member
Oct 17, 2012
57,595
215,272
Mwanzoni mwa mwaka huu katika kusherehekea kutimiza kwangu miaka 20 tangu nizaliwe, nilipata zawadi ya mkoba kutoka katika viwanda vya hapa kwetu. Mkoba ni nadhifu sana, bidhaa za ngozi huwa zinadumu kwa muda mrefu. Kasoro kubwa ilikua kwenye kumalizia, hadhi ya zipu hailingani na ubora ya mkoba.

Kama nilivyosema awali bidhaa za ngozi ni imara sana. Kuipa heshima bidhaa ya ngozi zipu na vifungo ni lazima viwe kwenye ubora unaondana na thamani ya bidhaa.

Ni vigumu kubuni mtindo wa pochi na ukubalike na wengi sokoni. Watengenezaji wwngi wanaiga mitindo ya wabunifu wakubwa kama Yve Saint Laurent (YSL), Gucci, Channel na baadae wakina Kelvin Claine ba DKNY wanatoa toleo kwa bei nafuu zaidi.

Wabunifu wetu wawe wanafuatilia matoleo ya wabunifu wakubwa ili kuvutia soko. Zipu zianaweza kuagizwa kutoka Uturuki au China, mradi ziwe zenye ubora. Unaweza kuweka kichwa cha zipu chenye logo ya kampuni. Hapa hata mshona viatu hawezi kuiga.

Hali kadhalika kwa mikanda ya kiume na ya kike. Pamoja na makubazi ya kike na ya kiume.

1624088132183.jpeg
 
Kitu kingine, ngozi zetu ni ngumu sana. Naona hatuna ujuzi wa kutosha wa Tanning. Ukiangalia mikanda na sandal wanauza wamasai ni vigumu sana. Pia 'lock' za mikanda hazivutii kabisa. Kwa ngozi ile ukitengeneza wallet itakuwa inatuna mfukoni balaa.

Tunahitaji sana ngozi bora, sijui Rostam na kiwanda chake cha Moro anatoa ngozi quality kiasi gani.
 
Hakika. Mimi ni shabiki wa vitu halisi. Kwa sasa ninashona baadhi ya nguo zangu kwa mafundi/wabunifu wetu hapahapa tz. Kwakweli wapo watz wanafanya vema. Kwa mfano, kuna kaunda suti moja nikiipiga, hata mwenyewe najiona ilivyonikaa. Binafsi ninaona hali ni mbaya zaidi kwa hizo bidhaa za ngozi. Umaliziaji na, kwa viatu, soli bado ni mtihani. Kuna jamaa pale Moshi, anatengeneza kiatu bomba sana, shida ni soli. Lakini, nimewadadisi, ukiacha udhaifu wao, serikali haijafanya juhudi za kuwalinda na kuwasapoti hawa watu. Kodi bado ni kubwa, vifaa vingi bado vinatoka nje, na havina ubora.
 
Back
Top Bottom