dali kimoko
Senior Member
- Jan 25, 2021
- 114
- 138
Ndugu wanajamvi Nawasalimuni kwa jina la jamhuri ya muungano.
Nimeona niamke na hoja hii kwani wakazi wa kisukulu tumejikuta kwenye mateso ya muda mrefu. Kwa wale wasiojua kisukulu ni wapi, Kisukulu ni kata inayoangukia kwenye jimbo la uchaguzi la segerea wilaya ya ilala kwa utambulisho zaidi naweza kusema Tabata kisukulu.
Iko hivi. Ukiwa unatokea mabibo external (Mandera road) kuna njia ya lami inayoelekea tabata kimanga,Kimara korogwe,kisukulu na segerea kupitia jeshini.
Ukiendelea mbele kuna daraja maarufu (maji chumvi) pale barabara ya lami inachepuka kwenda kutokea kimara korogwe hiyo yote ni lami,lakini mara baada ya kuvuka daraja ukinyosha kuna barabara ya vumbi ambayo inaenda kuunganika na barabara ya lami (bonyokwa segerea). Hicho kipande japokuwa ni kiungo muhimu sana ni kibovu sana na kinaharibu magari na kusababisha hasara kubwa hasa eneo korofi sana ni pale panapoitwa KAGENYI.
Mbali na kuharibika kwa magari,ikitokea gari limepakia mgonjwa au mama mjamzito au vifaa vyovyote vinavyohitaji uangalifu, unaweza kujikuta umesababisha matatizo zaidi ya lengo lako la kutoa msaada.
Ndugu zangu, kufuatana na barabara hii kuwa ni mkato na inarahisisha kukwepa foleni za magari (Buguruni) yanayotokea
Ubungo kwenda segerea, kinyerezi, majumbasita, kitunda kuelekea Gongo la Mboto na viunga vyake mpaka majohe
Tumejikuta wananchi wa Tabata kisukulu hata tulipojitahidi kutumia nguvu zetu kuziba hayo mashimo haichukui muda kuharibika
kufuatia wengi wa magari yanayotumia njia hii.
Andiko hili lina lengo la kuomba msaada kwa mamlaka husika,kwamba pamoja na ahadi zilizowahi kutolewa
kwamba DMDP watashughulikia, tunaomba matengenezo ya muda mfupi kwa kuweka kifusi angalau barabara ipitike kirahisi.
Pia kuwatahadharisha wakazi wa kitunda, Gongo la Mboto n.k wenye magari madogo wasije haribu magari yao kwa kutafuta njia mkato.
Baba yetu Mh.Isdori Mpango, waumini wenzako tuliosali wote kigango cha Mazda tukitokea kisukulu kwa sasa ni ngumu kufika kama unatumia gari inabidi uende parokia ya makoka japo kuna umbali.
Tunakuomba utuangalie kwa jicho la huruma ututoe kwenye mateso haya. Pia ndugu yetu Mh. Chongolo ,Tunakuomba pia uliangalie jambo hili utusaidie.
Nawashukuru sana ndugu zangu kwa kusoma.
Kazi iendelee.
YAANI NI KERO SANA HALAFU HICHO KIPANDE HAKIFIKI HATA KM 4, SIJUI NI NI TATIZO TUMEWAKOSEA NINI HASA WEE KIBONA?