Uamuzi wa wabunge wa CHADEMA kutohudhuria Bunge na kujiweka karantini ni sahihi kabisa

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,478
30,140
Wiki iliyopita Mwenyekiti wa Chadema, Mheshimiwa Freeman Mbowe, alilitangazia Taifa kuwa wabunge wa Chadema, hawataendelea tena na vikao vya Bunge na wameamua kujiweka karantini kwa siku 14, ili kuangalia afya zao kama wameambukizwa ugonjwa huu wa COVID 19 au laa

Ni uamuzi wa busara kabisa waliochukua wabunge hao na ndiyo unaosisitizwa sana na shirika la afya la dunia (WHO) wa kujali afya yako na ya wengine.

Sasa kituko kimekuja baada ya hao Chadema kutoa tamko hilo, ambapo lilipokelewa kwa vitisho vya hali ya juu kutoka kwa watawala wetu

Alianza Rais Magufuli akiwa kijijini kwake Chato, wakati anamwapisha waziri wa sheria na Katiba, jumapili iliyopita alipotamka hadharani kuwa amemuagiza Spika wa Bunge, awakate posho zao wabunge wote waliosusia vikao hivyo!

Akaja Spika Ndugai mwenyewe, akawaambia wabunge hao warudishe posho hizo za per diem na sitting allowances, kabla hajalikabidhi suala hilo kwa vyombo vya usalama, ili waweze kushughulikiwa kama wahalifu wengine wa jinai!

Akafuatia Mkuu wa mkoa wa Dar, Paul Makonda, ambaye alikwenda mbali zaidi, kwa kutoa amri kwa wabunge wote wa Chadema, waliokuja jijini kwake, warudi Bungeni kwao ndani ya saa 24, ama sivyo atawakamata kama wazururaji, aliowafananisha na machangudoa!

Hapo ndipo ninapojiuliza maswali kadhaa, hivi hawa wabunge wa Chadema, si wamechukua hatua hiyo ya tahadhari ili kuokoa maisha yao na ya wale wanaokaribiana nao, ambalo ndilo jambo linalisisitizwa sana na WHO??

Tukumbuke pia hao wabunge wa Chadema ndicho kilikuwa kilio chao kikubwa sana kwa kumuomba Spika wa Bunge aruhusu wabunge wote wapimwe ugonjwa wa COVID 19 kabla yya kuendelea na vikao hivyo na Spika Ndugai, akawagomea!

Hivi kwa mazingira hayo ya Bunge kupoteza wabunge wake 3 ambao wamefariki katika kipindi kisichozidi wiki 2 hivi kwa uamuzi waliochukua wabunge wa Chadema, bado unaonekana siyo wa busara kweli??

Kwa maoni yangu uamuzi uliochukuliwa na wabunge wa Chadema ni wa busara sana kwa kuokoa maisha yao na ya wale wanaokutana nao kila siku
 
Mystery,

Tuna watawala wa ajabu,Tatizo hatuna viongozi Bali tuna watawala waliojificha kwenye kitu kinaitwa utawala Bora badala ya uongozi bora.

Sent using Jamii Forums mobile app
Elice Elly
Inashangaza kwa wabunge wa Chadema kutamka hadharani kuwa wameamua kujiweka karantini ya siku 14, ili kuangalia afya zao na vile vile kuwaepusha wengine maambukizi ikiwa wao watakuwa na maambukizi.....

Hilo ndilo kosa kubwa la jinai, hadi watawala wetu mbalimbali wajitokeze na kupiga "mkwara" mzito wa kuwataka wabunge hao warejee Bungeni, ama sivyo wawe tayari kukosa posho zao??

This happens only in TZ!
 
Tatizo ni sisi Watz tulio wengi hatujitambui ndiyo maana hawa Watawala wanafanya watakavyo hata kwa kuvunja Sheria za Nchi. Siku tukizinduka usingizini ndiyo itakuwa mwisho wao wa kutuonea.

Hebu fikiria Kiongozi kama Makonda anatoa wapi ujeuri ule wa kuingilia kazi za Spika? Na Spika mwenyewe yuko kimya bila kumuita kwenye ile kamati yake ya kinga na maadili ya Bunge. Waziri Mkuu nae kimya Waziri wa Sheria na Katiba kimya Waziri wa Mambo ya Ndani kimya. Kwakuwa tu wanaoshughulikiwa ni Wapinzani ndiyo maana Katiba na Sheria za Nchi zinakiukwa wazi wazi.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni sahihi sana sana....hii ni serikali ya kishetani kabisa
Yaani anachofanya Spika Ndugai, ni sawasawa na kumlazimisha mtu aingie kwa nguvu kwenye "cage" ambako yupo simba mwenye njaa!

Kwa kuwa ni yeye mwenyewe Spika Ndugai, amegomea wabunge wote wasipimwe kipimo cha COVID 19
 
Elice Elly
Inashangaza kwa wabunge wa Chadema kutamka hadharani kuwa wameamua kujiweka karantini ya siku 14, ili kuangalia afya zao na vile vile kuwaepusha wengine maambukizi ikiwa wao watakuwa na maambukizi.....

Hilo ndilo kosa kubwa la jinai, hadi watawala wetu mbalimbali wajitokeze na kupiga "mkwara" mzito wa kuwataka wabunge hao warejee Bungeni, mama sivyo wawe tayari kukosa posho zao??

This happens only in TZ!
Wamefanya Jambo la kipuuzi bunge linaendelea wapo bungeni wanaleta ujinga wao kwani bunge limesimamishwa? Na Cha ajabu wakawa wanazurura na kukesha mabar kifupi wamekimbia majukumu yao
 
Ni muendelezo wa ujinga na upuuzi unaofanywa na chadema kifupi wamekurupuka
Screenshot_20200507-193453.jpg
 
Wamefanya Jambo la kipuuzi bunge linaendelea wapo bungeni wanaleta ujinga wao kwani bunge limesimamishwa? Na Cha ajabu wakawa wanazurura na kukesha mabar kifupi wamekimbia majukumu yao
Kama wewe unaona wamefanya kitendo cha kipuuzi na wapuuzwe..........

Inakuwaje kwa watawala wako hawaishi kutoa povu kwa kupiga mkwara mzito kuwa ni lazima wabunge hao warejee Bungeni na kuendelea na vikao hivyo??
 
Kila mtu hatakiwi kujiweka karantini.Kuna watu wanaweza kujiweka karantini na maisha yakaendelea.Sio lazima unywe Bar kipindi hiki,sio lazima uende msikitini au kanisani kipindi hiki.
Kila mtu akijiweka karantini nani atafanya kazi.? Manesi nao wanatamani kukaa karantini pamoja na askari. Wamekimbia wajibu wao tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama wewe unaona wamefanya kitendo cha kipuuzi na wapuuzwe..........

Inakuwaje kwa watawala wako hawaishi kutoa povu kwa kupiga mkwara mzito kuwa ni lazima wabunge hao warejee Bungeni na kuendelea na vikao hivyo??
Unauliza kwanini wanaambiwa warudi bungeni wakati unajua wametoroka bungeni Sasa nikujubu nini tena?,na utawala ulioko madarakani ni utawala wa wote mimi wewe yule sio utawala wangu tu ukisema utawala wangu labda wewe sio mtanzania ni mjinga tu ndio atachekelea upuuzi waliofanya wabunge watoro
 
Elice Elly
Inashangaza kwa wabunge wa Chadema kutamka hadharani kuwa wameamua kujiweka karantini ya siku 14, ili kuangalia afya zao na vile vile kuwaepusha wengine maambukizi ikiwa wao watakuwa na maambukizi.....

Hilo ndilo kosa kubwa la jinai, hadi watawala wetu mbalimbali wajitokeze na kupiga "mkwara" mzito wa kuwataka wabunge hao warejee Bungeni, mama sivyo wawe tayari kukosa posho zao??

This happens only in TZ!
Posho ni kitu gani? wameshakaa jela siku nyingi tu bila kupata posho. Serikali ipambane na corona na iache kupambana na CHADEMA!
 
Yaani anachofanya Spika Ndugai, ni sawasawa na kumlazimisha mtu aingie kwa nguvu kwenye "cage" ambako yupo simba mwenye njaa!

Kwa kuwa ni yeye mwenyewe Spika Ndugai, amegomea wabunge wote wasipimwe kipimo cha COVID 19
Cha kushangaza ndugai alishakubaliana na rais awe anawafukuza bungeni na yeye atadeal nao nje na wamefanya hivyo kwa miaka yote mitano lkn makamanda hawajayumba leo anawalazimisha kurudi bungeni.....HAWA MBWA WANAKERA SANA AISEE
 
Back
Top Bottom