Mbunge wa Tarime-CHADEMA, Chacha Wangwe amekuwa ni mtu ambaye ana sifa ya kukurupuka na kuropokaropoka, ukiondoa thread ya kubwabwaja bbc kuhusu majeshi ya Tanzania kwenda Comoro, sasa anamtaka Waziri mpya wa Nchi ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Bwana Steven Wassira aka Tyson kujiuzulu wiki moja baada ya Kukabidhiwa rasmi ofisi ya mpya..
wiki moja iliyopita, iliripotiwa na Gazeti la Mwananchi kuwa Waziri Mkuu mpya, mhe Mizengo Kayanza Peter Pinda alimkabidhi rasmi Mhe Wassira ofisi ya TAMISEMI, Wizara ya Pinda kabla ya mabadiliko, mjini Dodoma, na baadae Gazeti la This day <http://www.thisday.co.tz/News/3693.html> kuripoti kuwa Wizara ya TAMISEMI imemwajibisha Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala Bwana John Lubuva aliyehusika moja kwa moja na Sakata la kuvunjwa nyumba za Tabata jijini Dar Es Salaam..
Mheshimiwa mbunge wa Tarime Wangwe, sasa anatoa wito wa huyu Waziri nae ajiuzulu kwa kumfukuza aliyehusika na uvunjaji au kwa kuwa ni mtindo kuwa kusema watu wote wajiuzulu tu pasipo utathimini wa kazi yao?
Jamani JF, naelewa upinzani wa Tanzania ni mchanga, lakini, wito/ushabiki wa kila kona na watu kuomba au kutakwa kila kiongozi ajiuzulu wa aina ya kina Chacha Wangwe hauwezi saidia Upinzani wa Tanzania wala ushindi wa uchaguzi kwa wananchi...
Inakuwa nayo kukurupuka, wananchi watachoka sasa..Nadhani sikosei kuwa Tyson ni kati wa mawaziri wachache credible (hawajahusishwa 1 kwa 1 na ufisadi uliokithiri) katika Serikali ya JK.
Na hivi, JF, huyu Chacha Wangwe ana elimu ya aina gani jamani? si mara ya kwanza kusikia kukurupuka na kutoa hoja nzito zenye pumba..
wiki moja iliyopita, iliripotiwa na Gazeti la Mwananchi kuwa Waziri Mkuu mpya, mhe Mizengo Kayanza Peter Pinda alimkabidhi rasmi Mhe Wassira ofisi ya TAMISEMI, Wizara ya Pinda kabla ya mabadiliko, mjini Dodoma, na baadae Gazeti la This day <http://www.thisday.co.tz/News/3693.html> kuripoti kuwa Wizara ya TAMISEMI imemwajibisha Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala Bwana John Lubuva aliyehusika moja kwa moja na Sakata la kuvunjwa nyumba za Tabata jijini Dar Es Salaam..
Mheshimiwa mbunge wa Tarime Wangwe, sasa anatoa wito wa huyu Waziri nae ajiuzulu kwa kumfukuza aliyehusika na uvunjaji au kwa kuwa ni mtindo kuwa kusema watu wote wajiuzulu tu pasipo utathimini wa kazi yao?
Jamani JF, naelewa upinzani wa Tanzania ni mchanga, lakini, wito/ushabiki wa kila kona na watu kuomba au kutakwa kila kiongozi ajiuzulu wa aina ya kina Chacha Wangwe hauwezi saidia Upinzani wa Tanzania wala ushindi wa uchaguzi kwa wananchi...
Inakuwa nayo kukurupuka, wananchi watachoka sasa..Nadhani sikosei kuwa Tyson ni kati wa mawaziri wachache credible (hawajahusishwa 1 kwa 1 na ufisadi uliokithiri) katika Serikali ya JK.
Na hivi, JF, huyu Chacha Wangwe ana elimu ya aina gani jamani? si mara ya kwanza kusikia kukurupuka na kutoa hoja nzito zenye pumba..