Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 18,300
- 33,913
Taifa lenye watu wengi wasio na uadilifu ni kawaida sana kuwepo kwa wizi wa mitihani ama udanganyifu kwenye mitihani. Uadilifu ni zaidi ya mtu kutokuiba ama kusema uongo, uadilifu pia ni pamoja na mtu kujali maslahi ya wengi pale anapokuwa na cheo kwa niaba ya Umma.
watu waadilifu wataweka mifumo rahisi na yenye ubora kwa ajili ya watu kufanya mitihani na kusahihishiwa mitihani yao. watu waadilifu ni wale wanaojua kwamba mitihani inatakiwa iwe kipimo cha uelewa na siyo kipimo cha uwezo wa kukariri.
Ili mitihani iwe kipimo cha uelewa ni lazima watu waadilifu waweke mifumo inayofanya watoa elimu (Waalimu/wahadhiri) watimize wajibu wao wa kufundisha na kuhakikisha asilimia kubwa ya wanaofundishwa wanaelewa. Watu waaadilifu hawajivunii asilimia kubwa ya watu kufeli mitihani yao kuliko kufaulu.
Leo ni kawaida kabisa baadhi ya watahiniwa kuhonga, kuingia na majibu kwenye vyumba vya mitihani, kununua mitihani, kughushi vyeti, kutumia majina yasiyo yao na kadhalika na kadhalika. Wanaposhikwa ndipo jamii hushikwa na butwaa kama vile haijui kuna watu kama hao kwenye jamii yetu.
watu waadilifu wataweka mifumo rahisi na yenye ubora kwa ajili ya watu kufanya mitihani na kusahihishiwa mitihani yao. watu waadilifu ni wale wanaojua kwamba mitihani inatakiwa iwe kipimo cha uelewa na siyo kipimo cha uwezo wa kukariri.
Ili mitihani iwe kipimo cha uelewa ni lazima watu waadilifu waweke mifumo inayofanya watoa elimu (Waalimu/wahadhiri) watimize wajibu wao wa kufundisha na kuhakikisha asilimia kubwa ya wanaofundishwa wanaelewa. Watu waaadilifu hawajivunii asilimia kubwa ya watu kufeli mitihani yao kuliko kufaulu.
Leo ni kawaida kabisa baadhi ya watahiniwa kuhonga, kuingia na majibu kwenye vyumba vya mitihani, kununua mitihani, kughushi vyeti, kutumia majina yasiyo yao na kadhalika na kadhalika. Wanaposhikwa ndipo jamii hushikwa na butwaa kama vile haijui kuna watu kama hao kwenye jamii yetu.