mashishanga
JF-Expert Member
- Sep 16, 2016
- 611
- 427
Nije kwenye mada, inawezekanaje mwanamke uliyekua unampenda, unamjali ambaye ulikua unahisi bila yeye maisha yako hayawezi kwenda, anafanya kakosa kidogo badala yakukaa kuongea, basi unaanza kurusha matusi, dharau, makofi na ngumi?
Tena kipigo na hizo dharau unazionyesha mbele ya watoto, wakati mwingine mwanaume anachukua fimbo anaanza mchapa kama mtoto! Niulize, hivi wanaume hufanya hivyo kumlinganisha mkeo na mtoto au ni uonevu kwakuwa mwanamke hawezi kurudisha ngumi? Au kupiga na dharau ndio uanaume unajulikana?
Nimeleta hili maana ninaona threads nyingi watu wanajisifia kupiga wapenzi wao. Mara utasikia "mke bila kupiga hakuna penzi". Ni nini kinasababisha asilimia kubwa ya wanaume kufanya hivi? Hivi ukimwambia mkeo/mwenzio kuwa sipendi hichi hawezi kuelewa? Maana wako wanawake wamepata vipigo kwa wapenzi wao na waume zao hadi wakafa.
Tena kipigo na hizo dharau unazionyesha mbele ya watoto, wakati mwingine mwanaume anachukua fimbo anaanza mchapa kama mtoto! Niulize, hivi wanaume hufanya hivyo kumlinganisha mkeo na mtoto au ni uonevu kwakuwa mwanamke hawezi kurudisha ngumi? Au kupiga na dharau ndio uanaume unajulikana?
Nimeleta hili maana ninaona threads nyingi watu wanajisifia kupiga wapenzi wao. Mara utasikia "mke bila kupiga hakuna penzi". Ni nini kinasababisha asilimia kubwa ya wanaume kufanya hivi? Hivi ukimwambia mkeo/mwenzio kuwa sipendi hichi hawezi kuelewa? Maana wako wanawake wamepata vipigo kwa wapenzi wao na waume zao hadi wakafa.