Uandikishaji majengo nyumba kwa nyumba kuanza karibuni

Crocodiletooth

JF-Expert Member
Oct 28, 2012
18,631
20,966
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Selemani Jafo amesema kuanzia tarehe 15 hadi 28 Februari wataendesha kampeni ya kuorodhesha majengo yote nchini ili wamiliki wake waweze kulipa kodi.

Jafo amebainisha hayo jana mkoani Morogoro kwenye uzinduzi wa kiwanda cha kufungasha mazao jamii ya kunde ambapo mgeni rasmi alikuwa Rais Dk John Magufuli.

Aidha, Jafo amesema kuwa zoezi hilo halitazihusu taasisi za dini bali wamiliki wa majengo wa kawaida.

“Kwahiyo niwaombe watanzania kuanzia Jumatatu tunaanza kampeni itakayoisha tarehe 28 mwezi huu na mimi pamoja na watendaji wakuu wangu wote tutashiriki zoezi hili tunataka tuorodheshe majengo yote ndani ya Tanzania ukiachilia majengo ya dini ili tuweze kulipa kodi kwa mustakabali wa nchi yetu” amesema Jafo.

#Mngetupumzisha watanzania tukabaki walau na akiba ya kununulia malimao na tangawizi

jaffo.jpg
 
Back
Top Bottom