Ubaguzi wa rangi: Mnigeria auawa huko Italia

chinchilla coat

JF-Expert Member
May 16, 2016
5,107
10,961
150128133533_italian_police_640x360_epa_nocredit.jpg


Hili wimbi la kufanyia vitendo vya chuki na kuuwa watu weusi linaendelea, kutoka India, hadi Marekani na sasa Italia

Polisi nchini Italia wamemtia mbaroni mwanamme mmoja anayeshukiwa kumpiga hadi kufa mhamiaji mmoja raia wa Nigeria katika shambulizi la kibaguzi kwa misingi ya rangi.

Emmanuel Chidi amekuwa akiishi Italia tangu mwaka wa 2015, baada ya kutoroka vita nchini Nigeria.

Emmanuel Chidi alivamiwa siku ya jumanne alasiri katika mji Fermo alipokuwa akitembea na mkewe.

Ripoti zinasema raia mmoja wa Italia alimtusi mkewe Chidi matusi ya kibaguzi .

Matusi hayo yalichochea mvutano.

Mwanamme huyo raia wa Italia kwa jina Amedeo Mancini baadaye alimshambulia Chidi kwa kutumia chuma.

Chidi aliaga dunia siku moja baadaye.

Maafisa wa polisi sasa wamemkamata mwanamme huyo na kumshtaki kwa makosa ya maauji yasio ya kukusudia, yaliyochochewa na ubaguzi wa rangi.

Mauaji hayo yamelaaniwa vikali kote nchini Italia.

Waziri mkuu wa Italia bwana Matteo Renzi, amelaani vikali mauaji hayo na kusema kuwa waitaliano wote wanapaswa kupinga ubaguzi wa rangi.

Wengi wanahofia kwamba huenda ikawa ishara ya taharuki inayotokana na wahamiaji wengi wanaopewa hifadhi nchini humo kutoka barani Afrika.

Chanzo: BBC
 
Wewe chinchila coat ndio mfia wazungu, you were defending mauaji ya blacks marekani kwenye thread ingine. I saw your comment
 
Wewe chinchila coat ndio mfia wazungu, you were defending mauaji ya blacks marekani kwenye thread ingine. I saw your comment
Mimi sio mfia mzungu waa muafrika au muarabu ni upuuzi, mimi nilikua nashangaa hii attitude ya watu weusi na wanavyofanyiana violence wao kwa wao kisha hakuna anayejali wala kuandamana, hadi auwawe na mzungu ndio dunia inasimama
 
Mimi sio mfia mzungu waa muafrika au muarabu ni upuuzi, mimi nilikua nashangaa hii attitude ya watu weusi na wanavyofanyiana violence wao kwa wao kisha hakuna anayejali wala kuandamana, hadi auwawe na mzungu ndio dunia inasimama

That is violence, hata wao weupe kwa weupe wanafanyiana violence, the issue is kuuana kwa sababu ya rangi ya mtu ndio tatizo, weusi ni victim wa mauaji kisa rangi zao duniani pote sio marekani tu.
 
That is violence, hata wao weupe kwa weupe wanafanyiana violence, the issue is kuuana kwa sababu ya rangi ya mtu ndio tatizo, weusi ni victim wa mauaji kisa rangi zao duniani pote sio marekani tu.
Violence ya weupe kwa weupe sio kubwa na ikitoea huwa inakemewa wa nguvu sana... ila watu weusi sijui wanajiona wana thamani wakiuawa na mzungu tuu!!!??
 
Back
Top Bottom