Ubovu wa barabara iendayo Kurasini

nzoka ya pi

Senior Member
May 16, 2017
153
107
Napenda kutoa malalamiko yangu juu ya ubovu wa barabara ya bandari kule TPA Kurasini. Tafadhali Mamlaka husika tunakerwa na ubovu wa barabara ile na hasa nyakati zingne inaonekana kuna watu wanafungulia chemba za maji taka kuelekezea barabarani kumekua na harufu kali na isiyovumilika. Tafadhali mamlaka husika mpitiapo uzi huu mkumbuke kufanya maboresho juu ya barabara ile. Ni kero na usumbufu si kwa watu tu bali piah ata vyombo vya usafiri.
 
Ningependa tuanze na hao wanaofungulia chemba zao kuelekea barabarani
 
Good mleta uzi,ukweli ni kwamba ile barabara sijui iko chini ya halmashauri au tanload ilo sijajua ila ninacho jua barabara ile inaingiza pesa nyingi sana serikarini maana hakuna mzigo unao ingia bandarini usipite njia hiyo na akuna mzigo unao shuka kwenye meli na usipite njia ile swali wahusika awaoni au ndo ule utaratibu kila kitu mpaka aseme baba jesca au bashite ndo mfanye?
yawezekana wahusika awaoni ile barabara lakini viongozi wa bandari ndo njia mnayo tumia kila siku mnashindwa kuwaambia wahusika raisi akiingia bandarini mnampitisha njia nzuri za mjini kule ampitishi maana mnajua tatizo acha ilo mayor wa jiji isaya ndo njia anayo tumia kila siku kutoka kwake kigamboni nawe uoni iyo njia ili jambo lina kera sana na ukizingatia ni njia kubwa ya kutegemewa na bandari ila iko vile sasa hata ivyo viwanda mnavyo taka kujenga machine zina pitia njia hiyo kwenda viwandani kutoka bandarini,oneni aibu jamni!!!
 
Hio njia sasa hivi inanilazimisha kuzunguka uhasibu ambako ni mbali sana ukitoka/ukienda daraja la kigamboni.
 
Back
Top Bottom