Ubunge wa Viti Maalum hauna faida kwa Taifa

Mwanapropaganda

JF-Expert Member
Aug 19, 2014
4,235
2,501
Nimeona mwaka huu wanawake wale wasiojiheshimu na waliopoteza heshima kwenye jamii wanatangaza nia ya kugombea ubunge wa viti maalum.

Kuitwa mbunge kunaenda sambamba na kuitwa mheshimiwa, jina/cheo kinachoonekana kuwa na hadhi ya juu nchini Tanzania.

Kilichonishangaza ni kuwa watu waliojijengea picha mbaya kwenye jamii ndio wanaokimbilia kazi hiyo ya uheshimiwa! tunawezaje kuwa na waheshimiwa wasiojiheshimu?

Siku zote nidhamu ndio sifa ya kiongozi, hata mwanafunzi wa shule ya msingi anajua hivyo, ndio maana ili uweze kuwa kiranja wa shule au darasani unatakiwa kwanza uwe na sifa nzuri kama kielelezo kwa wengine, watu wajifunze kutoka kwako, Sasa hao watu wanawafundisha nini wanawake wenzao walioko kwenye jamii hasa watoto wetu wadogo?

Mtu ameshindwa kujikomboa kifikra atawezaje kukomboa wengine, mtu aliyepoteza dira ya maisha hawezi kuwapa dira ya kimaendeleo watu walio moyo wa kujituma.

Sasa hivi Tanzania siasa imekuwa rahisi ndio na kila mtu anayejiona ni maarufu anaweza kujiingiza ili kusaka fursa ya ubunge.

Katika uchaguzi mkuu ujao kutakuwa na idadi kubwa ya wanamuziki, wacheza filamu na vichekesho watakaotaka na wao kuwa wawakilishi wa nafasi ya viti vya ubunge huku wengi wa wanawake kukimbilia viti maalum.

Ni vyema vyama vya kisiasa kuhakikisha kuwa mchakato wa kupata wawakilishi viti maalum ukaangalia kwanza historia ya mtu kwenye jamii yake na uwezo wake kisiasa maana hakuna nafasi ya wananchi kuwapima kama walivyo wabunge wa kugombea majimboni ambao jamii inaweza kuwakataa kupitia sanduku la kura.

Ni afadhari tu kuviondoa viti maalum au kuwapa watu wenye ulemavu kama wafugaji na wakulima watakaowakilisha sekta zinauzotegemewa kwa ustawi wa uchumi wa nchi.

Wanawake sasa wanaweza, fursa zipo sawa kwenye elimu na ajira kwanini waendelee kukomalia viti maalum? tatizo la nchi yetu kitu kikishawekwa hakitolewi hata kionekane kimepitwa na wakati.

Siasa za vyama ndio inatuletea viongozi wa serikali, wabunge ndio wanakuja kuwa mawaziri.
Watu wanaopitishwa kuwa wabunge ndio hao hao watakaotutungia sheria.

Baadae msije mkalalamika kusikia kuna wabunge wanatetea hoja ya cameroun bungeni ili kuihalalishs iwe sheria, kumbe tatizo ni ninyi wenyewe ndio mliwapeleka huko.

Tunataka wabunge wenye nidhamu, uelewa mzuri na wanaojiheshimu.
 
Dawa yake imo katika KATIBA ya WANANCHI. Jiunge na teammabadiliko/teamlowassa na utapata jibu sahihi baada ya Oct 25. Sio tu viti maalum, bali pia wabunge wasiowajibika (walaghai) kwa wapigakura wao baada ya kuukwaa ubunge.

Nani amesema viti maalum vitaondolewa kwa kuwa havina tija?
 
Mpaka sasa najiuliza hili swali viti maalum imewekwa kwaajili ya kuongeza idadi au uwajibikaji?

Kuna maana gani kulazimisha idadi ya wanawake iwe sawa na ya wanaume bungeni bila sababu ya msingi?

Hawa viti maalum hakuna wanachofanya zaidi ya kelele nyingi za ndio na posho za vikao.

Sijui ni nani alitudanganya hii woman empowerment ni lazima wabunge wa kike wawe sawa na wakiume, kwani bunge linajadili mada za JINSIA?

Mimi nadhani kama mwanamke ana uwezo apambane kwenye uchaguzi kama wanawake wenzie akikosa basi atulie ajue wananchi hatumuhitaji,kwani kina Mdee nawengine wamewezaje?

Pia nadhani viti maalumu imekuwa njia ya wachache kuwekwa na ndugu zao na wapendwa wao na si wananchi.

Kwanza hawa wanacontroliwa na chama na si wananchi kwa hiyo sioni hadhi yao ya kuingia bungeni kama wawakilishi wetu labda kwenye mabaraza yao ya chama.

NASHAURI
Kufanyike marekebisho kwenye katiba viti maalumu viwe kwa wenye uwezo maalum/taaluma flani ili tuongeze idadi ya wataalamu hata kama ni wanaume na si kuchagua ili mradi mwanamke ambaye hana msaada wowote.
 
Kutokana namapungufu uliyoyataja, kama kweli tunahitaji viti maalum vya wanawake basi wasiteuliwe na vyama vya siasa bali watoke kwenye makundi mengine au wagombee kama independent women representatives.
A woman representative anaweza kugombea kutoka kwenye jimbo litakalowekwa kwenye ratiba na tume ya uchaguzi (siyo lazima kila jimbo liwe na woman representative).
Tume ya uchaguzi itapanga majimbo yatakayokuwa na women representatives kwa kufanya rotation.
Pia mwanamke akishapata hiyo nafasi mara moja, asiruhusiwe kugombea tena kama woman representative, labda agombee ubunge wa kawaida. Hii itawapa pia fursa ya kujifunza siasa kama wanaona uwezo wao wa kuingia front bila kubebwa ni mdogo.
 
Faida yake ni gender balance bungeni kwa mujibu wa uanzishwaji wake ila ukweli asilimia kubwa ni wadangaji wote.
.
Ukimpata mtoto wa bulembo anakuhonga V8 kudadadeki
 
Watu wamepata upenyo wa kujaza vimada na ndugu zao, kuna mambo yanafanyika nchi hii hadi unabaki kushangaa tu
 
Kama suala ni gharama, hakika tunagharamika sehemu nyingi tu. Suala la gharama nchi hii ni la kujitakia lakini pia labda turudie kule kule kwenye mabadiliko ya katiba. Wakuu wa wilaya na wakuu wa mikoa bila kujali jinsia zao wanafanya kazi gani ikiwa ma-ded wapo?...labda kuwe na ukomo wa nafasi hizi. Maana wimbo wa gharama umekuwa ni janga.
 
Hivi vililenga affirmative action;

Meaning efforts to promote the rights or progress of other disadvantaged persons eg women and disabled.
 
Mpaka sasa najiuliza hili swali viti maalum imewekwa kwaajili ya kuongeza idadi au uwajibikaji?

Kuna maana gani kulazimisha idadi ya wanawake iwe sawa na ya wanaume bungeni bila sababu ya msingi?

Hawa viti maalum hakuna wanachofanya zaidi ya kelele nyingi za ndio na posho za vikao.

Sijui ni nani alitudanganya hii woman empowerment ni lazima wabunge wa kike wawe sawa na wakiume, kwani bunge linajadili mada za JINSIA?

Mimi nadhani kama mwanamke ana uwezo apambane kwenye uchaguzi kama wanawake wenzie akikosa basi atulie ajue wananchi hatumuhitaji,kwani kina Mdee nawengine wamewezaje?

Pia nadhani viti maalumu imekuwa njia ya wachache kuwekwa na ndugu zao na wapendwa wao na si wananchi.

Kwanza hawa wanacontroliwa na chama na si wananchi kwa hiyo sioni hadhi yao ya kuingia bungeni kama wawakilishi wetu labda kwenye mabaraza yao ya chama.

NASHAURI
Kufanyike marekebisho kwenye katiba viti maalumu viwe kwa wenye uwezo maalum/taaluma flani ili tuongeze idadi ya wataalamu hata kama ni wanaume na si kuchagua ili mradi mwanamke ambaye hana msaada wowote.
Bunge la JMT lina meno 300+ ya kutafunia fedha ya wananchi. Ila Serikali ina meno mengi na makali zaidi ya Bunge.
 
Back
Top Bottom