Dotto C. Rangimoto
JF-Expert Member
- Nov 22, 2012
- 1,985
- 1,282
Ukishalipia huwa unapewa stakabadhi? baada ya hapo huwa unasomewa matumizi ya hizo pesa?
uko sahihi na hili ndio tatizo lilopo chadema na huu ndio udhaifu wa mbowe. Mbowe anakopesha chama bila maandishi na anakujakujilipa fedha nyingi kuliko kile alichokikopesha chama. rejea waraka wa CHACHA WANGWE na KITILA ambao hadi sasa hazijakanushwa pamoja na kwamba zinatolewa hoja za kukitaka chama kukanusha tuhuma zilizoibuliwa na nyaraka hizo. Mbowe akanushe hizi tuhuma, kinyume chake tutaendelea kuamini huo upande uliozitoa.
binafsi na najiuliza, kwanini hoja za akina Mwigamba, marehemu Wangwe na Kitila hazijibiwi badala yake watoa hoja huitwa wasaliti bila hoja zao kujibiwa? Binafsi naanza kuamini ndani ya chama chetu kuna tatizo la uongozi, uongozi wetu ni dhaifu, legelege na mbaya zaidi hauaminiki.
Ingekuwa ni uongozi shupavu, imara na wenye kuaminika tungeona wanaotoa tuhuma hadharani wakishughulikiwa lakini hizo tuhuma zilizotoka hadharani zikijibiwa hadharani kwa vielelezo na ushahidi uso na shaka. Salama ya CHADEMA kwasababu watz wameshaichoka CCM na mtindo wa chama chetu kulipua mabomu ya ufisadi; mambo haya mawili yamepelekea chama chetu kupendwa na kukimbiliwa na watu wengi, lkn viongozi wake ni MAJANGA, hawajui kuongoza wanachojua wao ni kuishambulia CCM na kulipua mabomu ya ufisadi.
Kwakuwa sasa wanaishambulia CCM kama chama tawala, tukishinda tutaishambulia kama chama cha upinzani chenye kuhatarisha ridhaa tutakayopewa na umma kuongoza nchi hii. Kwa mtindo wa kushambulia kama ndio njia ya kuwatumikia watz hatutafika mbali na tafauti yetu na CCM itakuwa ni JINA tu, lkn vitendo vyetu vitakuwa vilevile.
MUNGU WAPE BUSARA NA HEKIMA VIONGOZI WA CHADEMA NA WANACHAMA WAKE.