jitombashisho
JF-Expert Member
- Jun 11, 2020
- 667
- 2,242
Wapo madereva na wafanyabiashara wanaohitaji msaada wakati huu pale mpakani mwa Rwanda na Kongo,Gisenyi almaarufu GRAND BARRIER.
Watumishi wengi Watanzania wahudumuo kwenye mission maalum ya Usalama upande wa Kivu kaskazini wanaweza kutumiwa kuwaokoa ndugu zao endapo team leader atawasiliana na mamlaka za UN na za kwetu kidiplomasia ili kuwaokoa ndugu zetu.
Ikumbukwe, Nchi za wenzetu mara yatokeapo majanga kama hayo huwa hawachelei kusaidia ndugu zao.
Mfano Nchi zote za magharibi tokea jana usiku raia wao wamewahifadhi maeneo salama juu ya Goma huku wakisubiri utaratibu maalum wa kuvushwa kwa helicopter upande wa Rwanda,Gisenyi na huko wataabiri ndege maalum zilizoandaliwa na watapelekwa Kinshasa hadi pale dhahama hiyo itapokoma.
Watumishi wengi Watanzania wahudumuo kwenye mission maalum ya Usalama upande wa Kivu kaskazini wanaweza kutumiwa kuwaokoa ndugu zao endapo team leader atawasiliana na mamlaka za UN na za kwetu kidiplomasia ili kuwaokoa ndugu zetu.
Ikumbukwe, Nchi za wenzetu mara yatokeapo majanga kama hayo huwa hawachelei kusaidia ndugu zao.
Mfano Nchi zote za magharibi tokea jana usiku raia wao wamewahifadhi maeneo salama juu ya Goma huku wakisubiri utaratibu maalum wa kuvushwa kwa helicopter upande wa Rwanda,Gisenyi na huko wataabiri ndege maalum zilizoandaliwa na watapelekwa Kinshasa hadi pale dhahama hiyo itapokoma.