Ubadhirifu wa USD 400,000 za Sekta ya Afya: Philip Mpango alikuwa wapi mpaka aambiwe na Global Fund wenyewe?

Stuxnet,
Ukishadhibiti uhuru Wa habari,ukamtimua CAG mzalendo Assad,Huku ukiubinya upinzani usikohoe,mafisadi kina dau wakitunukiwa ubalozi wakazitumbue vizuri,wenye ushahidi wa video wa rushwa wakikumbatiwa ,huku mahakama ya mafisadi ikiota nyasi uhitaji kujiuliza jibu
 
Hivi serikalini kuna watu wengine watu walisomea kuiba? Mbona watu wizi, rushwa na ubadhilifu haukomi?
Tabia asili yetu kuanzia wenye maslai bora hadi wenye maslai duni,watawala wanaibia wananchi,baba anapiga ofisini anampa mama mama anapiga anasaidia kwao,dada wa kazi nae anapiga anatuma kwao,jamii nzima ni wapigaji kuanzia juu hadi chini.Ufisadi,wizi,upigaji,rushwa ndo chanzo cha ufukara wetu
 
Ukishadhibiti uhuru Wa habari,ukamtimua CAG mzalendo Assad,Huku ukiubinya upinzani usikohoe,mafisadi kina dau wakitunukiwa ubalozi wakazitumbue vizuri,wenye ushahidi wa video wa rushwa wakikumbatiwa ,huku mahakama ya mafisadi ikiota nyasi uhitaji kujiuliza jibu
Huyu CAG wa sasa aliyekuwa TRA yeye ni CAG kivuli
 
Tabia asili yetu kuanzia wenye maslai bora hadi wenye maslai duni,watawala wanaibia wananchi,baba anapiga ofisini anampa mama mama anapiga anasaidia kwao,dada wa kazi nae anapiga anatuma kwao,jamii nzima ni wapigaji kuanzia juu hadi chini.Ufisadi,wizi,upigaji,rushwa ndo chanzo cha ufukara wetu
Du kwa comment hii watoto ndio waathirika wakuu sasa. Hawapati huduma kama baba yao alivyokusudia.
 
Kama kuna ubadhirifu Global Fund wamegundua kupitia taarifa za kaguzi ambacho watakuwa wanahoji ni hatua kutochukuliwa kwa wakati. Ikumbukwe kuwa Taarifa ya CAG ya kuishia 30/6/2018 ndio sasa inajadiliwa na Bunge linaloendelea. Taarifa ya kuishia 30/9/2019 itajadiliwa Bungeni 2021
 
Bajeti ya sekta ya Afya inafadhiliwa na na mataifa ya Ulaya na America kwa takriban 80%. Yaani kwa kila Shillingi inayotumika kutibu binadamu Tanzania, Senti 80 imaletwa na wafadhili kwenye dawa za ukimwi, malaria, Kifua Kikuu, Uzazi wa Mpango, Chanjo za watoto na magonjwa yaliyo sahauliwa.

Unashangaa nchi tegemea kama hii, wafadhili hao hao wakiuliza kuhusu utawala bora tunawaita mabeberu.
Utawala bora, bora, bora, kila siku! Jiulize ni nini wanachotaka kuona ili wakiite utawala bora? Usilazimishe kuona kisichokuwepo. We unaamini US inaheshimu utawala bora wa nchi zingine. Tuna matatizo ya maisha tnasingizia wengine. Tukiona anayetusaidia kuzomea, tunaunga mkono bila kujua anazomea nini!
 
Pascal Mayalla, Leo pesa zikitolewa kwa ajili ya madawati, ukazitumia kuwekea milango ya madarasa tayari ni matumizi mabaya.

Hivyo yy kama Waziri ilipaswa kujua je pesa zimefanya kazi kusudiwa* ama LA na yy ni mmojawapo waliozipeleka katika matumizi yasiyo sahihi...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watumishi wa umma wanajua kula na kipofu, Wanapiga mpunga uku wanampigia mapambio. AWAMU HII YA TANO NDIO YA MAJIZI HAIJAWAHI KUTOKEA
Yani kabisaa tunakula nankipofu ukopita huku serikali kuu na kwenye almashauri saaa hv wote tuna kadi ya kijani. Alafu post zetu insta na fb ni full kusifia awamu.

Mfano mimi washkaji zangu insta wananizodoa sana kwakusifia utawala kumbe hawajui najitengezea kamrija fulani.
 
absolutely true mkuu
Kwa mazingira ya kukataa kukosolewa na kuzuia shghuli za kisiasa na Uhuru wa kutoa maoni na vitisho vinavyotolewa serikali ya awamu ya tano' itajikuta ndio serikali ambayo ina janga kubwa la rushwa na ufujaji/ufisadi kuliko awamu zote ambazo aidha zinaigusa Ikulu yenyewe au taasisi zake au watumishi wake.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom