Ubaguzi wa kisiasa anaouonesha Magufuli hadi CCM wenyewe wanamshangaa

Tabutupu

JF-Expert Member
Nov 26, 2010
13,108
18,326
Tumekua tukisikia kwamba mkuu wa nchi ni mbaguzi hasa linapokuja swala la mitazamo ya kisiasa, kitu ambacho si kuzuri na hakifai kwa mkuu wa nchi.

Tofauti na viongozi wengine, hata marais waliopita, Mheshimiwa hapa amefeli na inaonyesha anafanya makusudi.

Jana akiwa Msoga, diwani wa hilo eneo aliitwa atoe kero. Mh akadhani ni diwani toka chama cha Chadema kwa sababu hakuvaa sare ya CCM, akaamuru anyang'anywe mic na maneno makali juu lakini baada ya kuuliza chama gani akaambiwa ni wa CCM, mara moja akaamuru arudishiwe mic na aendelee kuongea.

Leo tarehe 29 June 2020 akiwa Kilosa akaanza kumponda mbunge wa eneo na kusema wananchi wa eneo hilo wanachagua kwa jazba akiamini mbunge wa eneo hilo ni wa Chadema. Anaongeza kwa kusema yeye angekua mbunge wa eneo hilo angekua amemaliza changamoto zote ila kwa sababu wananchi wanachagua kwa jazba na wanachagua wabunge sio, ndio maana bado changamoto zipo.

Baadaye akauliza mbunge wa hapo anaitwa nani na wa chama gani? Wananchi wakamtaja na kumwambia anatoka chama chamapinduzi. Bila hata aibu akaanza kumsifia na kuahidi kuzimaliza changamoto hizo akisadiwa na waziri husika.

Wananchi wa Tanzania sio watoto wanajua na wanaelewa vizuri, wao wanapendana bola kujali vyama, dini wala kabila lakini bado kuna viongozi karne hii wanasimamia ubaguzi.

Naamini mh Rais ana nia njema na Tanzania, lakini bado ana nafasi ya kuondoa hurka hii ya ubaguzi hata kama chadema walimpa wakati mgumu 2015.

Rais ndio kiungo pekee cha kuwaunganisha Watanzania.

Sio sababu ya yeye kuendelea kubagua vyama vya upinzani hali kazi zake alizo zifanya zinaonekana.

Haya mambo madogodogo yanamuondolea kitu fulani kama kiongozi.

Tuungane kuupinga ubaguzi. Na asilazimishe vyama vya upinzania kupata ajenda.






Prof Jay
 
Mleta mada huna hoja kabisa, unakalia majungu, mwageni data mmefanya nini tangu 2015? Mmekosa vitu vya kusema mmebakiza majungu, mnasubiri Jemedari wetu kasema nini ndiyo mnapata vya kuongea.
 
Tabutupu,

Magufuli ni Mbaguzi hadi anakera ....anaweza kufanikiwa kushinda na kupitisha wabunge wake kwa nguvu ..tena "wake" sio wa ccm lakini atakayeingia mwaka 2025 itakuwa ngumu sana kwake ...awe wa chama chochote ..kurudisha umoja wa kitaifa ...huwezi kuwabagua watanzania namna hii , hatukuzoea kabisa ....hii ni laana

Na kama amesoma picha wananchi wanaanza kukereka na hii tabia ...
 
Rais wetu ni mwanademokrasia nyie Wapinzani acheni kutafuta sababu za uwongo
Km mmeshindwa hoja mjipange 2025

Anayoyafanya chuki na nongwa ya wazi dhidi ya cdm yapo wazi. Sisi ni watu wazima na tunaona mwenendo wake. Kibaya zaidi hiyo chuki yake binafsi, anatumia vibaya madaraka yake kuagiza taasisi za kimamlaka kufanya kwa kadiri ya utashi wake.

Na taasisi za kimamlaka kutokana na katiba mbovu, zinatii atakacho ili kutekeleza matakwa ya rais kwa ajili vya kulinda vibarua vyao. Mahakama na jeshi la Malawi viligoma kutekeleza utashi wa rais aliyekuwa madarakani, kwani wanajitambua.
 
Halafu na kwa hali hii ya upendeleo anaouonesha naanza kukubali huyu mwamba bila shaka October atatumia nguvu kubwa sana wasirudi bungeni iwe mbunge au diwani wa upinzani halagu baada ya hapo katiba inabadilishwa anakua rais mpaka kifo..hii janja janja ya kusema atastaafu 2025 nimeanz kuikataa.
 
Na leo eti anasema anashukuru lijuakali yupo, japo wakati wabunge wa ccm wanaongea wananchi walikua kimya.. ila aliposimama mbunge wa mikumi bwana haule toka chadema hadi wananchi wamesimama kumchangilia na akaongea point tupu.
Mpaka inabidi awatumie kina Mbatia wafanye siasa za kumsujudia, ili awape viti vya upendeleo.
 
Back
Top Bottom