Ben Saanane
JF-Expert Member
- Jan 18, 2007
- 14,581
- 18,123
Mwenyekiti wa Chama cha Tanzania Labour (TLP), Augustino Mrema ambaye ameombwa kugombea ubunge Jimbo la Vunjo lililopo mkoani Kilimanjaro mwaka 2010 amekubali kugombea nafasi hiyo ikiwa atatakiwa hivyo na Mkutano Mkuu wa Chama hicho.
Akizungumza na waandishi wa habari juu ya kumwandikia barua Mrema ya kumtaka kugombea jimbo hilo, aliyewahi kuwa Mbunge wa jimbo hilo kati ya mwaka 2000 na 2005, Jesse Makundi alisema kuwa ameandika barua hiyo Februari 8 mwaka huu na kuikabidhi jana kwa Katibu Mkuu wa chama hicho, John Komba ili amkabidhi Mrema.
Alisema lengo la kumwomba kugombea nafasi hiyo, ni kutokana na mgawanyiko wa vyama vya upinzani ambao wameshajipanga kugombea jimbo hilo hali inayoonekana itaifanya CCM kupata ushindi jimboni humo.
Tayari Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi, James Mbatia ameshatangaza kugombea jimbo hilo na kwa mujibu wa Makundi, Mbunge wa Viti Maalumu wa Chadema, Susan Lyimo atagombea jimbo hilo mwaka 2010.
Kwa upande wake, Mrema aliliambia gazeti hili jana kwa njia ya simu akiwa mkoani Kilimanjaro kuwa yupo tayari kugombea nafasi hiyo ikiwa atapitishwa na Mkutano Mkuu wa Chama chake.
"Hilo jambo kubwa inabidi Kamati Kuu, Halmashauri Kuu na Mkutano Mkuu waangalie hali ya siasa nchini na baadaye Mkutano Mkuu utatoa uamuzi kama nigombee au nisigombee nafasi hiyo, mimi nitatekeleza maamuzi ya Mkutano Mkuu" alisema Mrema.
Akitoa sababu za kumtaka Mrema agombee nafasi hiyo, Makundi alisema amefikia uamuzi huo baada ya kuona katika jimbo hilo anahitajika mtu mwenye nguvu kisiasa ambaye ni tishio kwa CCM na mpambanaji asiyekata tamaa.
Mrema atakuwa Mwenyekiti wa nne kugombea nafasi ya ubunge. Tayari Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe ameshatangaza kugombea Jimbo la Hai, Mbatia atagombea Vunjo na kwa sasa Mwenyekiti wa UDP, John Cheyo ni Mbunge wa Bariadi Mashariki.
Source: HabariLeo
Akizungumza na waandishi wa habari juu ya kumwandikia barua Mrema ya kumtaka kugombea jimbo hilo, aliyewahi kuwa Mbunge wa jimbo hilo kati ya mwaka 2000 na 2005, Jesse Makundi alisema kuwa ameandika barua hiyo Februari 8 mwaka huu na kuikabidhi jana kwa Katibu Mkuu wa chama hicho, John Komba ili amkabidhi Mrema.
Alisema lengo la kumwomba kugombea nafasi hiyo, ni kutokana na mgawanyiko wa vyama vya upinzani ambao wameshajipanga kugombea jimbo hilo hali inayoonekana itaifanya CCM kupata ushindi jimboni humo.
Tayari Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi, James Mbatia ameshatangaza kugombea jimbo hilo na kwa mujibu wa Makundi, Mbunge wa Viti Maalumu wa Chadema, Susan Lyimo atagombea jimbo hilo mwaka 2010.
Kwa upande wake, Mrema aliliambia gazeti hili jana kwa njia ya simu akiwa mkoani Kilimanjaro kuwa yupo tayari kugombea nafasi hiyo ikiwa atapitishwa na Mkutano Mkuu wa Chama chake.
"Hilo jambo kubwa inabidi Kamati Kuu, Halmashauri Kuu na Mkutano Mkuu waangalie hali ya siasa nchini na baadaye Mkutano Mkuu utatoa uamuzi kama nigombee au nisigombee nafasi hiyo, mimi nitatekeleza maamuzi ya Mkutano Mkuu" alisema Mrema.
Akitoa sababu za kumtaka Mrema agombee nafasi hiyo, Makundi alisema amefikia uamuzi huo baada ya kuona katika jimbo hilo anahitajika mtu mwenye nguvu kisiasa ambaye ni tishio kwa CCM na mpambanaji asiyekata tamaa.
Mrema atakuwa Mwenyekiti wa nne kugombea nafasi ya ubunge. Tayari Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe ameshatangaza kugombea Jimbo la Hai, Mbatia atagombea Vunjo na kwa sasa Mwenyekiti wa UDP, John Cheyo ni Mbunge wa Bariadi Mashariki.
Source: HabariLeo