Ubovu wa barabara Kisukulu Maji Chumvi - Segerea ni kero kubwa

Ndugu wanajamvi Nawasalimuni kwa jina la jamhuri ya muungano.

Nimeona niamke na hoja hii kwani wakazi wa kisukulu tumejikuta kwenye mateso ya muda mrefu. Kwa wale wasiojua kisukulu ni wapi, Kisukulu ni kata inayoangukia kwenye jimbo la uchaguzi la segerea wilaya ya ilala kwa utambulisho zaidi naweza kusema Tabata kisukulu.

Iko hivi. Ukiwa unatokea mabibo external (Mandera road) kuna njia ya lami inayoelekea tabata kimanga,Kimara korogwe,kisukulu na segerea kupitia jeshini.

Ukiendelea mbele kuna daraja maarufu (maji chumvi) pale barabara ya lami inachepuka kwenda kutokea kimara korogwe hiyo yote ni lami,lakini mara baada ya kuvuka daraja ukinyosha kuna barabara ya vumbi ambayo inaenda kuunganika na barabara ya lami (bonyokwa segerea). Hicho kipande japokuwa ni kiungo muhimu sana ni kibovu sana na kinaharibu magari na kusababisha hasara kubwa hasa eneo korofi sana ni pale panapoitwa KAGENYI.

Mbali na kuharibika kwa magari,ikitokea gari limepakia mgonjwa au mama mjamzito au vifaa vyovyote vinavyohitaji uangalifu, unaweza kujikuta umesababisha matatizo zaidi ya lengo lako la kutoa msaada.

Ndugu zangu, kufuatana na barabara hii kuwa ni mkato na inarahisisha kukwepa foleni za magari (Buguruni) yanayotokea
Ubungo kwenda segerea, kinyerezi, majumbasita, kitunda kuelekea Gongo la Mboto na viunga vyake mpaka majohe
Tumejikuta wananchi wa Tabata kisukulu hata tulipojitahidi kutumia nguvu zetu kuziba hayo mashimo haichukui muda kuharibika
kufuatia wengi wa magari yanayotumia njia hii.

Andiko hili lina lengo la kuomba msaada kwa mamlaka husika,kwamba pamoja na ahadi zilizowahi kutolewa
kwamba DMDP watashughulikia, tunaomba matengenezo ya muda mfupi kwa kuweka kifusi angalau barabara ipitike kirahisi.
Pia kuwatahadharisha wakazi wa kitunda, Gongo la Mboto n.k wenye magari madogo wasije haribu magari yao kwa kutafuta njia mkato.

Baba yetu Mh.Isdori Mpango, waumini wenzako tuliosali wote kigango cha Mazda tukitokea kisukulu kwa sasa ni ngumu kufika kama unatumia gari inabidi uende parokia ya makoka japo kuna umbali.

Tunakuomba utuangalie kwa jicho la huruma ututoe kwenye mateso haya. Pia ndugu yetu Mh. Chongolo ,Tunakuomba pia uliangalie jambo hili utusaidie.

Nawashukuru sana ndugu zangu kwa kusoma.

Kazi iendelee.




YAANI NI KERO SANA HALAFU HICHO KIPANDE HAKIFIKI HATA KM 4, SIJUI NI NI TATIZO TUMEWAKOSEA NINI HASA WEE KIBONA?
 
YAANI NI KERO SANA HALAFU HICHO KIPANDE HAKIFIKI HATA KM 4, SIJUI NI NI TATIZO TUMEWAKOSEA NINI HASA WEE KIBONA?
Kibona ndo nani? au unamaanisha Mh.bona ambaye ndo mheshimiwa mbunge wetu wa jimbo la segerea?
 
YAANI NI KERO SANA HALAFU HICHO KIPANDE HAKIFIKI HATA KM 4, SIJUI NI NI TATIZO TUMEWAKOSEA NINI HASA WEE KIBONA?
Sio km 4 pale ni umbali wa km 1. Mie ndio maeneo yangu ya kukimbia mazoezi napita kuanzia Korogwe naenda mpk jeshini nakurudi na siku nyingine uwa napita hilo boda la vumbi naenda kugeuzia Segerea
 
Sio km 4 pale ni umbali wa km 1. Mie ndio maeneo yangu ya kukimbia mazoezi napita kuanzia Korogwe naenda mpk jeshini nakurudi na siku nyingine uwa napita hilo boda la vumbi naenda kugeuzia Segerea
Uyasemayo ni kweli kiongozi,hicho kipandeni kifupi sana ni suala la maamuzi(utashi wa kisiasa).
Ukiangalia umuhimu wa hii barabara,ilitakiwa hata kama si kuweka lami basi uhudumiwe kwa kuweka kifusi
ili kuwarahisishia raia wote wanaoitumia kupata riziki za kila siku.

Kuna mjumbe kasema barabara imebanwa sana,yaani watu wamejenga barabarani, ila ukweli ni kwamba ukiangalia hii barabara
na zile za mfano buguruni kwa mnyamani,na nyingine za mitaa kule temeke zilizorekebishwa huoni kama ufinyo wa barabara sio hoja.
Chukulia mfano sasa hivi ambapo pamoja na ubovu wake magari yanapishana makubwa kwa madogo,je si ikitengenezwa itakuwa bora zaidi.
 
Ndugu wanajamvi Nawasalimuni kwa jina la jamhuri ya muungano.

Nimeona niamke na hoja hii kwani wakazi wa kisukulu tumejikuta kwenye mateso ya muda mrefu. Kwa wale wasiojua kisukulu ni wapi, Kisukulu ni kata inayoangukia kwenye jimbo la uchaguzi la segerea wilaya ya ilala kwa utambulisho zaidi naweza kusema Tabata kisukulu.

Iko hivi. Ukiwa unatokea mabibo external (Mandera road) kuna njia ya lami inayoelekea tabata kimanga,Kimara korogwe,kisukulu na segerea kupitia jeshini.

Ukiendelea mbele kuna daraja maarufu (maji chumvi) pale barabara ya lami inachepuka kwenda kutokea kimara korogwe hiyo yote ni lami,lakini mara baada ya kuvuka daraja ukinyosha kuna barabara ya vumbi ambayo inaenda kuunganika na barabara ya lami (bonyokwa segerea). Hicho kipande japokuwa ni kiungo muhimu sana ni kibovu sana na kinaharibu magari na kusababisha hasara kubwa hasa eneo korofi sana ni pale panapoitwa KAGENYI.

Mbali na kuharibika kwa magari,ikitokea gari limepakia mgonjwa au mama mjamzito au vifaa vyovyote vinavyohitaji uangalifu, unaweza kujikuta umesababisha matatizo zaidi ya lengo lako la kutoa msaada.

Ndugu zangu, kufuatana na barabara hii kuwa ni mkato na inarahisisha kukwepa foleni za magari (Buguruni) yanayotokea
Ubungo kwenda segerea, kinyerezi, majumbasita, kitunda kuelekea Gongo la Mboto na viunga vyake mpaka majohe
Tumejikuta wananchi wa Tabata kisukulu hata tulipojitahidi kutumia nguvu zetu kuziba hayo mashimo haichukui muda kuharibika
kufuatia wengi wa magari yanayotumia njia hii.

Andiko hili lina lengo la kuomba msaada kwa mamlaka husika,kwamba pamoja na ahadi zilizowahi kutolewa
kwamba DMDP watashughulikia, tunaomba matengenezo ya muda mfupi kwa kuweka kifusi angalau barabara ipitike kirahisi.
Pia kuwatahadharisha wakazi wa kitunda, Gongo la Mboto n.k wenye magari madogo wasije haribu magari yao kwa kutafuta njia mkato.

Baba yetu Mh.Isdori Mpango, waumini wenzako tuliosali wote kigango cha Mazda tukitokea kisukulu kwa sasa ni ngumu kufika kama unatumia gari inabidi uende parokia ya makoka japo kuna umbali.

Tunakuomba utuangalie kwa jicho la huruma ututoe kwenye mateso haya. Pia ndugu yetu Mh. Chongolo ,Tunakuomba pia uliangalie jambo hili utusaidie.

Nawashukuru sana ndugu zangu kwa kusoma.

Kazi iendelee.
Aisee ni kweli kabisa.ile njia ni mbaya sana kabisa. kimsing ni shortcut nzuri sana ya kwenda airport na ukonga kutokea ubungo ukitaka kukwepa folen ya Dampo,Buguruni,tazara Vingunguti na kipawa
 
Hiii barabara inakera sana, mbaya zaidi Mbunge wetu kazi kupigwa Katerero tu mpaka kutalikiwa. Yaaani kutoka maji chumvi hadi migombani unahisi gari lote limekuwa screpa kwa mashimo.
WanaSegerea tuna jambo letu 2025 ngoja mbunge aendeleze drama.
 
Hiii barabara inakera sana, mbaya zaidi Mbunge wetu kazi kupigwa Katerero tu mpaka kutalikiwa. Yaaani kutoka maji chumvi hadi migombani unahisi gari lote limekuwa screpa kwa mashimo.
WanaSegerea tuna jambo letu 2025 ngoja mbunge aendeleze drama.
Hivi hakuna tunaloweza kulifanya kabla ya 2025?
Ndo maana kwenye uzi wangu nikamtaja VP Mh.Dr.Philip mpango,huyu alikuwa mwenzetu tukisali naye kigango cha Mazda pale, nikamtaja mh.Chongolo katibu mkuu wa ccm alikuwa mwanakisukulu mwenzetu,Leo Mungu amewainua hawawezi kutusaidia tukiwalilia?
na kimsingi ni maboss wa huyu mbunge ambaye haoni kama haya yanamhusu.
Hivi ni kweli wanakisukulu na watumiaji wote wa barabara hii kama short cut ya kuwahi uwanja wa ndege tunahitaji kusubiri 2025? kwenye box la kura?
 
Kiongozi wenye msemo huu hawana mbunge wa ccm,Kisukulu kuanzia wajumbe ,diwani mpaka mbunge ni ccm.
Kimsingi slogan ya mafiga matatu ilitendewa kazi lakini mateso kwa kwenda mbele.
Mwendazake alisema, wote kawabeba hakuna alieshinda uchaguzi, unategemea ufanisi? chadema hawapo sasa mpo wenyewe.
 
Ngoja nipitie kwa Dr Mangali hapa nimeze paracetamol,maana mpaka mwili unauma kwa mitikisiko ya hiyo barabara..
Pole sana mkuu,hukusoma taadhari niliyoitoa au ulipitia kujionea kwa macho yako mwenyewe😁😁
Wanakisukulu bado tunapiga moyo konde kwamba siku moja mamlaka husika zitatusikiliza na kulipatia suala hili ufumbuzi.
 
Mwendazake alisema, wote kawabeba hakuna alieshinda uchaguzi, unategemea ufanisi? chadema hawapo sasa mpo wenyewe.
Ni kweli tupo wenyewe,na ndo maana tunajaribu kupiga kelele ili watusikilize.
Chukulia mfano mnapokuwa kwenye daladala umesimama.ikitokea mtu akakukanyaga kwa bahati mbaya
na kwa kuwa haoni akaendelea kukanyaga mguu wako lazima umshtue ili ajue anakuumiza na mara atahamisha mguu wake.
Ni kweli mpo ndani ya daladala moja lakini aliyekanyagwa ni wewe na usiposema utaumizwa.
 
Dah,:rolleyes::rolleyes:,kiongozi hii umetoa kali lakini umenisaidia,
sasa naanza kupata mwanga,ila nina swali kidogo,kwani serikali nayo inalogwa?
weeee! Jaribu kuembelea huko ujifunze kitu anzia kwenye hicho kiduka cha mbena uone..
Sirikali si ni watu bana??tena wanaenda chooni kushusha makubwa waliyo shiba vya wizi? Au unadhani ni nini??
 
weeee! Jaribu kuembelea huko ujifunze kitu anzia kwenye hicho kiduka cha mbena uone..
Sirikali si ni watu bana??tena wanaenda chooni kushusha makubwa waliyo shiba vya wizi? Au unadhani ni nini??
Funguka zaidi maana maana sijakupata vizuri point yako.
Kwani pale mbena si anapanga? au ni nyumbani kwake,na kama ni issue ya
ufinyu wa barabara,mbona buguruni kwa mnyamani kumetengenezwa na vichochoro vingi kule temeke
iweje kisukulu ndo ufinyu wa barabara uwe issue kubwa kiasi kwamba barabara haitengenezwi. Pia najaribu kuunganisha dots kati ya uchawi na ubovu wa barabara nashindwa kupata majibu ndo maana nakuomba ufunguke zaidi.
 
Funguka zaidi maana maana sijakupata vizuri point yako.
Kwani pale mbena si anapanga? au ni nyumbani kwake,na kama ni issue ya
ufinyu wa barabara,mbona buguruni kwa mnyamani kumetengenezwa na vichochoro vingi kule temeke
iweje kisukulu ndo ufinyu wa barabara uwe issue kubwa kiasi kwamba barabara haitengenezwi. Pia najaribu kuunganisha dots kati ya uchawi na ubovu wa barabara nashindwa kupata majibu ndo maana nakuomba ufunguke zaidi.
funguka!! funguka mpaja saa ngapi bana weee!!! jiongeze. Af punguza kunywa uji asubuhi
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom