Ntaramuka
Senior Member
- May 2, 2008
- 169
- 27
Kwa watanzania wengi ukiuliza kwanini Tanzania bado ni masikini watakuambia ni UONGOZI MBAYA. Lakini binafsi nimegundua kuwa, licha ya uongozi wetu, tatizo letu kubwa zaidi ni tabia ya ubinafsi. Watanzania wengi tunapenda kushughulikia matatizo yetu binafsi na hatujali kabisa matatizo ya wengine bila kujua kwamba MATATIZO YA WENGINE YANA IMPACTS KWENYE MAISHA YETU.
Mathalan, wakati wa mgomo wa madaktari, watanzania tumeliacha suala hili kwa madaktar licha ya madhara yaliyojitokeza kwa watanzania, ikiwa ni pamoja na vifo. Hata CHADEMA ambao machoni mwa watanzania wengi wanaonekana kama watetezi wao, bado hawajaungana na madaktari kutoa sauti ya pamoja kulani tatizo hili. Badala yake watanzania tumekuwa mashabiki tu wa MADAKTARI VS SERIKALI.
Hata wakati walimu wanagoma bado suala hili lilibaki kuwa la walimu vs serikali.
Hakuna mkulima anayegoma kwasababu mwalimu anaonewa, mwalimu hagomi daktari akionewa , au mwanafunzi akionewa.
Mathalan, wakati wa mgomo wa madaktari, watanzania tumeliacha suala hili kwa madaktar licha ya madhara yaliyojitokeza kwa watanzania, ikiwa ni pamoja na vifo. Hata CHADEMA ambao machoni mwa watanzania wengi wanaonekana kama watetezi wao, bado hawajaungana na madaktari kutoa sauti ya pamoja kulani tatizo hili. Badala yake watanzania tumekuwa mashabiki tu wa MADAKTARI VS SERIKALI.
Hata wakati walimu wanagoma bado suala hili lilibaki kuwa la walimu vs serikali.
Hakuna mkulima anayegoma kwasababu mwalimu anaonewa, mwalimu hagomi daktari akionewa , au mwanafunzi akionewa.