Uanzishwaji wa Mahakama ya Kadhi uende sambamba na kuanzisha Mahakama ya Kikristu

mmaroroi

JF-Expert Member
May 8, 2008
2,960
544
Kwa kuwa sasa Serikali imeifanya Tanzania nchi yenye Dini kinyume na sheria(Katiba) basi ianzishe pia Mahakama ya Kikristu.Serikali isiwachanganye watanzania kwa kusema Tanzania haina dini huku ikiendekeza udini.
 
Kwa kuwa sasa Serikali imeifanya Tanzania nchi yenye Dini kinyume na sheria(Katiba) basi ianzishe pia Mahakama ya Kikristu.Serikali isiwachanganye watanzania kwa kusema Tanzania haina dini huku ikiendekeza udini.

waislamu wengi waliipigia kura ccm na wakristo wengi chadema, sasa mahakama ya kadhi ni sera ya ccm waliouziwa waislamu hivyo ni haki yao kuipata na wakristo kama nao wanataka mahakama ya kikristo ambayo naamini haipo kiuhalisia basi nao wanahaki kuwa nayo lakini ni kichekesho kwa wakristo kudai hiyo mahakama mara tu waislamu watakapoipata!!!

hii ni sawa na tabia ya watoto wadogo ambao huoneana wivu ikiwa mmoja kamuomba baba ake amnunulie chupi ya rangi nyeupe na mwingine atataka anunuliwe chupi kama hiyo!!!!
 
waislamu wengi waliipigia kura ccm na wakristo wengi chadema, sasa mahakama ya kadhi ni sera ya ccm waliouziwa waislamu hivyo ni haki yao kuipata na wakristo kama nao wanataka mahakama ya kikristo ambayo naamini haipo kiuhalisia basi nao wanahaki kuwa nayo lakini ni kichekesho kwa wakristo kudai hiyo mahakama mara tu waislamu watakapoipata!!!

hii ni sawa na tabia ya watoto wadogo ambao huoneana wivu ikiwa mmoja kamuomba baba ake amnunulie chupi ya rangi nyeupe na mwingine atataka anunuliwe chupi kama hiyo!!!!


Kwanza ni lazima iwekwe wazi sababu ya kutaka mahakama ya kadhi ianzishwe? Then hapo tunaweza kuanza kuongea mengine, mahakama ya wakristo inaweza kutengenezwa pia, na hii ya kawaida waachiwe wapagani.

Ni matusi kusema waislamu waliipigia kura CCM na wakristo waliipigia kura CHADEMA. Kuna waislamu wengi walioipigia kura CHADEMA na wakrito wengi waliipigia kura CCM. Sera ya udini si nzuri.
 
Katiba yetu inasema nchi yetu haina dini. Siungi mkono kujadili masuala ya kidini kwa mtizamo huo. Suala la mahakama ya kadhi waliongelee waislam wenyewe kwenye misikiti yao siyo humu jf wala mitaani.
 
biashara ya udini kalasi inatumiwa na mafisadi ili waibe na kuifisadi tanzania na watanzania wachache wasio jitambua wanaupigia debe Biashara iliyopo sasa ni kati ya walio nacho na wasio nacho hii biashara itatugharimu haibagui dini kabila chama au rangi maana wanaotesa na kuteseka ni hao hao huteseki kwa kuwa ni mkristo au mwislamu ima cuf au chadema MAVUVUZELA WA MAFISADI JITAMBUENI maana mchuma janga HULA NA WANAE!
 
Islamic law na canon law zote zipo kwenye sheria zetu sasa kwanini kuwepo na mahakama ya kadhi?
 
kwanza ni lazima iwekwe wazi sababu ya kutaka mahakama ya kadhi ianzishwe? Then hapo tunaweza kuanza kuongea mengine, mahakama ya wakristo inaweza kutengenezwa pia, na hii ya kawaida waachiwe wapagani.

Ni matusi kusema waislamu waliipigia kura ccm na wakristo waliipigia kura chadema. Kuna waislamu wengi walioipigia kura chadema na wakrito wengi waliipigia kura ccm. Sera ya udini si nzuri.

siamini kama ni tusi kusema waislamu wengi waliipigia kura ccm na wakristo waliowengi waliipigia kura chadema ni kiwa nasababu zifuatazo:

1)ccm ilipata kura nyingi sana maeneo wanamoishi waislamu wengi, mfano; mkoa wa pwani, tanga, dar, zanzibar, tabora, singida, dodoma, mtwara, lindi na ruvuma.
2)ccm ilizoa kura nyingi za urais baadhi ya maeneo ya mijini wanamoishi waislamu wengi,mfano; kondoa, morogoro,same mjini, mwanga mjini, moshi mjini, arusha mjini, bukoba mjini, iringa mjini, mwanza mjini, kigoma mjini, singida mjini, na dodoma mjini.
3) chadema walipata kura nyingi sana maeneo wanamoishi wakristo wengi, mfano, kilimanjaro,arusha, mwanza, shinyanga, mara, kagera, iringa, kigoma, rukwa, na maeneo wanamoishi wakristo wengi ktk jiji la dar, mfano; kinondoni na kawe.
4) chadema walipata kura chache sana ktk maeneo wanamoishi waislamu wengi , mfano; zanzibar, na mikoa yote ya ukanda wa pwani!
5) kufungwa kwa nyumba za ibada siku ya uchaguzi ni dalili tosha za kuegemea upande wa chadema kwa sababu kipindi cha kampeni kulitolewa kauli nyingi toka kwa viongozi wa makanisa kuwaelekeza waumini wao ni kiongozi gani anaefaa kuchaguliwa!

sasa sijui ni ushahidi gani mwingine utakaokuridhisha! Na huu uoga sijui watu wengine wanaupata wapi! Yaani ukitaja dini fulani tu, hapo ni kosa!! Unaambiwa wewe ni mdini, au unataka kuleta chuki na vita vya kidini!!! Yaani nashindwa kuelewa!! Tanzania ukitaja vitu viwili ni mwiko!!! Dini na muungano!!!! Na sijui ni nani alieturoga na vitu hivi viwili!!!

umefika wakati sasa wa kujadili mambo haya kwa uwazi kabisa bila ya uoga na kigugumizi kwa sababu tuna katiba yetu inayolinda dini na watu wake!!
 
Kwanza ni lazima iwekwe wazi sababu ya kutaka mahakama ya kadhi ianzishwe? Then hapo tunaweza kuanza kuongea mengine, mahakama ya wakristo inaweza kutengenezwa pia, na hii ya kawaida waachiwe wapagani.

Ni matusi kusema waislamu waliipigia kura CCM na wakristo waliipigia kura CHADEMA. Kuna waislamu wengi walioipigia kura CHADEMA na wakrito wengi waliipigia kura CCM. Sera ya udini si nzuri.

hivi Halima James Mdee ni dini gani? Naye ataheshimu mahakama ipi?
na Mbona (kama nilivyoambiwa) Pinda ameapa bila kushika Kurani, Bible au katiba. (mimi niko porini na sina umeme aliyeona vizuri anirekebishe ikiwa nimekosea)
 
sidhani kama wakristo waliipigia kura chadema wakti wakristo hao hao walikuwa wanasema ccm ni chaguo la Mungu. hapo hamueleweki...toka lini shehe alishawai kumsema vizuri candidate yeyote wa kikristo?...
 
Matusi acha kijana... Hiyo mahakama ya kadhi muianzishe kama taasisi ndani ya dini yenu wenyewe kwa gharama zenu wenyewe... Thats all... Lakini sio serikali iipitishe kisheria na kikatiba...maana nyie mnachotaka ni eti serikali igharamie kila kitu...

Serikali yetu ni ya ki-secular mkuu...kamwe haiwezi kuwa serikali ya waislam pekee.
waislamu wengi waliipigia kura ccm na wakristo wengi chadema, sasa mahakama ya kadhi ni sera ya ccm waliouziwa waislamu hivyo ni haki yao kuipata na wakristo kama nao wanataka mahakama ya kikristo ambayo naamini haipo kiuhalisia basi nao wanahaki kuwa nayo lakini ni kichekesho kwa wakristo kudai hiyo mahakama mara tu waislamu watakapoipata!!!

hii ni sawa na tabia ya watoto wadogo ambao huoneana wivu ikiwa mmoja kamuomba baba ake amnunulie chupi ya rangi nyeupe na mwingine atataka anunuliwe chupi kama hiyo!!!!
 
waislamu wengi waliipigia kura ccm na wakristo wengi chadema, sasa mahakama ya kadhi ni sera ya ccm waliouziwa waislamu hivyo ni haki yao kuipata na wakristo kama nao wanataka mahakama ya kikristo ambayo naamini haipo kiuhalisia basi nao wanahaki kuwa nayo lakini ni kichekesho kwa wakristo kudai hiyo mahakama mara tu waislamu watakapoipata!!!

hii ni sawa na tabia ya watoto wadogo ambao huoneana wivu ikiwa mmoja kamuomba baba ake amnunulie chupi ya rangi nyeupe na mwingine atataka anunuliwe chupi kama hiyo!!!!

Vipi mahakama ya kadhi imeshapatikana au bado CCM iliwalaghai na mkaamini kuwa itaanzishwa,lol wajinga ndo waliwao
 
And now is endless debate of mental slavery idelologies...people are blind of reality...you hate someone because of what you belive? Nonsense....how much are you sure that the white man or the arab man ideology is true..what was your ideology before slavery..why are you christian or muslim? What if you was vorn to a different family belief? Religions debates sucks...
 
WAISLAM WENGI TU WA MADHEHEBU MENGINE WANAPINGA MAHAKAMA YA KADHI

KHIDMAT DWAAT LISIAMIYAT CENTRE REGISTERED TRUSTEES
P. O. BOX 16106, MOB. 0713-290272, 0784-403020.


1. Uanzishaji wa Mahakama ya Kadhi utaleta madahara makubwa ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa vile Wakristo hawagawanyiki katika suala la kuipinga, lakini sisi Waislamu tunagawanyika katika suala hilo. Kwa taarifa yako napenda nikuhakikishie kuwa Waislamu wa Madhehebu ya AnsarSunna HAWAIKUBALI Mahakama hiyo kwa vile wanaelewa kuwa itakuwa chini ya BAKWATA.

2. Pia wanaelewa kuwa miongoni mwa mamlaka ya Kadhi ni kutangaza mwezi wa Ramadhani kufunga na kufungua na wao wanaye Amir wao ambaye hutangaza mwezi kwa kufuata mwezi unaoandama Saudia (Saud Arabia). Kwa maana hiyo katika nchi yenye Kadhi kutokea mtu mwingine nje ya Kadhi kutangaza mwezi ni kosa la jinai.

3. Kitu ambacho kitaleta madhara makubwa kuliko mafanikio ingawa AnsarSunna ni kundi dogo lakini wanaburuza kundi kubwa sana la Waislamu, kuliko Taasisi yoyote ya Kiislamu hapa Tanzania kwa vile ushawishi wao ni mkubwa sana katika jamii ya Kiislamu.

4. ANSAR SUNNA ndio wanaoendesha Shuura ya Maimam, GAZETI LA AN-NUUR, AL-HUDA, NASAHA na RADIO IMANI. Pia wana ushawishi mkubwa TIMES FM. Je, BAKWATA wana uwezo wa kupambana na vyombo hivyo?

5. Je, Serikali inaweza kukabidhi Mahakama ya Kadhi kwa wanaharakati wa Kiislamu? Nina hakika haiwezi kufanya jambo hilo na kama haitofanya hivyo Chama Cha Mapinduzi (CCM) kinaweza kupata hasara zifuatazo:
(a) Wakristo wote wanaweza kujitoa ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kujiunga katika chama cha CHADEMA ambacho hakina Mahakama ya Kadhi katika Ilani yake.
(b) Waislamu wote walioko chini ya Shuura ya Maimamu ambayo ni Mpinzani Mkuu wa BAKWATA wataendelea kuipinga Serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), kwa kuikumbatia BAKWATA na huku wakiendelea kuiunga mkono CUF, hivyo CCM itajikuta imebakia na Waislamu wanaoiunga mkono BAKWATA tu. Suala la wanaharakati kuipinga Mahakama ya Kadhi ni jambo rahisi sana kwa vile Mahakama ya Kadhi sio madai yao ya msingi.

6. Waislamu (wanaharakati) dai lao la msingi ni MGAWANYO SAWA WA MADARAKA. Hivyo Serikali inapounda Wizara, wao hutizama Baraza la Mawaziri, WAISLAMU NI WANGAPI NA WAKRISTO NI WANGAPI NDIO MAANA WANAIUNGA MKONO CUF, KWA VILE CUF IMEELEWA TATIZO LAO NA WAO WAKAJA NA KAULIMBIU YA HAKI SAWA KWA WOTE, yaani kwa Wakristo na Waislamu, wala Ilani ya Uchaguzi ya CUF haisemi lolote kuhusu Mahakama ya Kadhi WALA HAITOSEMA!!

7. Pia Waislamu wanaharakati wanaelewa kuwa Mahakama ya Kadhi haina manufaa yoyote kwa Waislamu, kwa vile Zanzibar ipo na WAISLAMU WA ZANZIBAR HAWANA MAENDELEO YOYOTE KUWAPITA WALE WA BARA, NA UISLAMU SI NDOA NA MIRATHI TU WALA MUNGU HASEMI "SOMETHING IS BETTER THAN NOTHING." Huu ni msemo wa Wazungu.

8. Mwenyezi Mungu anasema: INGIENI KATIKA UISLAMU WOTE NA MSIFE BALI MMEKUWA WAISLAMU KAMILI (Surat Baqarah ya 2 aya ya 208). Kwa hiyo mimi nikiwa kama Mwislamu nashauri kuwa Mahakama hiyo ISIWEPO kwani haitakuwa na manufaa kwa Chama cha Mapinduzi (CCM) na italeta mgawanyiko miongoni mwa wanachama wako, chukulia mfano Zanzibar, Mufti na Kadhi wanavyopingwa na wanauamsho ambao wanaongozwa na Sheikh Farid hali wanauamsho ndio Shura ya Maimam na Shuura ya Maimam ndiyo Uamsho.


KWANINI MASHEIKH WA BAKWATA WANAITAKA?
9. Wanaelewa wanachokifanya, wao wanajua fika kuwa Serikali itakapoanzisha Mahakama ya Kadhi watakuwa wamepata AJIRA, kwa hiyo wao wanapigania maslahi yao tu, hawawezi kuangalia madhara yatakayokikumba Chama Cha Mapinduzi (CCM) na huku wakijua kuwa ushawishi wao ni mdogo katika Jamii ya Kiislamu na hawana hata Miundumbinu ya kuwashawishi Waislamu wote waweze kumkubali Mufti, na hali ya Mufti ameshaweka wazi milango kwa Taasisi zote za Kiislamu na Waislamu waje washirikiane naye.

10. Masheikhe hawa wanaelewa kuwa hakuna Hakimu anayehukumu makosa mawili tu, yaani NDOA na MIRATHI, ukiletewa mzinifu huruhusiwi kumhukumu, ukiletewa mwizi huruhusiwi, nk. lakini wanang'ang'ania hivyo hivyo kwa ajili ya mishahara tu na hiyo ni hatari.

11. Hujaribu kutoa hata mifano ya Serikali ya Uingereza kwamba mwaka 1920 iliweka Mahakama hizo, ukweli ni kwamba Serikali ya Uingereza haikuweka Mahakama za Kadhi tu bali za Maakida na Maliwali, lakini pia sababu ya kuziweka Mahakama hizo siyo kwa ajili ya kuutunza Uislamu au uliwali bali ilikuwa ni mbinu ya kuwatuliza Viongozi hao ili waweze kuwatawala bila vurugu kwani mkoloni aligundua kuwa ni watu wenye ushawishi katika jamii kwa hiyo ile ilikuwa ni mbinu ya kiutawala ili Masheikhe, Maliwali na Maakida wajione kuwa na wao ni sehemu ya Serikali ya Muingereza, kumbe ni watawaliwa, hivyo bado hoja hiyo haina msingi wowote wala haina maana kwamba Serikali ya Mkoloni ilikuwa nzuri kwa Waislamu kuliko hii ya CCM, na huku tukiambiwa kuwa Waislamu ndiyo walioanzisha harakati za kudai Uhuru, kama walikuwa wazuri kwa nini tuliwaondoa.

12. CCM inayo mambo mengi ya kujivunia kwa Waislamu kama vile kuwapatia Chuo Kikuu, na hilo ni jambo muhimu na la msingi kwa maendeleo ya Uislamu na Waislamu, kwa hiyo JAMBO HILO LA MAHAKAMA YA KADHI mnapaswa kuliangalia kwa umakini ijapokuwa limo ndani ya Ilani yenu. Lakini si kila jambo lililomo ndani ya Ilani litekelezwe, mengine yanaweza kushindikana kwa matatizo mbalimbali na hili ni tatizo kubwa KWANI LINAWEZA KUZAA MGOGORO WA KIDINI!!

WAKRISTO WANA HAKI YA KUPINGA MAHAKAMA YA KADHI
13. Sehemu kama Zanzibar ni rahisi kuweka Mahakama ya Kadhi kwa vile Waislamu kule ni asilimia 99.99 hali kama hiyo Wakristo kule ni kama hawapo wamemezwa kwa uchache wao. Lakini BARA NI PAGUMU kwa vile HUENDA WAKRISTO NI WENGI KULIKO WAISLAMU. KWA VILE WAISLAMU KWA UHAKIKA HUPATIKANA MIKOA ISIYOZIDI SITA AMBAYO NI DAR ES SALAAM, LINDI, TANGA, MTWARA, KIGOMA NA TABORA, pia katika mikoa hiyo siyo Wilaya zote, kwa mfano Mkoa wa Kigoma ni Ujiji na Kigoma Mjini tu.

14. Pamoja na hayo Masheikhe wa BAKWATA wanaoshikilia suala la kuwepo kwa Mahakama ya Kadhi bado hawajafahamu nini tatizo la Wakristo, hata hawakubali kuwepo kwa Mahakama hiyo, siyo kweli kabisa kwamba Wakristo hudhani Mahakama hizo zitawahukumu wao, la hasha na Masheikhe hutumia muda mwingi kuwaelimisha juu ya hilo, wakati hilo sio tatizo lao, na ni udhaifu wa kutokujua madai au matatizo ya mpinzani wako, ni nini tatizo la Wakristo ni hili:

(a) Mkumbuke kwamba mwaka 1993 hapa Tanzania kulikuwa na mgogoro wa bucha za nguruwe, mgogoro huo ulizaa harakati kubwa za Waislamu ambazo makao yake makuu yalikuwa msikiti wa Mtoro na kiongozi mkuu alikuwa marehemu Kasim bin Juma. Waislamu walipinga kuwepo Ubalozi wa Vatican hapa Tanzania na bado wanaendelea na msimamo huo hadi leo, wakati ubalozi huo hauendeshwi kwa Fedha za walipa kodi wa Tanzania bali ni Vatican yenyewe. JE, ITAKUWAJE LEO WAKRISTO WAKUBALI ZIWEPO MAHAKAMA AMBAZO ZITATOA AJIRA KWA WAISLAMU, KUANZIA MTAA, KATA, TARAFA, WILAYA, MKOA HADI TAIFA, TENA KWA FEDHA ZA WALIPA KODI WA TANZANIA WAKIWAMO NA WAO WAKRISTO? Hilo ndilo tatizo lao na hapo ndipo BAKWATA wanatakiwa wapatolee maelezo.

(b) Kwamba, mabilioni ya Watanzania yatakayowalipa Masheikhe kila mwezi nao wao watanufaikaje? Huo ndio mgogoro uliotengenezwa na Ilani yenu na ambao unaweza kuwagharimu katika uchaguzi ujao wa mwaka 2010 ENDAPO WAKRISTO WAKIIGA MFANO WA WAISLAMU WA MSIKITI WA MTORO walipoamua kukusanya Kadi za CCM mwaka 1993 ingawa jaribio hilo lilizimwa na Viongozi wa CCM.

HOJA ZA SHEIKH BASALEH
15. Sheikh Ali Basaleh ndiye ambaye amelielewa tatizo la Maaskofu ingawa ametoa mfano mzuri wa kuwatuliza katika kipeperushi chake cha Wito cha tarehe18/08/2006. Ijumaa kuwa kama mtu ana watoto wawili mmoja anakula sana na mwingine hali sana, Je, baba atamzuia yule anayekula sana ili alingane na yule asiyekula sana? Mfano wake ni mzuri lakini haufanani na tatizo lililopo kwani fedha za baba hazichangiwi na watoto wake, bali baba huzitafuta yeye mwenyewe kwa nguvu zake, LAKINI FEDHA ZA BABA SERIKALI ZINATOKANA NA KODI YA WAISLAMU NA WAKRISTO, HIVYO SERIKALI HAIPASWI KUTUMIA FEDHA NYINGI KWA DINI MOJA LAZIMA ITALETA MGOGORO NA NDIYO MAANA SISI WAISLAMU TUMEKUWA TUKIDAI HAKI SAWA!

16. Katibu Mkuu ni matumaini yangu kuwa hekima itatumika katika kulitatua tatizo hilo kwani ni rahisi kuziba ufa kuliko gharama za kujenga ukuta mwisho nakutakia kazi njema pamoja na afya njema.

WABILAH TAUFIQ,
ASANTE.
USTADH A. S. MKAMBAKU,
KATIBU MKUU.

Mungu akubariki, akupe maisha marefu kama aliyompa nabii musa, miaka 120 huku anaona vizuri kama kijana wa miaka 20! Umefafanua kwa kirefu na kwa upana ambao mtu mwenye ufahamu mzuri ni lazima aelewe ili kuepusha machafuko ktk nchi yetu, hakuna kitu kizuri kama kufanya shughuli zako ukiwa huru, hukohuko tumeozeshana, ni marafiki, bussinespatner, tutaangalianaje!? ulaku wa madaraka usitugawe watanzania, tuwe sawa kwenye madaraka, kuna watu wanashabikia bila kujua madhara yake, hawajifunzi na majirani zetu, mwisho wa ugomvi wa vita vya kidini kitachofuata ni ukanda na ukabila, MUNGU IBARIKI TANZANIA TUBAKIE NA AMANI YETU, AMEN.
 
Serikali haina dini. Japo kuwa Wananchi wanazo dini zao. Kuingiza mahakama za dini fulani katika mifumo ya Serikali ni kuifanya Serikali kuwa na dini. Tena dini ya imani ya hiyo mahakama ya mahakama ya dini itakayoanzisha.

Sasa hoja ni utawazuiaje Mabudhist wakitaka kuanzisha Mahakama za Dini yao? Wakristo kadhalika?

Waislam ndugu zangu anzisheni Mahakama hizo kwenye mfumo wenu wa Kiislam huko misikitini.

Kamwe pasitokee Mkristu mwenye kudai uchuro huo wa migawanyiko. Eti Mahakama ya Kijesuit!
 
Kwa kuwa sasa Serikali imeifanya Tanzania nchi yenye Dini kinyume na sheria(Katiba) basi ianzishe pia Mahakama ya Kikristu.Serikali isiwachanganye watanzania kwa kusema Tanzania haina dini huku ikiendekeza udini.
Kadhi court is diabolical and inhumane
 
Back
Top Bottom