Uadilifu wa sitta ,magufuli na mwakyembe!

niweze

JF-Expert Member
Oct 21, 2009
1,008
116
Wanajamii na Wananchi Tuchimbe Uteuliwaji wa Sitta na Mwakyembe Wizarani kwa Undani Zaidi. JK Anafanya Kazi Sana Kipindi Hiki Kuimaliza Demokrasia ya Tanzania. Wananchi Hasa Sisi Tusiopendelea Sera za CCM Tulikuwa Tunafuatilia Sana Vitendo vya Sitta na Mwakyembe Bungeni. Ukweli Sitta Aliruhusu Discussions Bungeni Ambazo Bila Hiyo Ruhusa Lowasa na Wizi Mwingi Tusingezijua kwa Kina. Simsifihii Sana Sitta kwa Vitendo Vyake Tangu Huko Nyuma Ila Alionyesha Kuchoshwa na Wizi wa Humo CCM na Yeye Sitta Akaona Kuisaidia Inchi Yake ni Vizuri Aruhusu Discussions Bungeni Kufungua Mlango kwa Wabunge Wengine Ndani ya CCM Kuongelea Hizi Issues. Wabunge wa CCM Kama Kawaida Yao ni Usingizi na Kuchukua Posho ya Wananchi. Bure Tupu.......Sasa Sitta Kawekwa Wizara Ambayo Haina Impact ya Maana na Hawezi Kujua Siri Nyingi na Ripoti Nyingi Haruhusiwi Kuzisoma Kama Ilivyo Bungeni. Kwa Kifupi Kafungwa Mdomo kwa Kutumia Post ya Uwaziri..

Mwakyembe Pia Kateuliwa Wizarani ili Atoke Bungeni Kuondoa Maswali Bungeni. JK na Washahuri Wake Kingunge na Rostam Wamemueleza Akimwacha Mwakyembe Bungeni Kipindi Hiki Bungeni ni Hatari kwa CCM. Mwakyembe kwa Kifupi, Katiwa Kofuri Mdomoni kwa Kwenda Wizarani. Hawa Wabunge wa CCM Huko Bungeni ni Wamedharauliwa Kiasi Kwamba Wanaonekana Mbele ya JK ni Mifuko ya Karatasi Haina Kazi. JK Anategemea Kulala Kwao Bungeni Sio Kuwawakilisha Wananchi kwa Kuuliza Maswali. Yale Yale JK Achukue Pesa na Kwenda Retirement........Hamkeni CCM Mtalala Mpaka Lini? Kwani Hamna Ndugu Wanakufa na Shida Tanzania? Inchi Inawahitaji Sana Wakina Sitta na Mwakyembe Wengine.

Vita Jk Anavianzisha na Chadema. JK na Washahuri Wake CCM Watapata Kuishambulia Chadema Kama Wanavyotaka Kukiwa Hakuna Wauliza Maswali Kutoka CCM. Sisi Wananchi Tunatakiwa Tusupport Chadema na Uongozi Chadema Wahakikishe Wanakaa Pamoja na Kushirikiana. JK na CCM Wanataka Kuvuruga Chadema Kutumia Usalama wa Taifa na Pesa. CCM Walifanikiwa Kuua NCCR na Vyama Vingine Inchini kwa Vitendo Hivi. Wananchi Tusikubali Demokrasia Iharibiwa na Watu Wachache ili Waendelee Kuiba na Kuwaua Wananchi Mahospitalini Kila Leo. Kazi Moja ya Usalama wa Taifa TZ ni Kupeleleza Wananchi Wauliza Maswali Sio Kupeleleza Criminals. Hii Ndio Sera za CCM Kama People's Party in China. Kutumia Jeshi na Vyombo vya Ulinzi Kuwamaliza Wananchi Wako....Tutaona Itaishia Wapi Tena...
"Kwa Taarifa Yenu CCM... Chadema Haitakufa Kama NCCR na UDP Zilivyoundwa. Chadema ni Sawa na Wananchi Wote Tanzania"
 
Wanajamii na Wananchi Tuchimbe Uteuliwaji wa Sitta na Mwakyembe Wizarani kwa Undani Zaidi. JK Anafanya Kazi Sana Kipindi Hiki Kuimaliza Demokrasia ya Tanzania. Wananchi Hasa Sisi Tusiopendelea Sera za CCM Tulikuwa Tunafuatilia Sana Vitendo vya Sitta na Mwakyembe Bungeni. Ukweli Sitta Aliruhusu Discussions Bungeni Ambazo Bila Hiyo Ruhusa Lowasa na Wizi Mwingi Tusingezijua kwa Kina. Simsifihii Sana Sitta kwa Vitendo Vyake Tangu Huko Nyuma Ila Alionyesha Kuchoshwa na Wizi wa Humo CCM na Yeye Sitta Akaona Kuisaidia Inchi Yake ni Vizuri Aruhusu Discussions Bungeni Kufungua Mlango kwa Wabunge Wengine Ndani ya CCM Kuongelea Hizi Issues. Wabunge wa CCM Kama Kawaida Yao ni Usingizi na Kuchukua Posho ya Wananchi. Bure Tupu.......Sasa Sitta Kawekwa Wizara Ambayo Haina Impact ya Maana na Hawezi Kujua Siri Nyingi na Ripoti Nyingi Haruhusiwi Kuzisoma Kama Ilivyo Bungeni. Kwa Kifupi Kafungwa Mdomo kwa Kutumia Post ya Uwaziri..

Mwakyembe Pia Kateuliwa Wizarani ili Atoke Bungeni Kuondoa Maswali Bungeni. JK na Washahuri Wake Kingunge na Rostam Wamemueleza Akimwacha Mwakyembe Bungeni Kipindi Hiki Bungeni ni Hatari kwa CCM. Mwakyembe kwa Kifupi, Katiwa Kofuri Mdomoni kwa Kwenda Wizarani. Hawa Wabunge wa CCM Huko Bungeni ni Wamedharauliwa Kiasi Kwamba Wanaonekana Mbele ya JK ni Mifuko ya Karatasi Haina Kazi. JK Anategemea Kulala Kwao Bungeni Sio Kuwawakilisha Wananchi kwa Kuuliza Maswali. Yale Yale JK Achukue Pesa na Kwenda Retirement........Hamkeni CCM Mtalala Mpaka Lini? Kwani Hamna Ndugu Wanakufa na Shida Tanzania? Inchi Inawahitaji Sana Wakina Sitta na Mwakyembe Wengine.

Vita Jk Anavianzisha na Chadema. JK na Washahuri Wake CCM Watapata Kuishambulia Chadema Kama Wanavyotaka Kukiwa Hakuna Wauliza Maswali Kutoka CCM. Sisi Wananchi Tunatakiwa Tusupport Chadema na Uongozi Chadema Wahakikishe Wanakaa Pamoja na Kushirikiana. JK na CCM Wanataka Kuvuruga Chadema Kutumia Usalama wa Taifa na Pesa. CCM Walifanikiwa Kuua NCCR na Vyama Vingine Inchini kwa Vitendo Hivi. Wananchi Tusikubali Demokrasia Iharibiwa na Watu Wachache ili Waendelee Kuiba na Kuwaua Wananchi Mahospitalini Kila Leo. Kazi Moja ya Usalama wa Taifa TZ ni Kupeleleza Wananchi Wauliza Maswali Sio Kupeleleza Criminals. Hii Ndio Sera za CCM Kama People's Party in China. Kutumia Jeshi na Vyombo vya Ulinzi Kuwamaliza Wananchi Wako....Tutaona Itaishia Wapi Tena...
"Kwa Taarifa Yenu CCM... Chadema Haitakufa Kama NCCR na UDP Zilivyoundwa. Chadema ni Sawa na Wananchi Wote Tanzania"

Haya ni Mawazo mgando, bunge la watu mia tatu na ushee wawili wana impact gani, sitta na mwakyembe? Kilango hayupo? na wengine.
Alafu unasema Chadema haianguki, unataka ianguke mara ngapi????????????????
Omba uzima ndugu yangu utaona na weka kumbukumbu ya maneno haya, ila ikifika siku uwe muungwana kuthibitisha kilichotokea....
 
Hivi kukaa bungeni nakuwa muuliza maswali yana paswa kuwa au kupewa uwaziri utekeleze yanayo paswa kuwa kipi bora?
 
nIMEKUWA NIKIJIULIZA utamaduni wetu (TZ) namna ambavyo tunaangalia ubora wa viongozi ...watawala wetu ,ama kwa hakika unatia mashaka .N pengine hili ni tatizo kubwa ambao wengi tunaliona ni dogo au hatulioni.Mijadala iliendelea hapa hasa baada ya uteuzi wa Sita,Mgufuli na mWAKYEMBE INADHIHIRISHA utamaduni huu.
Ukiwaangalia kwa makini watu hawa ,matendo yaliyowapa sifa (Sita na Mwakyembe0 yanatia shaka.Samweli Sitta ndiye aliyebeza ushahidi wa wizi wa Epa !nakumbuka sana mchana ule TVT wakihojiwa na bwana Tido alionesha dharau kubwa kwa ushadi ule .Inawezekana alikuwa hajui,lakini kwa nn hakufanyia uchunguzi! Ni yeye aliyehitimisha kwa maajabu mjadala wa Richmond !hivi hapo ushapavu wake wa kupambana na ufisadi uko wapi?Kama ni muadilifu asingekubali serikali itoe majibu mepesi kuwa MEREMETA ni suala la usalama halijadiliki!
Bwana Mwakyembe alikuwa ni kinara wa vita ya ufisadi hivi mbona hatujiulizi hiyo vita walikuwa wanapigana na nanin!?hivi inatisha tu kusema tunapigana vita na watu tuamini ......kubwa zaidi wakasema wanamdaidia RAIS! NI vita gani hiyo mbona haikuwa na mshiko na ILIISHAJE!ndivyo vita vinavyopiganwa ,mbona waliishia kutembelea mikoani na kutangaza VIKOBA .!rICHMOND iliyosimamisha nchi miaka miwili iko wapi nan i kashindwa katika vita hivyo?!
Mbona hatujiulizi
Kwa mheshimiwa ...Pombe kama ni mwadilifu .....ile dhambi ya kuuza nyumba za umma iltosha kumtoa katika kundil la waadilifu....!labda kama angejiudhuru,kAMA NI KUJENGA BARA2 NALAILA KIULA alifanya nini
Kuna haja ya kuwajua viuongozi bora na uongozi nini ,la sivyo tutaendelea kushangilia mabomu na hatutafika!
MBONA HATUKUTAFAKARI MANENEO YA LOWASA KUWA SUALA LA RICHMOND ILIKUWA NI UWAZIRI MKUU..!JE HITMISHO LAKE HALDHIHIRISHI KAULI HIYO,.....mAONI YANGU
 
Tutachambuana mpaka tutakosa mwelekeo. Baraza la mawaziri limeshatangazwa hilo tuwaache wafanyekazi, wanapoboronga tupaze sauti zetu na wanapofanya vizuri basi tuwasifie. Hebu tuache malumbano tuchape kazi kwa maendeleo ya nchi yetu. Yatosha sasa.
 
Hao mawaziri na manaibu wameshaanza kazi sasa. Muhimu ni kuona utendaji wao ndipo tutajua mchele ni upi na pumba ni ipi.
Hao ambao aliyeanzisha thread amekerwa kuona wakitajwa vizuri (Mh Sitta, Dr Magufuli & Dr Mwakyembe) nao tutaona utendaji wao kama utakidhi matarajio ya watu.
Namuomba threat-starter asikereke kuona hao watatu wanasifiwa. Yaelekea wengi wana matumaini nao, na pia kila mtu ana uhuru wa kumsifia amtakaye.
Tusubiri utendaji, ndipo tutasema zaidi.
 
Sijakereka na kupendwa kwao ,nauliza sababu ya kupendwa kwa uongozi wao kwa kuzingatia matendo yaliyopita wala si yajayo,na uwezo wetu wa kujua kiongozi mzuri na uongozi mzuri
 
we maada gani nayo hiyo.ulitaka wakuchague wewe au unaonagele?

"In looking for people to hire, you look for three qualities: integrity, intelligence, and energy. And if they don't have the first, the other two will kill you."
� Warren Buffet​
Do Mr. Sitta, Dr. Magufuli and Dr Mwakyembe have integrity? You be the judge!
 
Apo kwa Mwakyembe umetoa maelezo shallow sana kiasi kwamba hata hukuwa na haja ya kumuiclude kwa thread yako.
Mmwakyembe uadilifu wake unaanzia tangua alipojiuzulu kule NBC wakati wanaiuza mpaka kujiuzulu kwa Lowasa.
Magufuli aliuza nyumba kwa mwongozo wa mkuu wake wa kazi sasa kama Ben alikuwa hapendezwi na ilo basi angelikataa but it was an issue from the top and not Magufuri as he is.
Sitta wakati anapapmbana na mafisadi hakupata support ya chama na ndo maana aliishia kwa richmond
 
Jamani MUNGU hufanyakazi zake kwa kutumia wanadamu katika muda maalumu na kwa kazi maalumu isipokuwa katika mambo yaliyo katika ulimwengu wa roho ambako Roho Mtakatifu na malaika hutumika. Akina Mwakyembe na Sitta wameshatumika na kazi yao juu ya Richmond wameishia hapo walipoishia na sasa wamepewa majukumu mengine ya ujenzi wa taifa letu tuwaache watufanyie kazi tusiendelee kutunga hoja juu ya uteuzi wao. Maana najua kama watu hawa wangeachwa nje watu wangelalamika kwanini hawakupewa uwaziri. Si rahisi kumridhisha kila mtu.
 
Kulikua na mtu anaitwa Njelu Kasaka, Philipo Marmo na wenzake... walikuwa wakali bungeni kuliko pilipili, wakaanzisha hoja ya Tanganyika wakijiita G55. Nyerere akatoka Butiama na fimbo yake sijui walicharazwa, ila najua Mwinyi aliwapa uwaziri baadhi yao, wakatulia kuliko mtungi. Madaraka matamu.
 
Kulikua na mtu anaitwa Njelu Kasaka, Philipo Marmo na wenzake... walikuwa wakali bungeni kuliko pilipili, wakaanzisha hoja ya Tanganyika wakijiita G55. Nyerere akatoka Butiama na fimbo yake sijui walicharazwa, ila najua Mwinyi aliwapa uwaziri baadhi yao, wakatulia kuliko mtungi. Madaraka matamu.

Hata Mwakyembe na Sitta wako kwenye mlolongo huo huo - katu hutawasikia wakipambana na ufisadi kama walivyokuwa wanadai. Imetoka hiyo!
 
Back
Top Bottom