Ubabaifu wa Precision Air kiutendaji

Ze burner

JF-Expert Member
Jan 5, 2011
514
83
nimekuwa nikisikia malalamiko ya muda mrefu kutoka kwa wateja wao ila baadaye nami yalinikuta. tatizo la flight delay, bei isiyotabirika, kukosa nafasi ukiwa na ticket mkononi, poor customer care na mengineyo yote hayo ndiyo utamaduni wao. labda kwa sababu wengi wa waajiriwa wao ni watoto wa mafisadi ukweli wanachosha sana...

mnamo mwezi kama wa julai hivi mafisadi hawa wakaamua kuanza safari zao za usiku DAR - NAIROBI - MWANZA na kukifanya kiwanja cha mwanza kitambulike kuwa kinafanyakazi masaa 24. vyema ila walifanya hivyo bila maandalizi yoyote ni mwendo wa kukurupuka tu. abiria kama kawaida tukafurahia huduma za usiku licha ya huduma mbovu za jini hili. na kutokana na mwenendo na maandalizi mabovu tulijua fika kuwa safari hizo zina mwisho coz mara ndege inaingia saa mbili, mara saa nne mara haipo nk.

Hatujakaa vizuri tay ari tumeshapokea taarifa kuwa safari hizo za usiku kutokea nairobi hazipo, na hivi ndivyo hali ilivyo sasa.

Hivi jamani wana jf tujiulize. kuna kitu kama vile "cooperate social responsibility" ambacho ni kitu cha msingi sana kwa wawekezaji kweli jini hili linatekeleza wajibu huo. kwani naona ikiwa hata haki za mteja hazitekelezwi na hakuna anaejali hivi haki ya kijamii kwa ujumla kweli inatekelezwa? binafsi sijawahi kusikia Precision air imefanya kitu fulani kwa jamii sijui wenzangu. na hi kampuni kweli ni ya kitanzania maana hafadhali kampuni nyingine za kikenya zinajali kuliko hii. jee wana jf kweli hii kampuni inafanya vizuri au ndo basi tu??
 
nimekuwa nikisikia malalamiko ya muda mrefu kutoka kwa wateja wao ila baadaye nami yalinikuta. tatizo la light delay, bei isiyotabirika, kukosa nafasi ukiwa na ticket mkononi, poor customer care na mengineyo yote hayo ndiyo utamaduni wao. labda kwa sababu wengi wa waajiriwa wao ni watoto wa mafisadi ukweli wanachosha sana...

mnamo mwezi kama wa julai hivi mafisadi hawa wakaamua kuanza safari zao za usiku DAR - NAIROBI - MWANZA na kukifanya kiwanja cha mwanza kitambulike kuwa kinafanyakazi masaa 24. vyema ila walifanya hivyo bila maandalizi yoyote ni mwendo wa kukurupuka tu. abiria kama kawaida tukafurahia huduma za usiku licha ya huduma mbovu za jini hili. na kutokana na mwenendo na maandalizi mabovu tulijua fika kuwa safari hizo zina mwisho coz mara ndege inaingia saa mbili, mara saa nne mara haipo nk.

Hatujakaa vizuri tay ari tumeshapokea taarifa kuwa safari hizo za usiku kutokea nairobi hazipo, na hivi ndivyo hali ilivyo sasa.

Hivi jamani wana jf tujiulize. kuna kitu kama vile "cooperate social responsibility" ambacho ni kitu cha msingi sana kwa wawekezaji kweli jini hili linatekeleza wajibu huo. kwani naona ikiwa hata haki za mteja hazitekelezwi na hakuna anaejali hivi haki ya kijamii kwa ujumla kweli inatekelezwa? binafsi sijawahi kusikia Precision air imefanya kitu fulani kwa jamii sijui wenzangu. na hi kampuni kweli ni ya kitanzania maana hafadhali kampuni nyingine za kikenya zinajali kuliko hii. jee wana jf kweli hii kampuni inafanya vizuri au ndo basi tu??

bomu kabisa hawa
 
Tunasubiri alizoahidi Mh Nundu labda huo urasimu utaisha. ilishatokea tuko airport kwa safari ya kutoka mwanza kwenda dar saa 2 usiku lakini hapakuwa na mtu hata kwenye benchi lao wa kutoa feedback
 
Wanaliendesha shirika lao kwa kubabaisha na kubahatishabahatisha. Maranyingi tu nimetumia PW na kumekuwa na flight cancellations/delays zisizo na kichwa wala miguu. On top of that ndege zao nyingi choka mbaya yaani mtu ukifika mwisho wa safari unamshukuru Mungu. Customer service ndio ujeuri mtupu kuanzia counter hadi air hostesses.
 
Dah! delays hata hizo za ulaya naona ni uharo mtupu. Anyway wajirekebishe kama ndivyo walivyo. Ujumbe umefika.
 
kwa kweli labda tusubiri hiyo kampuni yetu ya walala hoi mana dah! halafu kuna ushahidi kabisa kuwa hawa jamaa wanawazuia kampuni nyengine kufanya kazi. kwa mfano kampuni ya 540 ilipata shida sana kufanya kaza kwa rout za ndani coz jamaa wanapiga majungu kwa mafisadi wenzao, kampuni y a jetlink nayo imeshindwa kabisaaa.....
siku moja nilikwenda kufanya booking then kama robo saaa hivi nikarudi na hela kilichotokea duh. fare imeongezeka kwa laki nzima within robo saa baada ya kuwaeleza kilichotokea na kuonesha kushindwa hiyo fare mpya walikubali nilipe bei ya awali. wanatisha hawa jamaa
 
Na hata imeanza kukosa wateja kwa kasi kubwa,ofice zao ulikuwa ukiingia unakuta foleni kubwa ya wageni toka nje na wabongo wakihitaji huduma,ila sasa kumedoda,itakufa soon!!
 
Na hata imeanza kukosa wateja kwa kasi kubwa,ofice zao ulikuwa ukiingia unakuta foleni kubwa ya wageni toka nje na wabongo wakihitaji huduma,ila sasa kumedoda,itakufa soon!!

Du! haya tena makubwa, ina maana sisi tulionunua vishea huko tumeliwa?
 
Na hata imeanza kukosa wateja kwa kasi kubwa,ofice zao ulikuwa ukiingia unakuta foleni kubwa ya wageni toka nje na wabongo wakihitaji huduma,ila sasa kumedoda,itakufa soon!!
ukweli ni kwamba mbadala wa ndege zilizopo hazitoshi vyenginevyo wangelibakia mafisadi peke yao. yaani mpaka unapanda precision unahuzunika ila basi tu.
 
roho zenu za kwanini ndozinawasumbua, the company is doing great setting the model for local investors. kama unatakapromote bidhaa yako, sema mazuri yake/ sio kuponda ya mwenzio.......
 
Kwanini mmeileta hii baada ya ATCL kutaka kuanza kujiimarisha tena au ndiyo mpango mkakati wa ATCL umeanza kwa kuanza kuishambulia Precision Air?. Ni mawazo tu!
 
roho zenu za kwanini ndozinawasumbua, the company is doing great setting the model for local investors. kama unatakapromote bidhaa yako, sema mazuri yake/ sio kuponda ya mwenzio.......
tena mkuu kuna taarifa za ndani kabisa kutoka shirika lenyewe kwamba tayari marubani wapatao watatu wameshakimbia kampuni hii na kusababisha ndege zao ikadhaa kutoruka na kupelekea usumbusu kwa abiria wake. we sema linaendelea vizuri tu. au na wewe ni mtoto wa fisadi nini?
 
Kwanini mmeileta hii baada ya ATCL kutaka kuanza kujiimarisha tena au ndiyo mpango mkakati wa ATCL umeanza kwa kuanza kuishambulia Precision Air?. Ni mawazo tu!
ukweli mzee ndo unabaki hivyo hivyo. tena kwa uhakika kabisa ni kwamba hizo ndege za kampuni ya ATCL zitajaa kupita kiasi the same to 540. tatizo ni kwamba kampuni pinzani zinakuja na ndege chache vyenginevyo hao ndugu zako wangeambulia patupu.
 
Hawafai kabisa hawa precision,naweza sema ndio shirika la ndege linaloongoza kwa ubabaishaji duniani,hawajali kabisa wateja wao,na mzigo hata ukizidi kg 1 utatozwa pesa tena huku wakikukejeli.ila ikianza atcl na 540 nawakawa wanatoa huduma nzuri naya uhakika basi precision ya mafisadi kina mramba itakufa haraka sana.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom