Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,391
- 39,484
Na. M. M. Mwanakijiji
Laputopu nimeshika, na dodosa wa porini,
Sina budi kuandika, niliseme la rohoni,
Mwenzenu nafadhaika, namngoja wa ubani,
U wapi ewe tabibu, fanya hima kunitibu!
Najilaza kitandani, homa imenizidia,
Na maumivu mwilini, nyongani yameshikia,
Na sasa ni mashakani, ugonjwa umevamia,
U wapi ewe tabibu, fanya hima kunitibu!
Yalianza kunisibu, kwanza nilipokuona,
Ukawa mwanzo wa tabu, na sasa nataka pona,
Namtaka mahabubu, mganga wa kiaina,
U wapi ewe tabibu, fanya hima kunitibu!
Ukaniteka mateka, ulo teka moyo wangu,
Ukanitoa mashaka, kuuliza jina langu,
Mtima ukashituka, nikaapa uwe wangu,
U wapi ewe tabibu, fanya hima kunitibu!
Namkiri Subihana, yeye kakupendelea,
Umbile lako mwanana, kama chezo waelea,
Wenzako wakikuona, gele wanakuonea,
U wapi ewe tabibu, fanya hima kunitibu!
Ewe tabibu wa ndani, mganga uloumbika,
Wewe binti wa nyumbani, ni lini utajafika,
Wa tabasamu la shani, na umbo la malaika,
U wapi ewe tabibu, fanya hima kunitibu.
Ahadi tukapeana, tarehe tuje kutana,
Tuzidi fahamiana, na kuzidi kujuana,
Na hata tulipoachana, na busu tukapeana,
U wapi ewe tabibu, fanya hima kunitibu!
Siku sasa zinapita, nakusibiri ufike,
Na homa nimeshapata, natetema niko pweke,
Nakaa najikunyata, nangoja giza litoke,
U wapi ewe tabibu, fanya hima kunitibu!
Michuzi nimetamka, kalamu naweka chini,
Imenipanda mizuka, namuwaza wa ubani,
Betti nimeziandika, usizabane mtani,
U wapi ewe tabibu, fanya hima kunitibu!
M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Shamba)
Mwanakijiji@klhnews.com
Laputopu nimeshika, na dodosa wa porini,
Sina budi kuandika, niliseme la rohoni,
Mwenzenu nafadhaika, namngoja wa ubani,
U wapi ewe tabibu, fanya hima kunitibu!
Najilaza kitandani, homa imenizidia,
Na maumivu mwilini, nyongani yameshikia,
Na sasa ni mashakani, ugonjwa umevamia,
U wapi ewe tabibu, fanya hima kunitibu!
Yalianza kunisibu, kwanza nilipokuona,
Ukawa mwanzo wa tabu, na sasa nataka pona,
Namtaka mahabubu, mganga wa kiaina,
U wapi ewe tabibu, fanya hima kunitibu!
Ukaniteka mateka, ulo teka moyo wangu,
Ukanitoa mashaka, kuuliza jina langu,
Mtima ukashituka, nikaapa uwe wangu,
U wapi ewe tabibu, fanya hima kunitibu!
Namkiri Subihana, yeye kakupendelea,
Umbile lako mwanana, kama chezo waelea,
Wenzako wakikuona, gele wanakuonea,
U wapi ewe tabibu, fanya hima kunitibu!
Ewe tabibu wa ndani, mganga uloumbika,
Wewe binti wa nyumbani, ni lini utajafika,
Wa tabasamu la shani, na umbo la malaika,
U wapi ewe tabibu, fanya hima kunitibu.
Ahadi tukapeana, tarehe tuje kutana,
Tuzidi fahamiana, na kuzidi kujuana,
Na hata tulipoachana, na busu tukapeana,
U wapi ewe tabibu, fanya hima kunitibu!
Siku sasa zinapita, nakusibiri ufike,
Na homa nimeshapata, natetema niko pweke,
Nakaa najikunyata, nangoja giza litoke,
U wapi ewe tabibu, fanya hima kunitibu!
Michuzi nimetamka, kalamu naweka chini,
Imenipanda mizuka, namuwaza wa ubani,
Betti nimeziandika, usizabane mtani,
U wapi ewe tabibu, fanya hima kunitibu!
M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Shamba)
Mwanakijiji@klhnews.com