Ubadhirifu Jijini Dar es Salaam: Alaumiwe RC Makonda au Madiwani wanaoendesha Manispaa?

Alex Fredrick

JF-Expert Member
Jun 21, 2016
680
1,338
Hivi majuzi Rais Magufuli alifanya ziara ya gafla kwenye ujenzi wa machinjio ya kisasa vingunguti Jijini Dar es Salaam.

Kwa maelezo ya Mh Rais Magufuli ni kwamba kupitia mradi huo wa ujenzi wa machinjio kuna ufisadi mkubwa umefanyika.

Leo tena katika dhifa ya kuwaapisha Viongozi Ikulu amerudia swala hilo kwamba jengo la ghorofa moja linajengwa kwa zaidi 14 Billion.

Sanjali na hilo pia Mh Rais Magufuli amezunguzia harufu ya Ufisadi mwingine kwenye ujenzi wa fukwe za Coco Beach jijini Dar es Salaam.

Baada ya rejea hizo zote naona mashambulizi mengi kwa RC Makonda kana kwamba yeye ndiye mhusika Mkuu wakati Jiji hili linangozwa na Meya kupitia vikao na Madiwani.

Watu wa kulaumiwa ni Madiwani ambao ndio wanapanga bajeti na kuidhinisha hiyo miradi, na sisi Wananchi kimsingi ndio tunawachagua kupitia masanduku ya kura.

RC Paul Makonda anaweza kuwa na madhambi yake mengine lakini tuache'"vijiba' vya roho kwa vitu ambavyo vipo wazi kwamba tunajua au tunapotosha makusudi kwakuwa tu tunamchukia huyu Kijana


Alex Fredrick
Dar es salaam
 
Kebwe yeye kule moro ndo alikuwa anaongoza vikao vya madiwani?

Hivi unajua Mamlaka ya mkuu wa mkoa kwenye usimamizi wa miradi ya maendeleo kwenye mkoa wake?
Tofauti kubwa kati ya Jiji na Mkoa,Kwa Jiji kama Dar es salam ni ngumu labda ahonge Madiwani kwenye Manspaa zote ambapo kuna miradi husika. Morogoro ni pesa zilitoka Serikali kuu zikaingia Direct kwenye Halmashauri ambapo DED ndio mwenye Fund kwahiyo Mkuu wa Mkoa husika rahisi kujua au kukagua
 
Tofauti kubwa kati ya Jiji na Mkoa,Kwa Jiji kama Dar es salam ni ngumu labda ahonge Madiwani kwenye Manspaa zote ambapo kuna miradi husika. Morogoro ni pesa zilitoka Serikali kuu zikaingia Direct kwenye Halmashauri ambapo DED ndio mwenye Fund kwahiyo Mkuu wa Mkoa husika rahisi kujua au kukagua
Dar kuna Hamshauri kama Moro.
Tena pengine ungemtetea wa Moro kwa sababu ana halmashauri nyingi kuliko wa Dar na ni rahisi kujua nini kinafanyika Jijini kuliko yule wa Moro kwa sababu ya changamoto za 'miundombinu'.

Bila kusahau ukiacha manispaa kuna Halmashauri ya jiji zima na ukubwa wa mradi. Kwa hiyo ni rahisi kwa mfuatiliaji.

Kwa mfano Rais anaongoza Nchi nzima lakini ni rahisi kujua kwa haraka madudu ya mradi wa Vingunguti na kushughulikia kuliko mradi wa soko huko Makambako kwa sababu ya Dar kama uso wa Nchi.

Kwa hapa Makonda alitakiwa kuwa makini sana
 
Mkuu wa mkoa wa Morogoro syo Diwani ila amewajibishwa kwa uzembe uliofanywa na watendaji wake, hivyo lawama zoote zimuendee Makonda kwa kushindwa kuusimamia mkoa wake.

Rais ambaye ni mkuu wa nchi aneweza kuona udhaifu ktk miradi hyo kwanini Makonda ambaye ni rais wa mkoa hakuona?
 
Dar kuna Hamshauri kama Moro.
Tena pengine ungemtetea wa Moro kwa sababu ana halmashauri nyingi kuliko wa Dar na ni rahisi kujua nini kinafanyika Jijini kuliko yule wa Moro kwa sababu ya changamoto za 'miundombinu'.

Bila kusahau ukiacha manispaa kuna Halmashauri ya jiji zima na ukubwa wa mradi. Kwa hiyo ni rahisi kwa mfuatiliaji.

Kwa mfano Rais anaongoza Nchi nzima lakini ni rahisi kujua kwa haraka madudu ya mradi wa Vingunguti na kushughulikia kuliko mradi wa soko huko Makambako kwa sababu ya Dar kama uso wa Nchi.

Kwa hapa Makonda alitakiwa kuwa makini sana
pamoja na hayo inaweza kuwa anamtafutia makonda sababu ya kumtoa,uchaguzi uko njiani kuna kundi linalengwa kurafurahishwa na tukio la kumtumbua yetu macho,tusubiri tuone
 
RAIS MAGUFULI: ILIKUWA TUFUKUZE VIONGOZI WOTE WA MKOA WA MOROGORO KUANZIA MKUU WA MKOA MPAKA MTENDAJI WA KIJIJI

"Mkoa wa Morogoro ilikuwa tuufanyie demo, tunafukuza kuanzia juu mpaka chini, Unaanza na Mkuu wa mkoa mpaka mtendaji wa kijiji, wote wanaondoka siku moja, halafu siku hiyo hiyo utangaza orodha ya viongozi wengine, tunaanza na watu fresh, mpaka Waziri Mkuu anakuja Morogoro anaoona milango mibovu kwenye kituo cha afya, Mkuu wa mkoa upo, RAS upo, DC upo, hivi Waziri Mkuu atatembelea mikoa mingapi?" - Rais John Magufuli
 
Baada ya rejea hizo zote naona mashambulizi mengi kwa RC Makonda kana kwamba yeye ndiye mhusika Mkuu wakati Jiji hili linangozwa na Meya kupitia vikao na Madiwani
WEWE ndo RC wa Dar?. Haihitaji rocket science kuona ufisadi kwenye mradi ule.
Mosi- serikali ilitenga 12.5 bn kutekeleza mradi, RC ndiye aliyechagua kampuni ya kutekeleza mradi kwa 14 bn--------'-', mpaka hapo hujaona fisad na ufisadi?



Huyo unayemtetea ni fsad na mradi hauna tija
 
RAIS MAGUFULI: ILIKUWA TUFUKUZE VIONGOZI WOTE WA MKOA WA MOROGORO KUANZIA MKUU WA MKOA MPAKA MTENDAJI WA KIJIJI

"Mkoa wa Morogoro ilikuwa tuufanyie demo, tunafukuza kuanzia juu mpaka chini, Unaanza na Mkuu wa mkoa mpaka mtendaji wa kijiji, wote wanaondoka siku moja, halafu siku hiyo hiyo utangaza orodha ya viongozi wengine, tunaanza na watu fresh, mpaka Waziri Mkuu anakuja Morogoro anaoona milango mibovu kwenye kituo cha afya, Mkuu wa mkoa upo, RAS upo, DC upo, hivi Waziri Mkuu atatembelea mikoa mingapi?" - Rais John Magufuli
Mi nadhani DSM ni hovyo kuliko Morogoro
 
Paul Makonda kapata mtihani mgumu wenye majibu mepesi.

Lakini Makonda alishasema njaa ndio shida, vinginevyo angeandika barua ya kuachia ngazi.
Sasa Magu anatumia weakness au uoga wa Makonda kumchana hadharani.

Lakini Makonda kaficha makucha ni mzoefu wa kupambana na vigogo, kama Lowassa na Warioba.
 
Hapa siyo kulaumiwa bali ni kuwajibika. Mh Rais mwenyewe kasema mambo yanafanyika utadhani hakuna Mkuu wa Mkoa wala Mkuu wa Wilaya na Wakurugenzi.

Makonda halaumiwa bali anawajibika kwa kuwa Mkoa upo chini yake. Kwani huwa humsikii akisema Wananchi wangu wa mkoa wangu wa Dasalaama?
 
pamoja na hayo inaweza kuwa anamtafutia makonda sababu ya kumtoa,uchaguzi uko njiani kuna kundi linalengwa kurafurahishwa na tukio la kumtumbua yetu macho,tusubiri tuone

Mkuu utaniambia kwa sababu zisizozuilika Makonda lazima atatumbuliwa ili wavuke salama kwenye uchaguzi wa 2020 ingawa uamuzi huo utakuwa ni muendelezo wa usanii uliozoeleka tu na baada ya muda atapewa shavu jipya la mpaka 2025
 
Kuna upigaji wa namna fulani Makonda anaufanya na huenda haya yeye alidukuliwa akawa na lugha tata ambazo mkuu hakuzipenda. Siku za karibuni inaonekana mkuu katumbukiwa nyongo na huyo Makonda, ila maagano yao ndio yanamfunga, huenda akamtumbua lakini ni katika kuosha nyota ya kisiasa zaidi.
 
Haijalishi nani kafanya miradi Dar ikija kufanikiwa yeye mkuu wa Mkoa anachukuwa sifa kama kiongozi mkuu wa mkoa na yakija madudu ajuwe kubeba lawama. Ukiona kiongozi yoyote anaanza kujikosha na kunyosha kidole kwa watu wake wa chini huyo sio kiongozi mzuri ni mbinafsi. Kiongozi bora anawajibika kiujumla kwa mazuri na mabaya.
 
Hakuna ufisadi mkuu acha kipamba mambo. CAG ndio anaweza thibitisha hilo na sio rais. Hata nyumba ya chini inaweza jengwa kwa 14b inategemea na quality. Swala la coco beach pia inategemea unahitaji structure aina gani. Unaweza ukatumia hata mil 2 ukitaka. Nashauri jengo liishe ndio useme hili jengo si la kiasi flani ya pesa zilizotumika ila si sasa hata kifusi bado.
 
Kwa hiyo unabishana na rais km yeye anashangaa mradi ule uchukue 14b ww unaona sawa tu huoni km hauko sawa mkuu
Hakuna ufisadi mkuu acha kipamba mambo. CAG ndio anaweza thibitisha hilo na sio rais. Hata nyumba ya chini inaweza jengwa kwa 14b inategemea na quality. Swala la coco beach pia inategemea unahitaji structure aina gani. Unaweza ukatumia hata mil 2 ukitaka. Nashauri jengo liishe ndio useme hili jengo si la kiasi flani ya pesa zilizotumika ila si sasa hata kifusi bado.
 
Back
Top Bottom