Ubalozi wa Tanzania Uingereza walalamikiwa kwa kutopokea simu, huduma duni kutoka kwa wageni watarajiwa, je wahusika wanakwepa lugha ya kiingereza?

Richard

JF-Expert Member
Oct 23, 2006
14,939
20,399
Tangu kuanzishwa kwa huduma ya kufanya maombi ya viza mtandaoni kwa wageni wanaotarajiwa kutembelea Tanzania, huduma hiyo imezorota katika siku za karibuni.

Muombaji viza anaetaka kutembelea Tanzania kwa kusudio lolote inanmbidi ajaze fomu ya maombi mtandaoni ambapo idara ya uhamiaji makao makuu kupitia mtandao huo itashughulikia maombi ya mgeni huyo na miwsho kutoa viza ya kwenye karatasi.

Viza hiyo ya kwenye karatasi ambayo huitwa e-visa itabebwa na mgeni huyo bila kuhitaji pasi yake ya kusafiria kuwekwa ganda maalum su sticker ya viza.

Tatizo ambalo limejitikeza hadi sasa ni kwamba wageni watarajiwa wamekumbwa na vikwazo vya kimtandao kama kusimama kwa zoezi zima la kujaza fomu hiyo mtandaoni kitendo kinachoitwa "freeze" ambapo muombaji hujikuta anashindwa kuendelea kufanya maombi na hivyo kuachana na zoezi zima.

Tatizo hilo linaonyesha kwamba kuna maombi mengi sana yanayofanywa mtandaoni na mfumo wa kompyuta kushindwa kuhimili uwingi wa maombi hayo.

Hivyo hali hii inapelekea kuleta mashaka juu ya utayari wa idara hiyo ya uhamiaji katika kuwezesha wateja wao kufanya maombi bila vikwazo na kisha kuingiza fedha za kigeni mbalimbali na watalii nchini kutokea Uingereza.

Hali hiyo imepelekea kuwafanya baadhi ya wageni hao watarajiwa kufunga safari kwenda ubalozini ili kuweza kupata habari zaidi kuhusu matatizo hayo, jambo ambalo linazaa tatizo jingine kwamba hakuna taarifa zaidi za kutosheleza juu ya mabadiliko katika kufanya maombi kwamba kwa sasa maombihayo yanafanywa mtandaoni.

Mara nyingi katika kufanya mabadiliko makubwa kama haya huwa ofisi za balozi mbalimbali za nchi zingine huweka alama nyekundu tembezi za kutahadharisha katika tovuti za balozi zao alama ziitwazo kwa kiingereza "Marquee sign" ambayo hujitokkeza kila sekunde.

Pia alama zingine zinazoashiria mabadiliko ni zile ziitwazo "News Alert" na pia taarifa zaidi za kusaidia wageni watarajiwa kupata msaada zaidi wa kuelewa kinachoendelea.

Tatizo jingine kubwa zaidi ambalo limelalamikiwa chinichini na wageni watarajiwa hao ni kitendo cha ubalozi huo kutopokea simu mbalimbali za maulizo au "enquiries" ambapo simu yaweza ikaita siku nzima na kisha kwenda katika sehemu ya mzungumzaji au switchboard ambapo pana maelezo mengi ya jinsi ya kupata huduma kwa kubonyeza namba toka 1 hadi 4.

Mpigaji simu anapochagua moja ya namba hizo khasa namba 2 au 3 kuambiwa asubiri na kwamba yupo kwenye msururu na kisha simu hiyo ya ubalizi hukata bila kutarajia.

Hali hiyo imekuwa ikisababisha usumbufu kwa wageni wengi ambao wengine wanaishi katika miji mingine ambapo huanza kufikiria kusafiri hadi London ili kuweza kuulizia shida zao zinazohusiana na maombi yao ya viza.

Kwa upande wa watanzania ambao wengi wao wamefanya maombi yao kuanzia mwezi wa August wamekuwa wakikumbana na tatizo hilohilo la simu kutopokelewa inapopigwa kiasi cha kuleta masuali kwamba huenda wahusika wanaogopa au wanakwepa kwa makusudi kuzungumza lugha ya kiingereza na kujibu masuali kadha wa kadha.

Katika kutatua tatizo hlo ubalozi ungeweza kuweka options mbalimbali katika switchboard yake kwa kuelekeza nini kifanywe na wapigaji simu.

Au pia kwa upande wa watanzania, ubalozi unaweza kutumia njia ya ujumbe wa maandishi au text messages alert kuwataarifu wale watanzania ambao pasi zao za kusafiria zinakuwa zimekwisharudi ubalozini kutoka Tanzania.

Hivyo basi katika mwaka mpya ujao wa 2020 ni budi ubalozi wetu ubadilike na kuendana na kasi ya matumizi ya mawasiiano iwe ni ujumbe mfupi wa maandishi au barua pepe.

Pia Ubaloizi waweza kabisa kujiunga na mitandao kama facebook na twitter ambapo mawasiliano na watanzania yanakuwa yapo au "available" wakati wowote.

Ikumbukwe kwamba Ubalozi wa Tanzania nchini Uingereza ni moja ya balozi muhimu sana kwa nchi yetu na unatakiwa khasa katika eneo la ajira uwe makini na aina ya watumishi inaowaajiri.
 
Kama wamepata kazi kwa vyeti feki hayo ndiyo madhara yake yaani mpaka uwe mweupe au msukuma
 
Huu upumbavu upo hata hapa nyumbani! Unapiga simu huduma kwa wateja kampuni ya simu X kwa kutumia menu ya kiingereza ukitarajia kuwa maongezi yatafanyika kwa kiingereza lakini ghafla unasikia; Unaongea na Metui Mesayanyika kutoka ______makao makuu...tafadhali naongea na nani, kutoka wapi na karibu nikusaidie! Yaani yote hayo mhudumu ameyaongea chini ya sekunde 3.
Sasa kwenye kuomba kazi vigezo vya communication skills, language skills, interpersonal skills & interfacing skills sijui huwa wanaweka vya nini! Na sijui vigezo gani vinatumika kwenye recruitment!
Yaani hii nchi kuna mambo yanachekesha na kusikitisha sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huu upumbavu upo hata hapa nyumbani! Unapiga simu huduma kwa wateja kampuni ya simu X kwa kutumia menu ya kiingereza ukitarajia kuwa maongezi yatafanyika kwa kiingereza lakini ghafla unasikia; Unaongea na Metui Mesayanyika kutoka ______makao makuu...tafadhali naongea na nani, kutoka wapi na karibu nikusaidie! Yaani yote hayo mhudumu ameyaongea chini ya sekunde 3.
Sasa kwenye kuomba kazi vigezo vya communication skills, language skills, interpersonal skills & interfacing skills sijui huwa wanaweka vya nini! Na sijui vigezo gani vinatumika kwenye recruitment!
Yaani hii nchi kuna mambo yanachekesha na kusikitisha sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
Unataka kuwatest kwa kimombo lazima wakupige chenga tu
 
Vilaza ndio huamini wenzao ni vilaza. Kuzoea lugha na lafudhi yake ni kitu kirahisi Sana hasa Kama unaishi katika mazingira sawia ya lugha hiyo. Mtu wa ubalozini humchukua mwezi mmoja tu kuzoea lafudhi ya lugha hasa Kiingereza ambacho tunakitumia pia hapa nyumbani.
 
Vilaza ndio huamini wenzao ni vilaza. Kuzoea lugha na lafudhi yake ni kitu kirahisi Sana hasa Kama unaishi katika mazingira sawia ya lugha hiyo. Mtu wa ubalozini humchukua mwezi mmoja tu kuzoea lafudhi ya lugha hasa Kiingereza ambacho tunakitumia pia hapa nyumbani.

Sasa ataizoea vipi ligha hiyo kama hayupo tayari kuisikiliza kutoka kwa watu mbalimbali wenye lafudhi tofauti kupitia simu?
 
Huu upumbavu upo hata hapa nyumbani! Unapiga simu huduma kwa wateja kampuni ya simu X kwa kutumia menu ya kiingereza ukitarajia kuwa maongezi yatafanyika kwa kiingereza lakini ghafla unasikia; Unaongea na Metui Mesayanyika kutoka ______makao makuu...tafadhali naongea na nani, kutoka wapi na karibu nikusaidie! Yaani yote hayo mhudumu ameyaongea chini ya sekunde 3.
Sasa kwenye kuomba kazi vigezo vya communication skills, language skills, interpersonal skills & interfacing skills sijui huwa wanaweka vya nini! Na sijui vigezo gani vinatumika kwenye recruitment!
Yaani hii nchi kuna mambo yanachekesha na kusikitisha sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
Niliwahi kujaribu hii. Nilicheka mpaka basi, nilipoongea broken kdg nikatajiwa jina langu na kuambiwa iwapo nina shida zaidi nikate simu kisha nipige tena.
 
Sirembi,huu ni ubalozi muhimu mno kiuchumi,hao maofisa wa kitengo hicho WAPUMZISHWE,AU KUONDOLEWA KABISA.
mbona wapo vijana wenye hari na kazi.
 
Vilaza ndio huamini wenzao ni vilaza. Kuzoea lugha na lafudhi yake ni kitu kirahisi Sana hasa Kama unaishi katika mazingira sawia ya lugha hiyo. Mtu wa ubalozini humchukua mwezi mmoja tu kuzoea lafudhi ya lugha hasa Kiingereza ambacho tunakitumia pia hapa nyumbani.
Kwenye redio RFA mtangazaji alishindwa kusoma neno Deluxe treni ya kwenda Moshi na kutamka dei luksi! Huyo dada aliniacha hoi. Mwingine jana Radio One matangazo ya vifo lililomhusu mkurugenzi wa kampuni moja Kurasini mtangazaji mdada tena alishindwa kusoma neno superintendent! Haya ni baadhi tu ya maneno madogo watangazaji wa Tanzania wanashindwa kuyasoma, aibu.
 
Nikiwa mwenyeji wa Nchi yangu pendwa Tanzania. Nawatetea kuwa sio kwamba wanakwepa kingereza ila MASHIRIKA YOTE YA SERIKALI NCHINI KWETU HAWANA TAMADUNI YA KUPOKEA SIMU .hadi najiuliza hivi wanaandikaga namba za nini?
Ukipata muda jaribu kupiga simu kama vile NECTA,NACTE,HESBL,NHIF, na mengine utapata jibu
 
Kama wamepata kazi kwa vyeti feki hayo ndiyo madhara yake yaani mpaka uwe mweupe au msukuma
Yaani kwa maoni yako haya inaonekana ukipewa wewe nafasi hii, hata ofisini hutakaa achilia mbali kupokea simu. Hii yote itakuwa ni kuogopa kukutana na wateja kwani hutajua unatakiwa uongee nao vipi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sasa ataizoea vipi ligha hiyo kama hayupo tayari kuisikiliza kutoka kwa watu mbalimbali wenye lafudhi tofauti kupitia simu?
Mnajua lakn balozi zetu huwa na watu wangapi? Kuna
1. Balozi mwenyewe
2. Mwambata wa maswala ya Fedha
3. Mwambata wa maswala ya Ulinzi
4. Na mwingine
Hao ndio notable people wenye kuweza kuwa na majibu ya maswali ya watu. Wengine wanaweza kuwa makarani ambao Mara nyingi sio raia wa Tanzania. Kwa kiwango hicho Cha Understaff inategemea nini nyakati za pressure ya kazi?
 
Back
Top Bottom