Ubinafsishaji wa Mashirika ya umma: Zitto, badala ya kumshauri Rais aunde Tume ya Uchunguzi, peleka hoja binafsi Bungeni

Bila kujali wewe ni Zitto kweli au Zitto photocopy kwani sioni kama ni verified user acha tu nikupe ushauri wangu. Kwa sasa hakuna demokrasia na wananchi wote tunaona. Ila mimi nimeshauri, ninashauri na nitaendelea kushauri kwa sasa ni vyema mkipata nafasi ndogo hiyo hiyo inayopatikana jaribuni kujikita kwenye siasa za maendeleo wangalau kwa 65% na asilimia iliyobaki 35% ndio iwe siasa za madaraka.

Kwanini nasema hivyo? Rais wa sasa sio muumini wa demokrasia na sehemu kubwa taasisi hazifuati sheria bali anachotaka rais. Ndio maana unaona siasa sasa hivi mnafanya anavyotaka rais na sio sheria inavyotaka. Kuna mambo mengi ya kunadi mnapokuwa majukwaani. Mfano kuhakikisha kila familia ya mkulima inakuwa na wangalau heka 2 za kilimo cha kisasa. Kushusha bei za vifaa vya ujenzi ili kila mtu ajenge nyumba bora. Upande wa afya ahidini mtakapopata madaraka mtajenga kila kijiji/kata zahanati. Elimu ni mpaka chuo kikuu bure, kurejesha mahusiano mema kati ya serekali na wafanya biashara. Ajira kwa wingi

Kwenye siasa za madaraka ahidini kufufua mchakato wa katiba mpya tena ya rasimu ya Warioba. Kurejesha demokrasia kama ilivyokuwa kabla ya awamu hii ya tano kuingia madarakani. Hakikisheni mnaweka watu kwenye vipindi vya televisioni na redio wenye kuweza kuhubiri maendeleo na siasa za madaraka. Sasa hivi mnaonekana kuhubiri siasa za madaraka zaidi kwani ccm sasa hivi inawafanya kujihami zaidi kuliko kushambulia huku ccm chini ya Magufuli ikiwa na madhaifu kibao. Maisha ni magumu kumebaki vitisho na uchumi unazidi kudorora.
NB: siku hizi wewe huonekani kwenye mijadala ya TV, sijui shida ni nini. Jipangeni japo tunajua ni ngumu ila tumieni nafasi hiyo finyu kwani tayari udhaifu wa Magufuli kiuchumi na kidemokrasia sasa uko wazi zaidi. Huku kwenye mitandao njoo na hizo verified ID wekeni mambo na sisi tuko nyuma yenu.
Umetoa ushauri mzuri sana.Ni bahati mbaya sana tunatumia muda mwingi kujadili mapungufu na kauli za mkulu huku tukitumia muda kidogo sana kuwashauri wapinzani ni nini cha kufanya kujabiliana na hii hali iliyopo sasa.

Tunatumia muda mwingi kukosoa serikali badala ya kutumia muda mwingi kuwashauri wapinzani the way forward.

Pia na wapinzani kwa sasa wanapaswa kukutana na kuweka mikakati ya pamoja ya nama ya kukabiliana na hali hii.

Tusijikite tu katika kukosoa kauli na matendo ya mheshimiwa bali sasa tujikite zaidi katika kubuni mbinu zitakazotuwezesha kutumia mapungufu hayo kuiodhoofisha CCM.
 
Okay Kosa nikuwaambia wapeleke
Mijadala kwenye TV natamani kujua ni TV ipi mpaka Sasa inaruhusu kujadili issues Serious zakujenga NCH zaidi yakusifia hata mambo yakijinga... pia kwenye Magazeti mpaka Sasa kuna Gazeti gani la Maana linaruhusu Mijadala Seriously ndugu Kwanza tuwaunge Mkono akina Zitto kwa kufanya kazi kwenye Mazingira magumu ukweli Nchi ningumu sana

Mkuu sina mahali nilipomvunja moyo bali nimemwambia wajaribu kufanya juu chini kwenda kwenye Tv na kuitumia nafasi hiyo finyu. Kila mara tunawaona wapinzani haswa star tv wakijadili. Ila wamejikita zaidi kwenye siasa za madaraka. Wajaribu wawezavyo.
 
Mkuu sina mahali nilipomvunja moyo bali nimemwambia wajaribu kufanya juu chini kwenda kwenye Tv na kuitumia nafasi hiyo finyu. Kila mara tunawaona wapinzani haswa star tv wakijadili. Ila wamejikita zaidi kwenye siasa za madaraka. Wajaribu wawezavyo.
Na wapinzani kwa sasa inabidi wakubali kuingia gharama baadhi ya mikutano yao na waandishi wa habari iwe inakwenda live.

Nasema hivi kwasababu baadhi ya mambo sensitive na mazito wanayoyaongea kwa waandishi huwa hayaripotiwi na vyombo vya habari hivyo wananchi wengi wanakuwa hawaelewi ni nini hasa kinaendelea.


Kwa sasa kuna udhaifu mkubwa sana wa media kuripoti kwa ufasaha taarifa wanazopewa na wapinzani katika press conference na bahati mbaya watanzania wengi hawatafuti habari za siasa na wanasiasa kama wanavyotafuta habari kuhusu Diamond,ligi ya Uingereza na mambo mengine ya aina hiyo na pia wengj ni wavivu wa kusoma hivyo wanaishia tu kusoma headings za magazeti na kuendelea na shughuli zao.
 
Tumeshafanya hivyo sana ndani ya Bunge. Hiyo hoja Binafsi ndugu yangu hata kupangiwa haitapangiwa, nafasi ya kujadiliwa.

Acha tutimize wajibu wetu hivi pia.

Mwaka 2009 Bunge lilipitisha kufanyika kwa post privatization audit kufuatia hoja ya Kamati ya POAC wakati ule. CAG na POAC/PAC tulishatoa Taarifa kadhaa Bungeni kufuatia mashirika mbalimbali ikiwemo hili la Airtel. Wakati tunamaliza Bunge la 10 tulikuwa na Taarifa ya special audit ya privatization ya mashirika 10 ya Umma aliyofanya CAG. NBC ilikuwa kwenye Taarifa hiyo na SPM mgololo. Pia tulifanya extensive work kuhusu ukodishwaji wa Airbus kwa ATCL na Madeni makubwa famba tunayodaiwa. Nasikia Bombardier nyengine ile kubwa C300 imeshawekwa chini ya ungalizi kufuatia deni hili la hawa wa airbus. Tatizo Watanzania wana short memory span lakini ukweli ni kwamba haya mambo yanayosemwa sasa sio mapya maana tulishayaibua na yana maazimio ya Bunge
Kuhusu hili la Bombedier C 300 unaweza kumuuliza waziri husika kupitia mtandao wa twitter kama ulivyofana kipindi kile kwa kum-tag waziri husika alafu tusikie atajibu vipi.
 
We jamaa bwana! Hizo hoja wakiibua Lowassa na Sumaye wanakuwa wapi?

Yaani unataka kina Zitto waanze kutoboa mtumbwi(Lowasa na Sumaye) ambao wao wenyewe wamepanda?
We jamaa bwana! Hizo hoja wakiibua Lowassa na Sumaye wanakuwa wapi?

Yaani unataka kina Zitto waanze kutoboa mtumbwi(Lowasa na Sumaye) ambao wao wenyewe wamepanda?
Zitto anaweza kuibua akabaki salama lakini ule upande mwingine utaumia Kwa kuwa huenda hao wakuu wakaburuzwa Kwa pilato. Hii haipendezi Sana mbele ya macho ya CHADEMA na mmiliki wake Mkuu.
 
Hiki ulichofanya sasa ndio kinatakiwa, himiza na wabunge wengine waanze kumwaga mambo yaliyokuwa huko bungeni na yametupiliwa mbali. Zitto sio siri wewe una ushawishi, uzi wako hapa jukwaani unapata wachangiaji wengi. Jaribu kurushia hayo mambo hapa ili kila jambo liwe wazi. Sasa hivi serekali na watu wote waelewa wa mambo wako huku kwenye social media. Rusha jiwe gizani utaona tunavyoshambulia. Huko kwenye magazeti andikeni makala za kukumbushia tena jitahidini zipate front page. Sasa hivi wapinzani tunapambana na serekali inayotumia mabavu ila ina mbinu chache sana za kufanikiwa. Sasa ni nyie kutumia udhaifu huo. Inatakiwa ccm igeuke kuzuia mashambulizi na sio kushambulia kwa propaganda wakati ukweli hauko hivyo. Kama hutojali jaribu kuanzisha uzi kila baada ya wiki kuhusu mambo mliyopigania haswa hayo makampuni. Tutachangia kwa nguvu na tutawapoteza hao ccm. Usishinde Twitter zaidi kwani kule kuna word limit hivyo huwezi kufunguka vizuri.
Umejuaje kama Zitto mwenyewe mkuu?
 
Back
Top Bottom