Uchaguzi 2020 Ubunge Morogoro Mjini: Abood apitishwa kuwa Mgombea pekee. Wenzake wakosa vigezo

OKW BOBAN SUNZU

Platinum Member
Aug 24, 2011
49,191
103,713
Abdulazizi Abood (CCM) amepitishwa kama mgombea pekee katika Jimbo hilo baada ya wagombea wa upinzani kukatwa kwasababu ya makosa yaliyobainika kwenye ujazaji wa fomu

Abood.jpg

Msimamizi wa Uchaguzi jimbo la Morogoro mjini amewafutilia mbali wagombea wote wa vyama vya upinzani akiwemo Devotha Minja wa CHADEMA na kumbakiza Abdulaziz Abood wa CCM kuwa mgombea pekee, kwa madai kuwa wagombea wa upinzani walikosea kujaza fomu.

Tayari Msimamizi huyo amemtangaza Abood kupita bila kupingwa. Hii ina maana kuwa hatafanya kampeni wala kupigiwa kura bali atasubiri kuapishwa tu.

Wagombea waliokatwa ni wa CHADEMA, ACT Wazalendo, CUF na CHAUMA. Hata hivyo CHADEMA wamesema watakata rufaa kupinga maamuzi hayo.!
 
Msimamizi wa uchaguzi aache masihara kamanda wetu na jeshi lake ni waelewa, fomu hata kama zimekosewa zinaweza kujazwa upya hapo hapo ofisini.

Mgombea unaweza kwenda na fomu blank/ isiyojazwa mkakaa na Msimamizi ikajazwa vizuri na kuwakilishwa itakuwa hicho kinachoitwa 'imekosewa'!


Updates toka Morogoro


 
Nguvu ya Mafisadi huwa Ni kubwa Sana. Hongera Abood miradi yako ikaendelea kuwa salama
 
Hawajui wanatupigia promo, jambo dogo hilo mgombea kafika ofisini ndani ya muda muafaka, mchakato bado upo wazi kuweza kuweka mambo sawa.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro na msimamizi wa uchaguzi jimbo, Sheila Lukuba kada wa CCM afanya vitu vyake

Sheila Lukuba amefanya vitu vyake
 
Hivi hiyo ruzuku yenu mlishindwa kuandaa semina elekezi kwa wagombea wote jinsi ya kujaza fomu? Nyio ndio wa kuwapa nchi hii muongoze?
 
Back
Top Bottom