Uamuzi wa kuoa au kuolewa, unaweza ukabadilisha utumishi wako na wito wako kabisa

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,462
21,334
Uamuzi wa kuoa au kuolewa, unaweza ukabadilisha
utumishi wako na wito wako kabisa
Ngoja nikutolee mfano wa kibiblia. Unamkumbuka mtu mmoja aliyeitwa Samson, alimwoa dada mmoja aliyeitwa Delila, utumishi wake ulinyongewa huko kwenye maisha yao ya ndoa. Ukisoma kile kitabu cha Waamuzi.16:21 kinasema hivi, “Wafilisti wakamkamata wakamng’oa macho, wakateremka naye mpaka Gaza, wakamfunga kwa vifungo vya shaba naye alikuwa akisaga ngano katika gereza”.
Unajua huyu alikuwa ni mtumishi wa Mungu mzuri kabisa. Lakini hakujua ya kwamba yule mwanamke aliyempenda na akamwoa aishi naye alikuwa ni ‘ajenti’. Hakujua ya kuwa yule dada alikuwa ni ‘ajenti’ wa adui. Yule dada alikuwa ni ‘ajenti’; kabisa akambembeleza mume wake amweleze siri ya nguvu zake, lakini Samsoni mwenyewe alikuwa anaficha kusema siri ya nguvu zake iko wapi. Lakini yule dada alikuwa na ujuzi wa kubembeleza. Akambembeleza yule baba kiasi ambacho akashindwa kuficha siri yake, na akaisema.
Unajua inapofika kwenye masuala ya ndoa inatakiwa muweze kusaidiana, mtu asitumie udhaifu wako kukuangusha, mtu asitumie udhaifu wako kukuzamisha, mtu asitumie makosa yako kukupeleka jehanamu, inatakiwa ukimpata mwenzako ukiwa na udhaifu akusaidie, ukiwa kwenye dhambi akuombee utoke, unaelekea jehanamu akusaidie kwenda mbinguni, ndivyo inavyotakiwa iwe kwenye ndoa.
Lakini ninakuambia ukimpata mtu, na wewe una maisha yanayoelekea jehanamu, anakuambia nenda salama, hii ni hatari. Yule dada alikuwa anamfuatilia Samsoni kumnyang’anya kitu kilichokuwa ndani yake cha utumishi alichokuwa amepewa na Mungu, na Samsoni hakujua. Alipofika mahali pa kuisema siri yake alifikiri mke wake ni mwenzake ambaye anaweza akampa siri yake vizuri bila shida.
Ndio maana kwenye ndoa ambazo watu hawaaminiani vizuri, siri zao hawaambiani. Na ikishafika kwenye ndoa, mnasiri mlizozifichana iko shida, maana yake kuna eneo ambalo usingetaka liingiliwe, unafunga na ufunguo, kasha unatembea na ufunguo mfukoni. Ni eneo umeficha, kwenye ndoa mnatakiwa mfahamiane kila siku, na udhaifu wako, na shida ilioko, na matatizo yaliyoko, kila kitu kiwepo peupe, ili mwenzako atafute namna ya kukusaidia.
Samsoni aliona kitu cha tofauti, lakini alikuwa mke wake, maadui wakaja wakamshika, mke wake anatazama na kushangilia. Badala ya Samsoni kumtumikia Mungu, akaenda akawa anasaga ngano gerezani. Biblia inasema wakamtoboa macho. Kwa jinsi ya rohoni ningekuambia, wanaondoa macho yako ya rohoni, maono ya Kimungu yanapotea, mtazamo wa Kimungu unapotea, mipango ya Kimungu inapotea.
Ndio maana unakuta mtu ameolewa ameokoka, au ameoa huku ameokoka, akifika ndani ya ndoa maono ya Kimungu yanapotea, na utumishi wake unazama. Anabaki kusema ‘Bwana asifiwe’, kama bado anaweza akaendelea kusema ‘Bwana asifiwe’, lakini ndani ya moyo amenyonywa kiroho na hakuna kitu.
Sasa labda na ninyi ni mashahidi, wewe angalia vijana ambao wameoa na kuolewa, angalia kama bado wanao moto ule ule wa utumishi, ambao walikuwa nao kabla hawajaingia kwenye ndoa. Wengine wanabaki kumsingizia Mungu ya kuwa, ameesbadilishia huduma, wakati sio Mungu, kumbe ni mume wake amembadilishia huduma, au ni mke wake tu amembadilishia huduma! Maana hakuhesabu gharama ya ndoa kwenye wito wake.
Kwa mfano; Mke wako anakutaka nyumbani, huduma inakutaka kila siku uwepo barabarani, usije ukafikiri ni kitu kirahisi hicho. Utafika mahali lazima uamue, unataka kumpendezesha mke wako au unataka kumpendezesha Mungu.Haya si mambo ambayo ni rahisi kuyaweka vizuri na kuyaanisha bila msaada wa Mungu. Na kama alikuwa anajua anaolewa wapi, kusumbuliwa suala la kusafiri kwako kwenye huduma lisingekuwepo, angekua anakutia moyo na kukuombea, na kukusindikiza siku nyingine. Lakini inapofika anaanza kupata shida, maana yake kuoana kwenu kuna kasoro mahali, na kumekuwa mzigo.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom