Ubepari unaporomoka, What's Next?

Sasa hiyo ndiyo nini? Watu waliyoenda madrassah utawajua tu for their predisposition to rampant copying-and-pasting without feeling the need to explain anything further. Halafu hapo anajiona kachangia kitu cha maana.
Nilikuwa napata shida sana ni kwanini unakuta watu wanachinjana kwa sababu tu ya tofauti ya dini zao ila sasa nimeanza kuelewa. Hii tabia ya kudharau madrassa imeota mizizi sana hapa JF na isipokemewa na kuisha itatupeleka pabaya sana. Inashangaza sana, yaani watu wanajadili mada tofauti halafu mtu anatoka huko alikotoka anaona jambo la msingi ni kuleta dharau kwa madrassa.

Kwa kweli naomba niseme nimejaribu sana kutokujali lakini sasa naona imezidi. Na ninasema hizi dharau taratibu naona zinaanza kuzaa chuki kali sana moyoni mwangu. Tuwe makini sana maana kama tukiacha hali iendelee hivi, nina hakika itafikia mahali pabaya, na ubaya au uzuri mahali hapo mimi sipaogopi hata kidogo.

Tuheshimiane wakuu, msidhani waislamu ni wajinga sana.
 
Ungesoma maelezo hapo chini,I did explain!!
Kwa kiswahili,ni asilimia ya mapato ya serikali kulinganisha na mapato yote ya taifa.Kwa kuendelea zaidi,hiyo chati inaonyesha ukubwa wa serikali kiuchumi kulinganisha na sekta binafsi kwenye nchi husika.Tanzania kwa mfano,ni asilimia 12 tu ya uchumi wote ndio huenda serikalini kwa ajili ya matumizi mbalimbali kama elimu,afya,ulinzi,vitafunio n.k wakati asilimia 30 ya uchumi wa marekani humilikiwa na serikaLI AU TUSEME MAPATO YA SERIKALI NI ASILIMIA 30 NA SEKTA BINAFSI NI ASILIMIA 70.....Umeelewa bi mdogo?

Kwa uelewa wangu ni kwamba Tarakimu (Numbers) ukichanganya na maelezo yakinifu (Logic) ndiyo hutengeneza takwimu (Statistic) lakini data zineweza kuwa ni tarakimu,maelezo yakinifu au takwimu. Lakini vyote hivi hutengenezwa kwa madhumuni maalum.

watu wanaoshughulika na mambo haya ya tarakimu,takwimu na mantiki wanajua vizuri ni kwa jinsi gani falsafa ya nusu Glasi imejaa maji au nusu Glasi haina maji inavyofanyakazi. Ubepari au ujamaa ni falsafa hivyo huwezi kuzipima kwa tarakimu wala takwimu ispokuwa kwa maelezo yakinifu (mantiki)

Nchi ya kijamaa kutokana na mahitaji yake inaweza kutumia hata zaidi ya nusu ya mapato yake ghafi ya taifa(GDP) kwa ajili ya ulinzi na bado ikabakia ni ya kijamaa. Na nchi ya kibepari hata itoe misaada ya wingi kiasi gani (kama inavyofanya Marekani) kwa watu na nchi maskini duniani bado itabikia kuwa ni nchi ya kibepari.

Dhana ya Ubepari au Ujamaa inajengwa na mahusiano kati ya jamii katika kuzalisha mali na jinsi mapato ya uzalishaji mali yanavyomilikiwa na kugawanywa. Mahusiano ya uzalishaji mali yanatokana na nani anamiliki zana za kuzalisha mali (Means of Production) na nani anafaidika na ziada (surplus) na faida (Profit) inayopatikana. Takwimu pekee hazitoshi kuitambulisha nchi kama ni ya kijamaa au ni ya kibepari. Wala umaskini au utajiri wa nchi siyo kigezo cha ujamaa au ubepari.

Kwa kutumia takwimu na tarakimu unaweza kujidanganya au kujipa maarifa zaidi. Tanzania zaidi ya asilimia sabini (70%) ya watu wake hawako kwenye ajira rasmi lakini athari zake kwenye uchumi wa dunia haiwezi kuonekana kabisa. lakini ukosefu wa ajira (Unemployment) kwa asilimia tisa (9%) tu kwa marekani ni dhahama kubwa sana kwa uchumi wa nchi hiyo na dunia kwa ujumla.

Ndugu yangu kuna tofauti kubwa sana kati ya ulimwengu na dunia ingawa vyote viwili vinahusiana na kufanana!!
 
Comrade Kobello, bana naona unamwaga data!
Pamoja sana mkuu, taku-PM badae, endelea kwanza na mapambano
 
Nilikuwa napata shida sana ni kwanini unakuta watu wanachinjana kwa sababu tu ya tofauti ya dini zao ila sasa nimeanza kuelewa. Hii tabia ya kudharau madrassa imeota mizizi sana hapa JF na isipokemewa na kuisha itatupeleka pabaya sana. Inashangaza sana, yaani watu wanajadili mada tofauti halafu mtu anatoka huko alikotoka anaona jambo la msingi ni kuleta dharau kwa madrassa.

Kwa kweli naomba niseme nimejaribu sana kutokujali lakini sasa naona imezidi. Na ninasema hizi dharau taratibu naona zinaanza kuzaa chuki kali sana moyoni mwangu. Tuwe makini sana maana kama tukiacha hali iendelee hivi, nina hakika itafikia mahali pabaya, na ubaya au uzuri mahali hapo mimi sipaogopi hata kidogo.

Tuheshimiane wakuu, msidhani waislamu ni wajinga sana.
Si jambo jema kuingiza chuki za udini kwenye mada kama hii. Nadhani kuna watu wanahusisha Uislamu na uarabu na tatizo liko hapo, wengine wetu tunawaunga mkono Wapalestina kwa sababu tunadhani ni "waislam" wenzetu wanaonewa na Wayahudi ambao ni 'wakristo" na wengine tunawaunga mkono Waisraeli kwa sababu wao ni taifa teule la mungu na ni shina la "ukristo". dhana hizo mbili haziko sahihi.

Wayahudi wengi (labda 90%) hawaamini kama Yesu Kristo alikuwa ni masihi na wala siyo kila Mpalestina ni Muislam, kuna wakristo wengi sana Beirut ambao nao pia wanashambuliwa na waisrael kama wapalestina wenzao ambao ni waislam. Hoja iliyotolewa ni kwamba mbadala wa mfumo huu wa kibepari ni "islamic monetary system" ambayo sisi wengine tunauliza inafanyaje kazi? Madrassa imetoa baadhi ya watu waungwana na waadilifu sana ninaowafahamu!!
 
..nimesikia kwamba Ujerumani elimu ni bure toka chekechea mpaka chuo kikuu. sasa kwanini sisi tunajiona ni wajamaa kuliko wao?
 
..nimesikia kwamba Ujerumani elimu ni bure toka chekechea mpaka chuo kikuu. sasa kwanini sisi tunajiona ni wajamaa kuliko wao?
Nafikiri watu wengi tunapoteza maana halisi ya UJAMAA kama UMILIKAJI wa njia za KUZALISHA uchumi kwa kufikiria kwamba hata malnego ya maisha bora kama unalenga watu wote ni UJAMAA ule ule..

Hizi siasa za kushoto na kulia yaani Ubepari na Ujamaa unatofautiana ktk umiliki wa njia za kiuchumi kufikia lengo moja - MAISHA BORA kwa WANANCHI wake na tofauti inakuja ktk umilikaji wa njia ya KUZALISHA UCHUMI na sio matumizi wa mavuno yaliyopatikana..Ujamaa ukitaka njia hizo za kuzalisha uchumi ziwe mikononi mwa jumuiya nzima bila mwenyewe na hivyo kutomilikiwa na mtu mmoja au shirika binafsi lisilo la Umma...
Hali Ubepari unalazimu mtu mmoja mmoja au shirika kumiliki mali ya Taifa hivyo serikali kukusanya kodi zake kutoka fungu la mapato ya utajiri huo na kisha kuiendelea Jamii...

Sasa watu wengi sana tunachanganya baina ya Ujamaa kama siasa na njia ya umilikaji wa means of production na Ujamaa kama Umoja wa mafanikio ktk huduma za Kitaifa. Hawa wenzetu Mabepari wameisha ondoka ktk swala la umilikaji wa njia za kukuza uchumi.. wanakubaliana wote kwamba serikali haitakiwi kumiliki njia za kukuza uchumi isipokuwa sasa Wajamaa ni wale wanaosema HUDUMA zote muhimu kwa wananchi haziwezi kuingia ktk mfumo mzima wa njia za kukuza Uchumi, ila hizi ni muhimu ktk matayarisho ya jamii kuingia ktk uwanja wa uzalishaji...

Kwa hiyo ndio maana Wajamaa ktk Ubepari kina Liberal, Demokratic na kadhalika huzungumzia zaidi huduma za kitaifa kuwa mikononi mwa serikali kwani sii njia za kuzalisha uchumi bali ni msingi wa maisha ya jamii yenyewe, hali Mabepari wanataka control ya kila kitu mikononi mwa watu binafsi kwa maana kwamba hakuna kiti kisichokuwa biashara na kikakuza uchumi..hata shule, Hospital, social walfare, vyote hivi ni hela tupu na vitaimarika mikononi mwa watu binafsi kama biashara nyingine..Sasa ukijiuliza hivi kama kweli vitu vyote hivi vikibinafsishwa hizo kodi zetu serikali inazokusanya huzifanyia vitu gani?..Kwa mabepari kina Bush ndio hivyo hununua/hutengeneza zaidi silaha, kuanzisha vita na program za space kuwa matumizi yake makubwa ili mradi hakuna kitu kisichokuwa biashara..Lakini kwa nchi kama TZ ndio Ufisadi na kujitajirisha..

Kwa hiyo Germany kuwa na elimu bure ni matokeo ya mavuno wanayopata toka kodi zao na chama cha kikristu kimesimami elimu ni right ya mwananchi, Afya ni right na kadhalika ndio maana ujamaa wake wanakubali Ubinafsishaji lakini ile kodi inayokusanywa inapewa vipaumbele ktk elimu, afya, barabara, mazingira na kadhalika, vitu ambavyo vimetazamwa kama sii njia za kuzalisha uchumi bali njia za kuboresha maisha ya wananchi wake...Hivyo basi Germany sio wajamaa ila ni Mabepari kwa sababu malengo ya itikadi zote (Ujamaa na Ubepari) ni kutoa maisha bora kwa wananchi wake - No one is left behind!...
 
Nafikiri watu wengi tunapoteza maana halisi ya UJAMAA kama UMILIKAJI wa njia za KUZALISHA uchumi kwa kufikiria kwamba hata malnego ya maisha bora kama unalenga watu wote ni UJAMAA ule ule..

Hizi siasa za kushoto na kulia yaani Ubepari na Ujamaa unatofautiana ktk umiliki wa njia za kiuchumi kufikia lengo moja - MAISHA BORA kwa WANANCHI wake na tofauti inakuja ktk umilikaji wa njia ya KUZALISHA UCHUMI na sio matumizi wa mavuno yaliyopatikana..Ujamaa ukitaka njia hizo za kuzalisha uchumi ziwe mikononi mwa jumuiya nzima bila mwenyewe na hivyo kutomilikiwa na mtu mmoja au shirika binafsi lisilo la Umma...
Hali Ubepari unalazimu mtu mmoja mmoja au shirika kumiliki mali ya Taifa hivyo serikali kukusanya kodi zake kutoka fungu la mapato ya utajiri huo na kisha kuiendelea Jamii...

Sasa watu wengi sana tunachanganya baina ya Ujamaa kama siasa na njia ya umilikaji wa means of production na Ujamaa kama Umoja wa mafanikio ktk huduma za Kitaifa. Hawa wenzetu Mabepari wameisha ondoka ktk swala la umilikaji wa njia za kukuza uchumi.. wanakubaliana wote kwamba serikali haitakiwi kumiliki njia za kukuza uchumi isipokuwa sasa Wajamaa ni wale wanaosema HUDUMA zote muhimu kwa wananchi haziwezi kuingia ktk mfumo mzima wa njia za kukuza Uchumi, ila hizi ni muhimu ktk matayarisho ya jamii kuingia ktk uwanja wa uzalishaji...

Kwa hiyo ndio maana Wajamaa ktk Ubepari kina Liberal, Demokratic na kadhalika huzungumzia zaidi huduma za kitaifa kuwa mikononi mwa serikali kwani sii njia za kuzalisha uchumi bali ni msingi wa maisha ya jamii yenyewe, hali Mabepari wanataka control ya kila kitu mikononi mwa watu binafsi kwa maana kwamba hakuna kiti kisichokuwa biashara na kikakuza uchumi..hata shule, Hospital, social walfare, vyote hivi ni hela tupu na vitaimarika mikononi mwa watu binafsi kama biashara nyingine..Sasa ukijiuliza hivi kama kweli vitu vyote hivi vikibinafsishwa hizo kodi zetu serikali inazokusanya huzifanyia vitu gani?..Kwa mabepari kina Bush ndio hivyo hununua/hutengeneza zaidi silaha, kuanzisha vita na program za space kuwa matumizi yake makubwa ili mradi hakuna kitu kisichokuwa biashara..Lakini kwa nchi kama TZ ndio Ufisadi na kujitajirisha..

Kwa hiyo Germany kuwa na elimu bure ni matokeo ya mavuno wanayopata toka kodi zao na chama cha kikristu kimesimami elimu ni right ya mwananchi, Afya ni right na kadhalika ndio maana ujamaa wake wanakubali Ubinafsishaji lakini ile kodi inayokusanywa inapewa vipaumbele ktk elimu, afya, barabara, mazingira na kadhalika, vitu ambavyo vimetazamwa kama sii njia za kuzalisha uchumi bali njia za kuboresha maisha ya wananchi wake...Hivyo basi Germany sio wajamaa ila ni Mabepari kwa sababu malengo ya itikadi zote (Ujamaa na Ubepari) ni kutoa maisha bora kwa wananchi wake - No one is left behind!...

Lakini mkandara kwenye maudhui ya hoja yako kuna jambo nahitilifiana na wewe. Ni kweli kwamba Ujamaa au Ubepari huamuliwa na umilikaji wa njia za uzalishaji mali kama zinamilikiwa na Umma au kibinafsi. Lakini pia hata jinsi zinavyogawanywa huamua aina ya mfumo unaofuatwa.

Kwenye ubepari hizo "huduma za jamiii" hazitolewi hivihivi lazima kuna kuwa na hoja nyuma yake hasa kwamba kutolewa kwa huduma hizo kutasababisha kuongezeka kwa ajira miongoni mwa jamii, wakati kwa wajamaa kama Cuba huduma hizo hutolewa kama haki ya msingi ili jamii iendelee kuwepo ikiwa na afya njema.
 
..nimesikia kwamba Ujerumani elimu ni bure toka chekechea mpaka chuo kikuu. sasa kwanini sisi tunajiona ni wajamaa kuliko wao?

Tazama pia na asilimia ngapi ya Wajerumani wanalipa kodi halafu tazama na hapa kwetu. Asilimia 20 ya walipa kodi ndio inayobeba mzigo wa Watanzania wote wasiolipa kodi. Huo ndio ujamaa wa kweli. Natengeza kwa mwenzangu na kwangu kwa poromoka.
 
Labda tuanzie kwenye vitu vya msingi kwanza:

Ubepari ni nini?
Ujamaa ni nini?

Isije kuwa watu wanafikiria wanazungumza kitu kilekile kumbe wanazungumzia vitu viwili tofauti. Mojawapo ya fallacies ni ile ya pseudo obviousness kwamba watu wanachukulia kuwa kila mtu anaelewa au anafahamu kinachozungumzwa. Hivyo, kabla hatujajua sana kama ni mfumo gani unaporomoka na upi utaingia ni vizuri kujiuliza maana ya mifumo hiyo.
 
ni hivi maswali manne ya wachumi ni yafuatayo based on limited resources approach.

1... ni kipi chakuzalisha ambacho kitaleta the greatest hapiness katika jamii? kuna vitu chungu mtele vya kuzingatia hapa.
a...ni namna gani utatumia kujua watu wanataka nini? kwa sababu huwezi kumridhisha kila binadamu na mahitaji yanatofautina baina ya watu

b...the best choice is made based on the majority needs kwa kuanzia ni food, shelter and clothing. Then what follows is based on economical advances of that society which is bound to create new options and wants to different people based on income and social position.

c...kutambua jinsi watu watakavyo chagua hili uweze kuzalisha baada ya mahitaji yao muhimu matatu ya kisha tatuliwa ni utata mwingine. Huwezi kulazimisha watu wale ugali kila siku au mtu asihame nyumba wakati mshahara unamruhusu kutoka kwenye nyasi kwenda kwenye tofali.

d... kwa hiyo ni nani asimamie huu uzalishaji 'private sector' au serikali
i.... hapa ndio uchumi mwingi ambao uliokuwa centralised yaani things like ujamaa na upuuzi mwingine umeshindwa they ended up either over producing or under producing in economical terms its a waste of limited resources or not fulfilling people hapiness or simply a bad approach in allocative of resouces . The 'choice behaviour' is hard to predict si ajabu nchi za ujamaa uditekta huwa ni lazima hili kuwapunguzia watu personal choices.
ii...The free market insists in letting the market decide what to be produced, in a sense it allows so many people to produce based on what the market wants, this is where the theory of demand and supply arises. you see instead of the government over or under produce the burden falls into individuals or groups, therefore it escapes loses.

This mode creates creative people and assumes only the credible players will survive but others are allowed to participate if they think they got the trick. It can also create uncertainity in the market because greed can cause bigger players to outwit new and smaller ones to go into bankrupcy through pricing et al. It is the role of gov to moniter that, it is very technical so i will avoid explanations as countries approaches differ.

e...financing some of the playes is a very tricky business and you got a couple of disciplines that are dedicated into these outlooks. Some take years to master and advisors are rewarded well unfortunately; wetu ni Mkullo jamaa ni janga kwa taifa.

........so far the problem lies in 'allocative efficieny' to do with socialism or centralised mode and in the financial sector pinning who to lend to in the free market.

note capitalism hasnt failed monitoring is a trick so far.

Well then 2, 3, 4 will depend on the responce of 1.

alamsiki.
 
 
 
Labda tuanzie kwenye vitu vya msingi kwanza:

Ubepari ni nini?
Ujamaa ni nini?


Isije kuwa watu wanafikiria wanazungumza kitu kilekile kumbe wanazungumzia vitu viwili tofauti. Mojawapo ya fallacies ni ile ya pseudo obviousness kwamba watu wanachukulia kuwa kila mtu anaelewa au anafahamu kinachozungumzwa. Hivyo, kabla hatujajua sana kama ni mfumo gani unaporomoka na upi utaingia ni vizuri kujiuliza maana ya mifumo hiyo.
Dunia nzima majina ya mifumo ni hayo jee utendaji kazi wa mifumo hiyo inafanana kwa nchi na nchi. Ubepari wa Marekani na wa Ujerumani unafanana? na ujamaa wa Tanzania ulikuwa unafanana na wa Hungary?
 
ni hivi maswali manne ya wachumi ni yafuatayo based on limited resources approach.

1... ni kipi chakuzalisha ambacho kitaleta the greatest hapiness katika jamii? kuna vitu chungu mtele vya kuzingatia hapa.
a...ni namna gani utatumia kujua watu wanataka nini? kwa sababu huwezi kumridhisha kila binadamu na mahitaji yanatofautina baina ya watu

b...the best choice is made based on the majority needs kwa kuanzia ni food, shelter and clothing. Then what follows is based on economical advances of that society which is bound to create new options and wants to different people based on income and social position.

c...kutambua jinsi watu watakavyo chagua hili uweze kuzalisha baada ya mahitaji yao muhimu matatu ya kisha tatuliwa ni utata mwingine. Huwezi kulazimisha watu wale ugali kila siku au mtu asihame nyumba wakati mshahara unamruhusu kutoka kwenye nyasi kwenda kwenye tofali.

d... kwa hiyo ni nani asimamie huu uzalishaji 'private sector' au serikali
i.... hapa ndio uchumi mwingi ambao uliokuwa centralised yaani things like ujamaa na upuuzi mwingine umeshindwa they ended up either over producing or under producing in economical terms its a waste of limited resources or not fulfilling people hapiness or simply a bad approach in allocative of resouces . The 'choice behaviour' is hard to predict si ajabu nchi za ujamaa uditekta huwa ni lazima hili kuwapunguzia watu personal choices.
ii...The free market insists in letting the market decide what to be produced, in a sense it allows so many people to produce based on what the market wants, this is where the theory of demand and supply arises. you see instead of the government over or under produce the burden falls into individuals or groups, therefore it escapes loses.

This mode creates creative people and assumes only the credible players will survive but others are allowed to participate if they think they got the trick. It can also create uncertainity in the market because greed can cause bigger players to outwit new and smaller ones to go into bankrupcy through pricing et al. It is the role of gov to moniter that, it is very technical so i will avoid explanations as countries approaches differ.

e...financing some of the playes is a very tricky business and you got a couple of disciplines that are dedicated into these outlooks. Some take years to master and advisors are rewarded well unfortunately; wetu ni Mkullo jamaa ni janga kwa taifa.

........so far the problem lies in 'allocative efficieny' to do with socialism or centralised mode and in the financial sector pinning who to lend to in the free market.

note capitalism hasnt failed monitoring is a trick so far.

Well then 2, 3, 4 will depend on the responce of 1.

alamsiki.
 
 
Uchambuzi wako nimeupenda sana. Lakini hoja yangu kubwa ni kwamba hata kama tutaendelea na ubepari hatukuwa huu tunaoujua sisi hivi sasa. Historia inaonyesha kwamba kushindwa kujikidhi kwa Ulaya kwenye mambo makubwa matatu yaani masoko na Malighafi na nguvu kazi ya bei rahisi(Raw materials, Market and cheap labor) ndiko kulikopelekea kuparurana kugombea bara la Afrika na hatimaye kufanyika kwa mkutano wa Berlin.

Hali ile ndiyo naiona sasa inaendelea huko ulaya na sasa hivi Marekani. Hawa watu watatusalimisha waafrika au waafrika wafanye nini ili wanusurike kwenye dhahama ya kukolonishwa tena?
Hali
 
siyo kureplace capitalism - hatuwezi kuondoka na capitalism; tunazungumzia balancing capitalism au tunaweza tukasema ni modern capitalism in contrast to classical capitalism. In other words we need a new synthesis of a modern economic theory. We are talking about a theory that will describe a modern political system which will explain the relation between private capital and public good, foreign investment and local needs, laws and order as they relate to human rights and justice. Lakini kubwa zaidi ni theory ambyo itaangalia private property and private consolidation of wealth as they impact or relate to the needs of the large community.

Thanks MWANAKIJIJI for putting it in SIMPLE BUT TRUELY RIGHT WORDS
 
Kwa zaidi ya Miongo miwili sasa (2 decade ) nchi zinazoendelea na maskini sana duniani ziliaminishwa kwamba kwa kufuata mfumo wa kibepari nchi hizo zitaokoka katika janga la kuangamia kiuchumi kwenye "dunia kijiji" au al maarufu Global village.

Lakini sasa mfumo huo wa Kibepari unaporomoka kama ulivyoporomoka mfumo wa kikomunisti Urusi. Kama mbadala wa Ukomunisti na Ushoshalisti ulikuwa ni ubepari na ubepari sasa unaporomoka ni nini kitaziba ombwe litakalosababishwa na kuporomoka kwa ubepari? Tulikuwa tunaambiwa hata humu ndani tuliambiwa pia. "ujamaa ulituchelewesha kuendelea" Je sasa tuna haja ya kujivunia ubepari?

Maneno kama vile "Austerity" "Slump" au "Crunch" pia "Recession" tumekutana na " Budget talks stalemate in US" kuna hili pia "china hold 45% of US bond" na mengineyo mengi ni dalili za kuanguka kwa mfumo wa kibepari.

Ni mawazo tu usikasirike.
Mimi ninadahani system yenyewe ndiyo itazalisha mfumo, waweza kuwa mpya kabisa na ambao hujawahi kuwepo duniani, a combination ya mifumo iliyowahi kuwepo or something! Ningependa sana niishuhudie evolution ya mfumo unaokuja!
 
Uchambuzi wako nimeupenda sana. Lakini hoja yangu kubwa ni kwamba hata kama tutaendelea na ubepari hatukuwa huu tunaoujua sisi hivi sasa. Historia inaonyesha kwamba kushindwa kujikidhi kwa Ulaya kwenye mambo makubwa matatu yaani masoko na Malighafi na nguvu kazi ya bei rahisi(Raw materials, Market and cheap labor) ndiko kulikopelekea kuparurana kugombea bara la Afrika na hatimaye kufanyika kwa mkutano wa Berlin.

Hali ile ndiyo naiona sasa inaendelea huko ulaya na sasa hivi Marekani. Hawa watu watatusalimisha waafrika au waafrika wafanye nini ili wanusurike kwenye dhahama ya kukolonishwa tena?
Hali

Zama za kina king Leorpad, Stanley, Cecil rhodes, et al are over a century now. Dunia imeshapiga hatua ndefu sana nnchi zina uhuru, majukumu ya kujiamlia na namna za kujitawala kwa hivyo jambo kama la Berlin conference aliwezekani leo. Watu sasa wana sign mikataba na mashetani si wazungu tu kwenye dunia ya leo: wachina, waarabu, south americans, Indians etc wote wanalilia hii mikataba ya Africa na mariasili zetu.

Tatizo letu ni uhuru wa ndani na jinsi ya kujitawala wenyewe ndio janga kubwa la Africa.Hali hii aina tofauti kubwa sana tokea watu kama akina 'Stanley' walivyo ikuta, ni sababu zile zile walizoamua kututawala zama zile ndio zinawafanya watunyonye leo na mainly ni ignorance and how we govern ourselves.

Taifa aliwezi likawa gizani na waziri akabaki madarakani na wizara isio isha scandal, maisha haya wezi kuwa magumu bila kumuuliza waziri, kwanini mtu aonge kwenye haki yake au la lako aliendi na tuone sawa kuwa ndio hali halisi, kwanini viongozi waibe na wasiwajibishwe na kwanini watu wakubali viongozi wetu wajiamulie mishahara ya ajabu na marupu marupu hili hali wengine wanabangaiza maisha. Halafu jamii iende kuwapigia kura na kuwarudishia dhamana ya kuendelea na upuuzi ule ule we uoni hatari hapo na ignorance has a part.

On other hand dunia imeikubali 'free market' na moja ya kanuni zake ni hivi 'self interest' is good. 'Adam Smith' anasema mwenye bucha akuwekei kitoweo kwa sababu anakupenda sana wewe, ni kwa sababu anajijali yeye na faida yake. Lakini kwa kuuza kitoweo anasaidia jamii kupata bidhaa muhimu. Kwa maana hiyo kwenye kutafuta individual hapiness kunazaa social happiness kwa kuwa na wewe ukisha nunua kitoweo unaridhika.
Sasa tusitegemee eti tuendelee na upuuzi wa raisi anaekuja na kauli ambazo ajui kwanini sisi maskini au serikali aitengenezi mvua hili kutatua giza na tukaona sawa, au raisi anaetuwekea viongozi wenye uwezo duni ki-fikra na sisi tunaona sawa.

Hii ni hatari as national assets are at stake ambazo ndio zinatakiwa kutupa comparative advantage in the market matokeo yake tunagawa kama bure, dubious contracts zina tuzalishia madeni hela ambazo zingeongeza hapiness kama zingetumika katika jamii.

Amidst of all the nonsense in afrika wenzetu through self interest and the global village watu watakuja na wakikuta hali hipo hovyo viongozi wenyewe hawapo focused ofcourse watalamba ardhi, madini etc. Hapo tusilaumu capitalism bali ignorance yetu wenyewe like i said capitalism always evolve and those who have embraced it are clever societies inabidi tuache ushabiki maandazi kiongozi ajae ni lazima hawe na akili za kweli i dont care from what political party. Lakini lazima ajue vita vyenyewe vikoje its a jungle out there and only the fittest survive ukiwa na timu sophia simba ndani then u know its a joke.
 
Listen mkuu wangu economics ya vitabu haifanyi kazi tena.. Sisi toka Mwinyi tulianza na SAP hadi MKUKUTA over ten strategies, nchi ndio inazidi kuzama na ukisoma vitabu vyote vinakwambia nchi maskini inahitaji wawekezaji sijui kubinafsisha!.. Mbona tunazidi kuadhirika hakuna hata nafuu..
China haiihitaji US amini maneno yangu na sababu ni cheap Labour kisha sasa hivi vitu vyote Original vinatengenezwa China imefikia hadi magari, viwanda na vifaa vyote vya nyenzo kwa matumizi ya dunia nzima kwa sababu China wana wasomi ktk fani zote.. Vumbua kitu lete blue print kesho wanakutolea vile vile at the lowest cost hakuna siasa. Maisha kweli yanapanda hata China lakini kumbuka China has 1.5 billion people with over 200,000 living outside China na majority are doing well hata nje.. And besides all hardly uses (buy) foreign commodities - Utapata wapi taifa kama hilo wanajiingiza kila kona ya dunia na wanakubalika tena, USA pekee wameshika miji yote kuna ChinaTown na wanafanya biashara zote huku mali zao (almost all) comes from China. nenda Europe na sasa wanavamia Afrika, yaani mkuu wangu China kitu kingine kabisa ni kama mchwa..Hawa hawana mahesabu ya kiuchumi hata kidogo.


kwa wanaoijua china watakubaliana nawe hawajamaa hawasemi sana ila wanapiga mzigo
 
Lakini mkandara kwenye maudhui ya hoja yako kuna jambo nahitilifiana na wewe. Ni kweli kwamba Ujamaa au Ubepari huamuliwa na umilikaji wa njia za uzalishaji mali kama zinamilikiwa na Umma au kibinafsi. Lakini pia hata jinsi zinavyogawanywa huamua aina ya mfumo unaofuatwa.

Kwenye ubepari hizo "huduma za jamiii" hazitolewi hivihivi lazima kuna kuwa na hoja nyuma yake hasa kwamba kutolewa kwa huduma hizo kutasababisha kuongezeka kwa ajira miongoni mwa jamii, wakati kwa wajamaa kama Cuba huduma hizo hutolewa kama haki ya msingi ili jamii iendelee kuwepo ikiwa na afya njema.
Mkuu wangu unataka kunambia Japan, Canada, USA, UK ambao wanatoa pia huduma hizi bure ni Wajamaa?.. Sidhani kwa sababu Ujamaa kwao unatokana na kwanza umilikaji wa njia za uzalishaji..Siasa zao zinatazama kwanza msingi wa UCHUMI ktk uzalishaji wake..

Hao wanaoitwa Wajamaa (Liberal na Socialist) ndani ya Ubinafshaji hawakuwa wajamaa kwa sababu wanatoa hizi huduma bure, laa ila huduma hizo zimetanguliwa na sababu kubwa ya kimsingi policy yao KIUCHUMI sekta hizi ziwe au zipo chini ya umiliki wa serikali (AFYA na ELIMU), wakati Conservative wanataka kila kitu kibinafsishwe. Hivyo nakubaliana na wewe ktk mfululizo (chain) ya matumizi ya maneno haya lakini kunambia Conservative ni Ubepari pinzani ya Demokratik au Liberal ambao wanaitwa Wajamaa ili hali wote wanakubaliana Ubinafsishaji. Na ndio maana tunakubali mwana JF mmoja lipozungumzia USA kuwa wajamaa kuliko hata nchi za China kwa sababu hadi leo hii US na UK wana mashirika chini ya serikali ambayo kusema kweli huwezi hata kufikiria kwa nini tunalazimishwa sisi kubinafsishwa hali wao bado hadi leo wanasuasua kubinafsisha baadhi ya mashirika yao..

Mkuu wangu it's a little bit complicated than we think, kwa sababu Japan nao wanatoa huduma nyingi Bure, Canada wanatoa huduma hizo bure na kama sikosei Germany na UK wote hawa wamnazo huduma za bure Kia Afya na Elimu kwa wananchi wake na zinaendeshwa kama haki ya wananchi nbdio maana zinatolewa Bure, hivyo haiwafanyi nchi hizo kuwa Wajamaa ikiwa njia za uzalishaji zimebinafsishwa. Cuba wanaitwa Wajamaa kwa sababu ya POLICY, Sheria za Kiuchumi inayosema - Njia za uzalishaji zipo mikononi mwa serikali, na Marekani wanaitwa Mapebari kwa sababu sheria za Kiuchumi zinasema - Njia za uzalishaji ziko mikononi mwa watui binafsi - Period!.

Huu Ujamaa mwingine tunaousikia ndani ya Ubinafsishaji hauhusiani zaidi na Siasa ambazo ndio blue print ya UCHUMI wa nchi husika, ila ni Ujamaa unaopingana na Uasilia wa mila, desturi na tamaduni ili kuunda Taifa jipya lenye kutoa uhuru zaidi kwa wananchi wake kuchagua, na hakika huduma muhimu kama hizi kwa wananchi ni right yao badala ya kuwa privilage..Na ktk mtazamo wa maswala kama haya watu wote tunatofautiana kwa sababu unaweza kuwa Mjamaa ktk policy ya Kiuchumi lakini ukawa Conservative ktk kulinda tamaduni zenu Kama ilivyokuwa Russia na China enzi zile Macomunist lakini walipiga marufuku Dini na any imported material ambazo zinaweza kurubuni wananchi kiasi cha kuharibu malengo na culture zao..

Ndio maana mimi hapa ni Mjamaa naetaka sana Elimu na Afya nchini Tanzania iwe Bure, lakini at the same time najiona Conservative kwa sababu ya kuthamini mila, desturi na tamaduni za Mtanzania ambazo ningependa sana kuzilinda dhidi ya wageni na tamaduni zao. Wakija kwetu Rome, ni lazima wajifunze kuishi kama sisi sio sisi tunajaribu kujibadilisha ili tu fit in na kukubalika na wazungu, wachina, wahindi au waarabu..
 
Back
Top Bottom