Kashaijabutege
JF-Expert Member
- Oct 20, 2010
- 2,696
- 740
1.Mwanaume akiagiza kuku mzima, chipsi sahani tano, mayai kumi, na soda kubwa (2ltrs) mbili, miwa, ndizi mbivu, n.k na akala na kuvimaliza watu wanamsifia kuwa mwanaume anafukia. Akifanya hivyo mwanamama, mtaa mzima utajua na hata mmewe atapigiwa simu kama wadaku wanamjua. Kwa nini iwe hivyo?
2. Mwanaume akitembea na wanawake 6 kwa siku, sio ajabu sana kama akifanya hivyo mwanamke. Kwa nini inakuwa hivyo?
3. Mwanaume akioa wanawake wengi na kuacha haiwi kituko kama mwanamke akiachika mara nyingi. Kwa nini?
4.Mwanamme akila ulabu akajiegesha barabarani, haiwi kituko kama akifanya hivyo mwanamke. Kwa nini?
2. Mwanaume akitembea na wanawake 6 kwa siku, sio ajabu sana kama akifanya hivyo mwanamke. Kwa nini inakuwa hivyo?
3. Mwanaume akioa wanawake wengi na kuacha haiwi kituko kama mwanamke akiachika mara nyingi. Kwa nini?
4.Mwanamme akila ulabu akajiegesha barabarani, haiwi kituko kama akifanya hivyo mwanamke. Kwa nini?