U.A.E kukataza Raia wake kuonyesha sympathy kwa Qatar inafundisha nini watanzania?

Mgambilwa ni mntu

JF-Expert Member
May 30, 2017
2,869
3,188
Serikali ya Emirates - UAE imeonya kuwachukulia hatua kali raia wake watakaoonyesha huruma ama kutetea Nchi ya Qatar kufuatia hatua zilizochukuliwa na nchi washirika wa kiarabu zikiongozwa na Saudi Arabia kuiwekea vikwazo Qatar kwa tuhuma za kufadhiri vikundi vinavyojihusisha na ugaidi. Nchi hiyo imeweka adhabu ya Dola 136,000 na adhabu ya miaka 15 gerezani.

Mimi ni mmoja wa wanaopenda demokrasia kuwa mikononi mwa watu kwa kuwa ni muumini wa Utilitarianism na wala siungi mkono uamuzi huo wa UAE. Hata hivyo najaribu kulinganisha na mazingira ya Nchi yetu kuwa suala hilo lingechukuliwaje? Ndio tujifunze umuhimu wa kuwa na umoja kwenye masuala ya kitaifa hata kama muda mwingine watawala wetu wanakosea kwani nao ni binadamu. Masuala ya rasilimali za Nchi ni lazima yatuunganishe kwa namna yoyote hasa madini yetu. Hivi tukishindwa vita simple kama hiyo itakuwaje kwa lie ya Ziwa Nyasa dhidi ya Malawi hao watu watatuunga mkono? Nawasilisha
 
Hivi mfano mko vitani au jirani yenu anafadhili adui yenu afu kuna wapuuzi ndani ya nchi yenu wanawaonea huruma adui zenu wewe kama kiongozi wa nchi utafanyaje?
 
Dunia hii ni ya kidemokrasia sio vema kumlazimisha mtu kuunga mkono kila kitu serikali inafanya maana wakati mwingine serikali zinakosea na kuleta shida kwa watu wa kawaida wanapovunja mahusiano
 
Saudi Arabia ina roho ngumu sana aiseeh, ngoja siku aguse maslahi ya Urusi tuone atakavyo hangaika
 
Hivi mfano mko vitani au jirani yenu anafadhili adui yenu afu kuna wapuuzi ndani ya nchi yenu wanawaonea huruma adui zenu wewe kama kiongozi wa nchi utafanyaje?
Unasema kweli lakini mbona hasa kwetu tunasumbuka kudai madini yetu lakini wapuuzi Fulani wanatukebei asubuhi asubuhi kuwa tutashitakiwa? Hao watu utawategemea?
 
Qatar hadi sasa hizo nchi wanazodai inasaidia magaidi hawajaonyesha ushahidi wowote hii ni vita juu ya rasilimali maana Qatar imepiga hatua kubwa eneo la ghuba kwa biashara na uchumi wake unaimarika ingawa ni nchi ndogo ukilinganisha na saudia Arabia hivo ni wivu tu wa maendeleo waarabu wanatafuta sababu
Ninakubali wazi kuwa pamoja na kuwa na watu acha he tu wapatao millions 3 ni kweli wake juu kiuchumi kutokana na kuwa na reserve kuwa kabisa ya gesi duniani, nyuma ya Ruassia na Iran. Ndio maana nikasema italeta tu hasira kwa waislamu watakapogundua kuwa Saudia na washirika inataka Qatar asivisaidie vikundi kama Hamas ambavyo kwa waislamu wanakiona ndicho kinachopigania maslahi ya wapalestina.
 
Ninakubali wazi kuwa pamoja na kuwa na watu acha he tu wapatao millions 3 ni kweli wake juu kiuchumi kutokana na kuwa na reserve kuwa kabisa ya gesi duniani, nyuma ya Ruassia na Iran. Ndio maana nikasema italeta tu hasira kwa waislamu watakapogundua kuwa Saudia na washirika inataka Qatar asivisaidie vikundi kama Hamas ambavyo kwa waislamu wanakiona ndicho kinachopigania maslahi ya wapalestina.
Waislamu gani unawazungumzia?
 
Hii sijui tuiteje? Ni mhemuko wa waarabu? Au ni kitu gani? Maana ni as if walikuwa kwenye kikao na kutoka na maamuzi ya pamoja juu ya walichokifanya. Ghafla kaanza Saudia, kafuata Misri, UAE, Libya, Yemen, Jordan; duh. Mataifa ya kiislam/kisunni nje ya uarabuni ikiwemo Turkey, Pakistan, Indonesia yamejizuia. Mhemuko huu wa waarabu bila kufikiria ni hatari.
 
Qatar hadi sasa hizo nchi wanazodai inasaidia magaidi hawajaonyesha ushahidi wowote hii ni vita juu ya rasilimali maana Qatar imepiga hatua kubwa eneo la ghuba kwa biashara na uchumi wake unaimarika ingawa ni nchi ndogo ukilinganisha na saudia Arabia hivo ni wivu tu wa maendeleo waarabu wanatafuta sababu
Nadhani labda hufuatilii siasa za M.E, Qatar anawahifadhi viongozi wote wa Muslim brotherhood na Hamas wanaishi Qatar, hawa ndio tatizo na lazima urejee Qatar ni nchi ndogo sana na usitake kuwafananisha na Saudia au UAE kiutajiri. wao ni matajiri kutokana na uchache wao lakini kimapato ya kijumla hawafikii KSA au UAE. wewe chukulia hapa Tz watu ambao wanapinga serikali au kutaka kupindua fanya Rwanda au Burundi kawachukuwa na kuwapa hifadhi, Tanzania watakaa kimya? Rwanda tu na udogo aliamuwa kuwafuata wabaya wake mpaka Congo.
 
Upo sahihi kabisa kwanini tusingeanza kwa kuwanyonga ma Lord lofa walioingia hiyo mikaraba ya kipuuzi???
Au mnachezea wana nchi mapicha picha waone mkuu anapiga kazi!!!
Hivi wewe kwa akili yako ni rahisi kiasi hicho kukamatwa viongozi waliotuingiza mkenge kwenye mikataba lie bila nchi kutikisika. Kama vi-issue vidogo tu vya mabadiliko ndani ya CCM vimewagawanya sana wana-CCM he la kuwakamata wakulu?
Tukubali tu kuanza upya na turekebishe tulipojikwaa maana kila MTV alijua kuwa tulikuwa tu Aliya kwenye madini japokuwa hatukujua kwa kiasi gani. Ukifuatilia sana mambo anayofanywa na Magufuli utaamini tumepata sana Bahati ya kumpata huyu jamaa. Nchi majirani wamekuwa wakitucheka sana kuwa sisi watanzania tumelala kutokana na jinsi tulivyokuwa tukiendesha nchi yetu lakini pole pole wana za kutuchukia kimoyomoyo kwa kuwa WASIYEMTAKA NDIYE KAJA.
 
Waislamu Wengi duniani wanakipenda Hamas dhidi ya Fatah cha Abuu Mazen "Abbas" kutokana na approach yake ya ubabe dhidi ya Israeli kuliko Abuu Mazen ambaye Yuko reconciatory kwa Israeli. Nadhani umeelewa.
Ninavyofahamu ni kwamba, makhawaariji ambao ni wachache ndio wanaowaunga mkono hamas. Wakidanganywa na wairan.
Wanalikuza tatizo la Palestina kwakuwa wanafaidika na mgogoro huo.wamepuuza ushauri wa wanachuoni wa kiislamu ili kutatua mzozo na Israel. Leo wanawaona wasuudi ni maadui
 
Hivi wewe kwa akili yako ni rahisi kiasi hicho kukamatwa viongozi waliotuingiza mkenge kwenye mikataba lie bila nchi kutikisika. Kama vi-issue vidogo tu vya mabadiliko ndani ya CCM vimewagawanya sana wana-CCM he la kuwakamata wakulu?
Tukubali tu kuanza upya na turekebishe tulipojikwaa maana kila MTV alijua kuwa tulikuwa tu Aliya kwenye madini japokuwa hatukujua kwa kiasi gani. Ukifuatilia sana mambo anayofanywa na Magufuli utaamini tumepata sana Bahati ya kumpata huyu jamaa. Nchi majirani wamekuwa wakitucheka sana kuwa sisi watanzania tumelala kutokana na jinsi tulivyokuwa tukiendesha nchi yetu lakini pole pole wana za kutuchukia kimoyomoyo kwa kuwa WASIYEMTAKA NDIYE KAJA.
Kijana bado sana mkuu hii picha bado uniangalia kwenye tv zenye antenna ya analogy kwaiyo unaona chenga nyingi kuliko picha !!!!
Unaidanganya nafsi yako bure hakuna litakalo tendela bila kuwa kamata waliyo ingiza nchi kwenye mikataba tata !!!
Kama kweli tumempata akamate mali zote zilizopatikana kwa malipo haramu tutampa hii nchi milele vinginevyo ni kelele za chura hazizuwie ngombe kuendelea kunywa maji!!!
 
Hivi mfano mko vitani au jirani yenu anafadhili adui yenu afu kuna wapuuzi ndani ya nchi yenu wanawaonea huruma adui zenu wewe kama kiongozi wa nchi utafanyaje?
Hapo inaonyesha mwenye uadui na Qatar sio wananchi wa UAE ni viongozi , viongozi wanataka kulazimisha wananchi waichukie Qatar kwa faida yao
 
Back
Top Bottom