opportunist2012
Member
- Feb 8, 2012
- 92
- 8
Tukiwa tunaelekea siku ya kupinga vitendo vya ubaguzi duniani,hali bado ni mbaya katika idara ya elimu ya sekondari manispaa ya Bukoba.Afisa elimu sekondari wa manispaa,afisa taaluma pamoja na baadhi ya wakuu wa shule waendeleza ubaguzi,upendeleo na ukabila katika kuwahudumia walimu walioajiriwa katika manispaa ya Bukoba.Ubaguzi huu uko wazi wazi kwani Afisa elimu anadiriki kuwateua walimu anaotoka nao kijiji kimoja,kabila moja au anaosoma nao pamoja Open University kila katika fursa yenye malipo:iwe semina,kusimamia mitihani ya kitaifa na hata kusahihisha mitihani hiyo.Huku walimu wasiokuwa na uhusiano wa kikabila,kimaeneo na hata kidini wakiachwa bila kuteuliwa kufanya shughuli mbalimbali zinazoongeza kipato.Hali hii imewafanya walimu wanaobaguliwa kukata tamaa kabisa ya kufanya kazi.Wengi wao wanafikiria kuhama au kuacha kazi hii ya ualimu.Walimu wanaoteuliwa kwa sababu ya ukabila,undugu kutoka kijiji kimoja hamna hata siku moja waliokosa kuteuliwa kufanya shughuli hizo maalum yaani kusimamia mitihani,semina na kwenda kusahihisha mitihani.Sidhani hii ndo ile Tanzania aliyoitaka hayati Baba wa Taifa Mwalimu JK Nyerere.Sielewi kwanini viongozi wanafumbia macho hali hii ovu ya ubaguzi unaokwenda kinyume na katiba ya nchi yetu.