Tyson "Wassira" kuwa Waziri Mkuu?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,463
39,929
Katika kuokoa jahazi na kujaribu kuweka mwelekeo... ili tuweze kufocus..

Hapana; Resume ya Tyson ni ndefu zaidi ya hapo ingawa ni ile ya old guard. Ameshashika madaraka mbalimbali serikalini kuliko watu wengi sana walioko serikalini.

Elimu: Darasa la nane Nyambitilwa Middle School kati ya mwaka 1964 na 1967 hivi sina uhakika.


Kazi na Uzoefu:
  1. Kutoka Shule - 1969 : Bwana Maendeleo wa tarafa moja huko Ukerewe
  2. 1969 - 1972: Katibu mtendaji wa TANU wilaya ya Musoma
  3. 1970-1975: Mbunge wa Mwibara.
    Ushindi wake katika kinyang'anyiro cha ubunge ule ulikuwa wa bahati sana na nadhani kuwa hapo ndipo nyota ya Tyson ilipoanza kung'aa. Alishindana na mtu mmoja aliyekuwa anajulikana kama Muyenjwa ambaye aliwahi kuwa Mkuu wa Tarafa nadhani ya Kenkombyo ambako alikuwa amenyanyasa watu sana. Kwa hiyo watu wa maeneo yale hawakutaka kumpigia Muyenjwa kura, na hivyo kumpa Tyson ambaye walikuwa hawamjui.​
  4. 1972-1974: Waziri mdogo wa Kilimo.
  5. 1974-1983: Mkuu wa Mkoa wa Mara
    Hapa Tyson alipata nafasi ya kumwoa mtoto wa Chifu Wanzagi na hivyo akwa ni mkwe wa Nyerere. Aliondolewa pale kutokana na skendo kadhaa zikiwamo za kutumia madaraka yake kuvuruga uchaguzi wa ubunge wa jimbo la Musoma mwaka 1980, na matumizi mabaya ya nafasi yake kujipatia huduma kutoka kiwanda cha MUTEX.​
  6. 1983-1984: Kazi Maalum Wizara ya Mambo ya Nje.
  7. 1984-1985: Ofisa wa Ubalozi wa Tanzania huko Marekani, Washington DC.

    Inasemekena katika kipindi hiki alijiendeleza kielimu na kujipatia digrii kadhaa za uzamili za utawala, uchumi na ushirikiano wa kimataifa: Master of Public Administration, Master of International Relations, na Master of Economic Planning.​
  8. 1985-1990: Mbunge wa Bunda.
    Ubunge ule nao aliupata kinamna kwa vile kulikuwa na mvutano kati ya Mwenyekiti wa CCM wa Bunda (nadhani akiitwa Mnubi Salama) na Mbunge wa Bunda wakati huo Mugeta. Mwenyekiti akaendesha kampeini mapema kabisa kuwa watu wasimpigie kura Mugeta kwa sababu alishindwa kuleta maendeleo kwanye jimbo la Bunda. Watu wakawa wamekubaliana na mwenyekiti kuwa Mbunge yule ang'olewe. Lakini walikuwa hawajui kuwa nani atapambana naye. Ilipofika mwezi July 1985, Wassira akatangaza kugombea Bunda, ndipo Mwenyekiti aliposhtuka na kujaribu ku-reverse kampeini zake against Mugeta lakini ilikuwa too late.​
  9. 1985-1990: Waziri mdogo wa Tawala za Mikoa, na Serikali za Mitaa; Waziri wa Kilimo, Ushirika, Masoko.
    Hapa sina uhakika na majina ya wizara alizoongoza ila najua mojawapo ilihusika pia na ushirika, ambapo alitumia madaraka yale kumfukuza kazi Meneja wa Bodi ya Pamba na kumteua kaka yake George Wassira kuikaimu indefinitely. Kipindi hicho aliachana na binti wa Wanzagi na kumwoa dada yake na Waryoba ambaye alikuwa waziri mkuu.​
  10. 1990-1994: Mkuu wa Mkoa wa Pwani:
    Kipindi hicho hakuombea ubunge wa Bunda ili kumpisha Waryoba. Badala yake akateuliwa kuwa mkuu wa mkoa nadhani wa Pwani. Inawezekana alihamishiwa mikoa kadhaa ila kipindi cha pili cha utawala wa Mwinyi, Bwana Tyson hakuwa waziri. Ninadhani kuwa katika mabadiliko ya serikali ya mwaka 1994 ambapo Msuya alipoteuliwa kuwa Waziri Mkuu badala ya Malecela, huyu tyson alipotenza nafasi yake ya ukuu wa mkoa; hata hivyo sina uhakika sawasawa.​
  11. 1995-1997: Mbunge wa Bunda.
    Kwenye uchaguzi huo alienguliwa kwenye primaries za CCM ambapo walimpitisha Waryoba aliyekuwa incumbent ; Tyson akaamua kujiunga na NCCR-Mageuzi ambapo alitwaa kiti kile. Hata hivyo kwa vile alikuwa amecheza faulo nyingi sana kwenye kampeini za uchaguzi ule kama ilivyo kawaida yake, Mahakama Kuu ilitengua ushindi huo na kumzuia kugombea kwa miaka mitano. Kwa hiyo mwaka 2000 hakugombea hadi mwaka 2005 alipogombea tena.​
  12. 2005-Todate: Mbunge wa Bunda na Waziri kwenye awamu ya nne. Ameshaongoza Wizara mbili.
 
Si mchezo amekula kuku since the 1970's mpaka leo. Sito shangaa nikiambiwa hana Investment yoyote ya maana na huko kwenye jimbo lake hakuna maendeleo yoyote ya yeye kujisifia nayo...kweli ukishajua siasa za CCM zinachezwa vipi...ni uongozi mpaka kufa (Wakenya hutumia sana ule msemo (political survivors) yani piga ua hawachomoki, hawa ndo wazee ukikaanae utake kuandika biography yake unaweza kuchanganyikiwa ili ku establish were exactly their political policies stand...kaaazzzz kweli kweli...
 
Naona mna-prempt jamaa halafu atazira na ndio mtakuwa mmemharibia kabisa mwenzenu. Mnakumbuka ya Mzee JSM?
 
..hivi,kuna vigezo vimetolewa kumuweka tyson katika nafasi hiyo ya ushindi [hizo polls zisizo rasmi!]
 
DAR si LAMU, Resume ya Steven Wasira ambayo iko Wikipedia inaonyesha mtiririko ufuatayo: Kuna utofauti wa Miaka na Tarehe zilizowekwa na Kichuguu...


# Member of Parliament - Mwibara Constituency 1970 - 1975

# Deputy Minister of Agriculture 1972 - 1975

# Regional Commissioner Mara Region 1975 - 1982

# Minister Counselor at the Embassy of Tanzania, Washington, DC, USA - 1982 - 1985

# Member of Parliament - Bunda Constituency 1985 -1990

# Deputy Minister for Local Government 1987-1989

# Minister of Agriculture and Livestock Development 1989- 1990

# Regional Commissioner Coastal Region 1990 - 1991

# Member of Parliament - Bunda Constituency 1995 -1996

# Member of Parliament - Bunda Constituency 2005 -Present

# Minister for Water - Jan 2006 - Oct 2006

# Minister of Agriculture and Food Security - 2007 - Present


Education ya Wassira inaonyesha,mwanasiasa huyo ana shahada kama nne alizopata nchini Marekani

BA in Economics, American University in Washington, DC, USA.

BA in Political Science, American University in Washington, DC, USA.

MA in Economics, American University in Washington, DC, USA.

Masters in Public Administration, American University in Washington, DC, USA.


Wassira ana resume ndefu iliyomweka Bungeni akiwa na miaka 25,na kuwa Deputy Minister Agriculture akiwa na umri mdogo wa miaka 27 ..Wassira is a seasoned politician kwa muda alioanza katika public service, kiumri anapishana miaka mitano tu na JK,kawahi kuanza uongozi...JK kazaliwa 1950, Wasira 1945 .

Ripoti ya REDET iliyoangalia performance ya Wizara za Serikali ya JK, Waziri Wassira amekuwa rated juu akitokea Maji, Kuwa promoted Wizara hiyo kubwa na Nyeti (Kilimo), amerekebisha Biashara ya korosho kati ya Wananchi na wanunuzi, kafukuza kazi watendaji warasimu na wahujumu, na kufuta vibali vya makampuni yaliyogoma kununua bei ya kufaidisha maslahi ya wananchi. Kilimo kazi sio rahisi,Wizara inayolenga 80% ya wananchi,wengi maskini, lakini walio ndani ya wizara hiyo na bodi zake za mazao wamenukuliwa wakisifu bidii iliyojitokeza baada ya Tyson kuhamia pale.

Uchaguzi wa 2005, Tyson katika Jimbo la Bunda alipita bila kupingwa (walikuwa kama watano hivi nchi nzima).Ukweli Tyson Bunda na Mara anapendwa na watu,umaarufu wake unaweza kulinganishwa na Mwandosya kule Mbeya.

Na uhasisi wa jina lake "Tyson", ambalo JK pekee ndio mwenye ruhusa ya kulitumia jina hilo, according to Tyson au Wassira mwenyewe,ulitokana na uwezo wake kujenga hoja na sifa yake kisiasa katika uchaguzi wa jimbo la Bunda 1995 ambapo alimwangusha na kumstaafisha siasa Waziri Mkuu wa zamani Jaji Joseph Sinde Warioba anayetokea vijiji vya ikizu jimbo hilo hilo la Bunda kupitia ticket ya NCCR-Mageuzi.Mizengwe ya CCM Bunda ilimhamisha Tyson kwenda NCCR-Mageuzi, kufutwa matokeo ya Bunda kwa Wasira ilikuwa personal dhihaka ya Tume ya Rushwa iliyoongzwa na Warioba mwenyewe baada ya kushindwa uchaguzi huo na Wassira .Hivi sasa ndani ya CCM, Tyson, ni mjumbe wa NEC kupitia lile kundi la kifo (Super 20).

Katika enzi za challenge za ethics,rushwa, mafisadi wa BOT,Buzwagi,etc, si shangai kwa nini jina la Tyson likitajwa kuwa nafasi hiyo...Ni that No non-sense,experienced guy asiyeogopa mtu, wala mapambano na mtu..
 
Ni kweli inawezekana nimekosea kidogo katika baadhi ya miaka lakini mtiririko wangu bado uko sahihi. Ameshika madaraka mengi sana nchini hapa, na alipata digrii nne katika kipindi kisichozidi miaka miwili alichokuwa afisa wa ubalozi pale Washington DC akiwa na entry qualifications za darasa la nane. Baada ya kutoka Ukuu wa Mkoa wa Mara alikaa benchi kidogo pale foreign Affairs kabla hajapelekwa DC; ninadhani kuwa post hiyo ya DC ilitokana na ukweli alikuwa mkwe wa Nyerere kwa vile hakuwa na qualifications zozote za diplomatic corps.

Sina uhakika kama kweli anaweza kuwa Waziri Mkuu wa kusaidia nchi hii iliyogubikwa na matatizo ya sasa hivi hasa kwa vile ni mtu mwenye visasi sana. Badala ya kuendeleza demokrasia, nadhani huyu ndiye atakayeibomoa kabisa. Mojawapoa ya unyonge wake ni kuwa ukipingana naye kwa ishu yoyote, anakuchukulia adui na anatafuta namna ya kukumaliza kabisa. Alimaliza watu wote waliokuwa wapinzani wake kwenye chaguzi za ubunge; hasa Muyenjwa na Mugeta. Nina uhakika uhasama wake na Waryoba kufuatia uchaguzi wa 1995 haujafutika na akipata madaraka ya Uwaziri Mkuu anaweza kutafuta sababu za kumweka ndani Waryoba. Akina Dr. Slaa na Zitto wanaoipiga serikali madongo watajikua wote wapo lupango.


Hayo ni maoni yangu ambayo yanaweza kuwa siyo sahihi; tusubiri tuone.
 
Swala la Uwaziri Mkuu ni swala ambalo Rais JK pekee ndio anajua na ataamua kama atafanya hayo mabadiliko ya kiwango hicho, Waziri Mkuu yupo na yupo kwa sababu zake JK mwenyewe..

Maoni ni Maoni na Facts ni Facts.

Siasa za Mara, hata Tarime ambayo Chacha Wangwe alishinda ni CHADEMA..Mara ni Aggressive Politics by nature ya wa-mara (hata wanapigana mawe saa zingine,Chambiri huko Tarime), CCM ilianguka Tarime 2005..Bunda CCM Tyson aliwashinda akiwa Upinzani NCCR against Jaji Sinde Waryoba, Jimbo la Mwibara Upinzani ulikuwa na hilo Jimbo kupitia TLP mpaka 2005,na sasa halina mbunge-mahakama imetengua ubunge, Musoma Vijijini NCCR (Balozi Ndobo) alikuwa Mbunge 1995..Rorya Mabere Marando akiwa NCCR-Maguezi aliwahi kuwa Mbunge, hata Musoma Mjini 2005, Dr Wandwi angemshinda Veda Mathayo isingikuwa Tyson kupiga sana Kampeni,nao walienda mahakamani ...Majimbo yote ya Mara yako hivyo siku zote,sasa Visasi ni tabia ya mtu, sio kitu unaweza kupima kwa kuangalia resume/CV au kusema hawezi kufuata Ilani ya Uchaguzi ya CCM--akiwa Waziri Mkuu ndio ataanza visasi? huwezi tabiri hayo yote ..Tyson aliwaangusha wote hao katika uchaguzi sasa kama Bwire-Mugeta (alikuwa Mwalimu) na Warioba (aliwahi kuwa Waziri Mkuu, ni ushindani hata kupata M/kiti wa Wilaya ni Burudani tupu..

Ukwe wa Nyerere, hiyo sijui,ila hiyo haiwezi nayo kuwa sehemu ya CV ya mtu, thats personal life not professional experience ya mtu-I cannot comment on someone life.

Kama sijakosea Elimu na Degree za Tyson Wassira zimepatikana katika kipindi cha 1982-1995, miaka takriban 13 kupata degree Bachelor & Masters katika Gaps, degree za mwanzo kati ya 1982 na 1986,

# Minister Counselor at the Embassy of Tanzania, Washington, DC, USA - 1982 - 1985

# Member of Parliament - Bunda Constituency 1985 -1990

# Deputy Minister for Local Government 1987-1989

# Minister of Agriculture and Livestock Development 1989- 1990

# Regional Commissioner Coastal Region 1990 - 1991

Alitangazwa kwenda masomoni awamu ya pili ya Rais A.H Mwinyi na hapo Prof . Philemon Sarungi akawa Mkuu wa Mkoa wa Pwani (1992), Wassira alienda kujiendeleza masomoni baada ya 1991. Huwezi kupata degree kwa Miaka Miwili ukiwa ubalozini, hata Strayer University au University of Phoenix On-line hawatoi haraka hivyo...Ila kwa System navyoielewa ya Elimu Marekani watu wanaweza kupata GED tu na kuingia moja kwa moja Chuo kikuu, sembuse darasa la 8 kama unafanya Pre-college examination, unapata Admission.Watu hupata credit hours za experience, let alone college admission..Alafu American University ni chuo kikubwa kinajulikana kiko Washington DC, lazima alifuata taratibu zote.

Hamna anayejua kweli kama hili "Tyson "Wassira" kuwa Waziri Mkuu?" linaweza kutokea au laa (JK Mwenyewe anajua) ..Ila Najua Waziri Mkuu ni mtu (mwenye mandate) ambaye anaweza kufuata Ilani za Maendeleo, kama ilani ya CCM ya Uchaguzi ipasavyo na ni mtu ambaye yuko tayari kuchafuka, kuingia sokoni Kariakoo Asubuhi mapema ikibidi,kutoa maamuzi magumu, kutembea kwenye Matope ikibidi, ufupi kuwa Msaidizi wa Rais ambaye anaweza kuongoza bila kulinda watu au Kuogopa mtu.

Kama ni uongozi, sijui kama vigezo hivyo havipo au kiuwezo katika resume tuliona hapo.
 
DAR si LAMU, Resume ya Steven Wasira ambayo iko Wikipedia inaonyesha mtiririko ufuatayo: Kuna utofauti wa Miaka na Tarehe zilizowekwa na Kichuguu...


# Member of Parliament - Mwibara Constituency 1970 - 1975

# Deputy Minister of Agriculture 1972 - 1975

# Regional Commissioner Mara Region 1975 - 1982

# Minister Counselor at the Embassy of Tanzania, Washington, DC, USA - 1982 - 1985

# Member of Parliament - Bunda Constituency 1985 -1990

# Deputy Minister for Local Government 1987-1989

# Minister of Agriculture and Livestock Development 1989- 1990

# Regional Commissioner Coastal Region 1990 - 1991

# Member of Parliament - Bunda Constituency 1995 -1996

# Member of Parliament - Bunda Constituency 2005 -Present

# Minister for Water - Jan 2006 - Oct 2006

# Minister of Agriculture and Food Security - 2007 - Present


Education ya Wassira inaonyesha,mwanasiasa huyo ana shahada kama nne alizopata nchini Marekani

BA in Economics, American University in Washington, DC, USA.

BA in Political Science, American University in Washington, DC, USA.

MA in Economics, American University in Washington, DC, USA.

Masters in Public Administration, American University in Washington, DC, USA.


Wassira ana resume ndefu iliyomweka Bungeni akiwa na miaka 25,na kuwa Deputy Minister Agriculture akiwa na umri mdogo wa miaka 27 ..Wassira is a seasoned politician kwa muda alioanza katika public service, kiumri anapishana miaka mitano tu na JK,kawahi kuanza uongozi...JK kazaliwa 1950, Wasira 1945 .

Ripoti ya REDET iliyoangalia performance ya Wizara za Serikali ya JK, Waziri Wassira amekuwa rated juu akitokea Maji, Kuwa promoted Wizara hiyo kubwa na Nyeti (Kilimo), amerekebisha Biashara ya korosho kati ya Wananchi na wanunuzi, kafukuza kazi watendaji warasimu na wahujumu, na kufuta vibali vya makampuni yaliyogoma kununua bei ya kufaidisha maslahi ya wananchi. Kilimo kazi sio rahisi,Wizara inayolenga 80% ya wananchi,wengi maskini, lakini walio ndani ya wizara hiyo na bodi zake za mazao wamenukuliwa wakisifu bidii iliyojitokeza baada ya Tyson kuhamia pale.

Uchaguzi wa 2005, Tyson katika Jimbo la Bunda alipita bila kupingwa (walikuwa kama watano hivi nchi nzima).Ukweli Tyson Bunda na Mara anapendwa na watu,umaarufu wake unaweza kulinganishwa na Mwandosya kule Mbeya.

Na uhasisi wa jina lake "Tyson", ambalo JK pekee ndio mwenye ruhusa ya kulitumia jina hilo, according to Tyson au Wassira mwenyewe,ulitokana na uwezo wake kujenga hoja na sifa yake kisiasa katika uchaguzi wa jimbo la Bunda 1995 ambapo alimwangusha na kumstaafisha siasa Waziri Mkuu wa zamani Jaji Joseph Sinde Warioba anayetokea vijiji vya ikizu jimbo hilo hilo la Bunda kupitia ticket ya NCCR-Mageuzi.Mizengwe ya CCM Bunda ilimhamisha Tyson kwenda NCCR-Mageuzi, kufutwa matokeo ya Bunda kwa Wasira ilikuwa personal dhihaka ya Tume ya Rushwa iliyoongzwa na Warioba mwenyewe baada ya kushindwa uchaguzi huo na Wassira .Hivi sasa ndani ya CCM, Tyson, ni mjumbe wa NEC kupitia lile kundi la kifo (Super 20).

Katika enzi za challenge za ethics,rushwa, mafisadi wa BOT,Buzwagi,etc, si shangai kwa nini jina la Tyson likitajwa kuwa nafasi hiyo...Ni that No non-sense,experienced guy asiyeogopa mtu, wala mapambano na mtu..

Yaani HATA Masatu kuwa Waziri Mkuu!!!!.Eeh
 
Hizi habari mbona sizielewi? zimetoka wap? yaani hata Tyson anaweza kuwa Waziri Mkuu katika njii hii kweli au masihara hayo,na Lowassa atakuwa nani? maswali mengi kuliko majibu,naomba ufafanuzi.
 
Kwanini anaitwa Tyson??? wana udugu au alipotwanga mtu ngumi???

Mina karamagi watamkoma!!!!
 
Kwanini anaitwa Tyson??? wana udugu au alipotwanga mtu ngumi???

Kina karamagi watamkoma!!!!
 
Swala la Uwaziri Mkuu ni swala ambalo Rais JK pekee ndio anajua na ataamua kama atafanya hayo mabadiliko ya kiwango hicho, Waziri Mkuu yupo na yupo kwa sababu zake JK mwenyewe..

Maoni ni Maoni na Facts ni Facts.

Siasa za Mara, hata Tarime ambayo Chacha Wangwe alishinda ni CHADEMA..Mara ni Aggressive Politics by nature ya wa-mara (hata wanapigana mawe saa zingine,Chambiri huko Tarime), CCM ilianguka Tarime 2005..Bunda CCM Tyson aliwashinda akiwa Upinzani NCCR against Jaji Sinde Waryoba, Jimbo la Mwibara Upinzani ulikuwa na hilo Jimbo kupitia TLP mpaka 2005,na sasa halina mbunge-mahakama imetengua ubunge, Musoma Vijijini NCCR (Balozi Ndobo) alikuwa Mbunge 1995..Rorya Mabere Marando akiwa NCCR-Maguezi aliwahi kuwa Mbunge, hata Musoma Mjini 2005, Dr Wandwi angemshinda Veda Mathayo isingikuwa Tyson kupiga sana Kampeni,nao walienda mahakamani ...Majimbo yote ya Mara yako hivyo siku zote,sasa Visasi ni tabia ya mtu, sio kitu unaweza kupima kwa kuangalia resume/CV au kusema hawezi kufuata Ilani ya Uchaguzi ya CCM--akiwa Waziri Mkuu ndio ataanza visasi? huwezi tabiri hayo yote ..Tyson aliwaangusha wote hao katika uchaguzi sasa kama Bwire-Mugeta (alikuwa Mwalimu) na Warioba (aliwahi kuwa Waziri Mkuu, ni ushindani hata kupata M/kiti wa Wilaya ni Burudani tupu..




Alitangazwa kwenda masomoni awamu ya pili ya Rais A.H Mwinyi na hapo Prof . Philemon Sarungi akawa Mkuu wa Mkoa wa Pwani (1992), Wassira alienda kujiendeleza masomoni baada ya 1991. Huwezi kupata degree kwa Miaka Miwili ukiwa ubalozini, hata Strayer University au University of Phoenix On-line hawatoi haraka hivyo...Ila kwa System navyoielewa ya Elimu Marekani watu wanaweza kupata GED tu na kuingia moja kwa moja Chuo kikuu, sembuse darasa la 8 kama unafanya Pre-college examination, unapata Admission.Watu hupata credit hours za experience, let alone college admission..Alafu American University ni chuo kikubwa kinajulikana kiko Washington DC, lazima alifuata taratibu zote.

Hamna anayejua kweli kama hili "Tyson "Wassira" kuwa Waziri Mkuu?" linaweza kutokea au laa (JK Mwenyewe anajua) ..Ila Najua Waziri Mkuu ni mtu (mwenye mandate) ambaye anaweza kufuata Ilani za Maendeleo, kama ilani ya CCM ya Uchaguzi ipasavyo na ni mtu ambaye yuko tayari kuchafuka, kuingia sokoni Kariakoo Asubuhi mapema ikibidi,kutoa maamuzi magumu, kutembea kwenye Matope ikibidi, ufupi kuwa Msaidizi wa Rais ambaye anaweza kuongoza bila kulinda watu au Kuogopa mtu.

Kama ni uongozi, sijui kama vigezo hivyo havipo au kiuwezo katika resume tuliona hapo.


Hii nitajibu haraka kabla sijaingia mitini.

Asante, nadhani wewe unafahamu taarifa za Tyson kwa kina. Mimi pia namfahamu sana, ndiyo maana najua kuwa ni mtendaji kazi na mpiga kampeini mzuri lakini ana weaknesses fulani fulani zinazomfanya akose sifa ya kuwa kiongozi mkuu kama PM. Ninakubaliana na views zako zikiwa na mashihisho yafuatayo.


(a) Swala la uteuzi wa PM liko mikononi mwa President, ambaye anaweza kumteua mtu yeyote: kilaza au kipanga. Hiyo ni fact na wala haipingwi. Maoni yangu yalikuwa juu ya yatoakanayo na uteuzi wa namna hiyo. Nina imani kuwa ukiwa kiongozi mwenye visasi, huwezi kutenda haki katika madaraka yako. Ndiyo maana nikasema kuwa kwa vile Tyson ana tabia ya kuendeleza visasi vya kampeini hata kama baada ya kushinda uchaguzi, basi hawezi kuwa PM mwenye kutenda haki. Viongozi huongoza kwa msingi kuwa watawatendea haki raia wote bila kujali itikadi zao, hata kama hawakumpigia kura.

(b) Siasa za Mara ni kweli ziko aggressive sana, hata hivyo ni jukumu la kiongozi aliyechaguliwa kuwaunganisha tena watu pamoja na kusahau mizengwe ya kampeini badala ya kuindeleza kwa madai kuwa "fulani ananipiga vita," phrase ambayo ni ya kawaida kwa Tyson.

(c) Kuhusu Tyson kwenda kusoma, inawezekana kweli kuwa kutokea Mkoa wa Pwani alikwenda kusoma tena, lakini aliporudi kugombea uchaguzi wa kiti cha Bunda mwaka 1985 akitokea DC, alikuwa na digrii tatu alizokuwa amepata katika kipindi hicho cha miaka miwili. Nilisoma maelezo yake binafsi aliyotoa wakati wa kampeini za ubunge; hata elimu yake ya awali ilikuwa imeongezewa kuwa alimaliza darasa la 12 huko Bwiru Sekondari. Hiyo ilikuwa in contrast na maelezo aliyokuwa ameyatoa wakati wa uchaguzi wa mwaka 1970 alipoonyesha kuwa alikuwa amemaliza darasa la nane pale Nyambitilwa.

(d) Kuhusu ukwe wake kwa Nyerere kweli haiwezi kuwa sehemu ya CV ya mtu, lakini ilikuwa ni mojawapo ya facts zilizomfanya Nyerere awe na upendeleo fulani kwa Tyson.

(e) Kuhusu jina la "Tyson" alijipachika alipotishia kumpiga ngumi mwandishi mmoja wa habari pale Maelezo alipokuwa akiohjiwa kuhusu kesi ya Uchaguzi ya mwaka 1995. Nadhani hakufurahia swali moja aliloulizwa na mwandishi yule, basi akahamaki na kumtishia kumpiga ngumi akisema yeye ni Tyson.
 
Jina La 'tyson' Wasssira Ikumbukwe Lilikuja Wakati Wa Kifo Cha Tupac, Ambaye Alipigwa Shaba Baada Tu Ya Mpambano Wa Mike Tyson (1996) Vegas..umaarufu Mpya Wa Tyson Muda Huo Ktk Ndondi Ukafananishwa Na Upset (ko) Ya Kumshinda Kigogo ,incumbent & Former Pm Warioba Ktk Uchaguzi Jimboni Bunda Akiwa Upinzani..

Ni Baada Ya Uchaguzi Wa Kwanza Wa Vyama Vingi
 
Jina La 'tyson' Wasssira Ikumbukwe Lilikuja Wakati Wa Kifo Cha Tupac, Ambaye Alipigwa Shaba Baada Tu Ya Mpambano Wa Mike Tyson (1996) Vegas..umaarufu Mpya Wa Tyson Muda Huo Ktk Ndondi Ukafananishwa Na Upset (ko) Ya Kumshinda Kigogo ,incumbent & Former Pm Warioba Ktk Uchaguzi Jimboni Bunda Akiwa Upinzani..

Ni Baada Ya Uchaguzi Wa Kwanza Wa Vyama Vingi

Hapana, nadhani huelewi chanzo cha jina la "Tyson." Mzee huyu alijiita mwenyewe kuwa anaweza kumpiga ngumi mwandishi fulani kwa madai kuwa yeye ni kama "Tyson" wakati anoangelea kesi iliyokluwa imefunguliwa kupinga ushindi wake pale kwenye ukumbi wa Maelezo. In fact alimpiga ngumi, na yule mwandishi alifungua kesi ingawa baadaye aliifuta baada ya kusuluhishana nje ya mahakama.

Hilo pambano la Mike Tyson na Evander unalodai kuwa ndilo lililofanya "Tyson" apewe jina hilo siyo kweli kwa vile baada ya pambano hilo na Mike Tyson kutolewa kwa TKO na Evander, hakuwa na umaarufu tena wa kuweza kufananishwa na mshindi dhidi ya Waryoba (1995) hadi aitwe "Tyson" (1996.)
 
Kichuguu,
You are right on this. Jina Tyson alijipachika baada ya kumkwida konde yule mwandishi wa habari. Lakini itakuwa interesting kumwona Wassira akiwa waziri mkuu. The only thing going for him ni kwamba ( as far as I know) hajaguswa na corruption iliyokithiri katika serikali yetu.
 
Kifo cha Tupac Shakur ni (1996) haikuwa Tyson na Evander, ilikuwa the in-famous "Fix Fight" kati ya Tyson na Bruce Seldon, kupata WBA Title aliyejidondosha Round 1. Tulikuwa tunakesha kuangalia mapambano ya Tyson mpaka asubuhi,ilikuwa 1996...Kesi za Uchaguzi haziwezi kuwa 1995 hiyo hiyo, ni 1996 baada ya Uchaguzi...Tyson na Evander ni 1997..1996 Tyson alikuwa maarufu na ilizidi sababu ya Warioba sio Mwandishi..Ni kweli alijita mwenyewe, habari zika-repoti..Facts are Facts
 
Kichuguu,
You are right on this. Jina Tyson alijipachika baada ya kumkwida konde yule mwandishi wa habari. Lakini itakuwa interesting kumwona Wassira akiwa waziri mkuu. The only thing going for him ni kwamba ( as far as I know) hajaguswa na corruption iliyokithiri katika serikali yetu.

Ni kweli, kwa corruption yuko safi kabisa kulinganisha na viongozi wengine wengi walioko madarakani sasa hivi. Hajahusika na corruption yeyote ya kishindo katika kipindi cha miaka 20 iliyopita zaidi ya ule upendeleo alioufanya kwa kaka yake George Wassira pale Pamba House.

Hata hivyo, siamini kuwa yuko clean kabisa kwani huenda hajapata nafasi ya kuonyesha makucha yake. Wakati akiwa RC wa Mara kulitokea madai yaliyomhusisha na utoroshwaji wa majora ya vitenge vya MUTEX ambavyo vilikuwa vikipelekwa Kenya kuwekwa label ya kiwanda fulani cha Kenya kabla ya kurudishwa TZ kama "vitenge vya Mombasa."

Kifo cha Tupac Shakur ni (1996) haikuwa Tyson na Evander, ilikuwa the in-famous "Fix Fight" kati ya Tyson na Bruce Seldon, kupata WBA Title aliyejidondosha Round 1. Tulikuwa tunakesha kuangalia mapambano ya Tyson mpaka asubuhi,ilikuwa 1996...Kesi za Uchaguzi haziwezi kuwa 1995 hiyo hiyo, ni 1996 baada ya Uchaguzi...Tyson na Evander ni 1997..1996 Tyson alikuwa maarufu na ilizidi sababu ya Warioba sio Mwandishi..Ni kweli alijita mwenyewe, habari zika-repoti..Facts are Facts

Inawezekana kuw kifo cha Tupac kilitokea kabla ya pambano la Tyson na Evander, hata hivyo jina la "Tyson" kwa Mzee Wassira ni la kujipachika na wala halikuwa na uhusiano wowote na ushindi wake dhidi ya Waryoba.
 
dah! ila you guys (kichuguu and serengeti) u dig zis man inside- out,Kwa upande wangu naungana mkono nawe Kichuguu huyu bwana hastahili kabisa kuwa PM basing na mambo uliyosema ila kubwa ni mtu wa jazba na visirani kweli..Hatutaki ubabe katika kuongoza watu maana wa Tz wenyewe tayari ni wanyonge sasa ubabe wanini tena..Hope kwa sasa JK hana mpango wa kufanya changes may be later on...but NOT zis year
 
DAR si LAMU, Resume ya Steven Wasira ambayo iko Wikipedia inaonyesha mtiririko ufuatayo: Kuna utofauti wa Miaka na Tarehe zilizowekwa na Kichuguu...


# Member of Parliament - Mwibara Constituency 1970 - 1975

# Deputy Minister of Agriculture 1972 - 1975

# Regional Commissioner Mara Region 1975 - 1982

# Minister Counselor at the Embassy of Tanzania, Washington, DC, USA - 1982 - 1985

# Member of Parliament - Bunda Constituency 1985 -1990

# Deputy Minister for Local Government 1987-1989

# Minister of Agriculture and Livestock Development 1989- 1990

# Regional Commissioner Coastal Region 1990 - 1991

# Member of Parliament - Bunda Constituency 1995 -1996

# Member of Parliament - Bunda Constituency 2005 -Present

# Minister for Water - Jan 2006 - Oct 2006

# Minister of Agriculture and Food Security - 2007 - Present


Education ya Wassira inaonyesha,mwanasiasa huyo ana shahada kama nne alizopata nchini Marekani

BA in Economics, American University in Washington, DC, USA.

BA in Political Science, American University in Washington, DC, USA.

MA in Economics, American University in Washington, DC, USA.

Masters in Public Administration, American University in Washington, DC, USA.


Wassira ana resume ndefu iliyomweka Bungeni akiwa na miaka 25,na kuwa Deputy Minister Agriculture akiwa na umri mdogo wa miaka 27 ..Wassira is a seasoned politician kwa muda alioanza katika public service, kiumri anapishana miaka mitano tu na JK,kawahi kuanza uongozi...JK kazaliwa 1950, Wasira 1945 .

Ripoti ya REDET iliyoangalia performance ya Wizara za Serikali ya JK, Waziri Wassira amekuwa rated juu akitokea Maji, Kuwa promoted Wizara hiyo kubwa na Nyeti (Kilimo), amerekebisha Biashara ya korosho kati ya Wananchi na wanunuzi, kafukuza kazi watendaji warasimu na wahujumu, na kufuta vibali vya makampuni yaliyogoma kununua bei ya kufaidisha maslahi ya wananchi. Kilimo kazi sio rahisi,Wizara inayolenga 80% ya wananchi,wengi maskini, lakini walio ndani ya wizara hiyo na bodi zake za mazao wamenukuliwa wakisifu bidii iliyojitokeza baada ya Tyson kuhamia pale.

Uchaguzi wa 2005, Tyson katika Jimbo la Bunda alipita bila kupingwa (walikuwa kama watano hivi nchi nzima).Ukweli Tyson Bunda na Mara anapendwa na watu,umaarufu wake unaweza kulinganishwa na Mwandosya kule Mbeya.

Na uhasisi wa jina lake "Tyson", ambalo JK pekee ndio mwenye ruhusa ya kulitumia jina hilo, according to Tyson au Wassira mwenyewe,ulitokana na uwezo wake kujenga hoja na sifa yake kisiasa katika uchaguzi wa jimbo la Bunda 1995 ambapo alimwangusha na kumstaafisha siasa Waziri Mkuu wa zamani Jaji Joseph Sinde Warioba anayetokea vijiji vya ikizu jimbo hilo hilo la Bunda kupitia ticket ya NCCR-Mageuzi.Mizengwe ya CCM Bunda ilimhamisha Tyson kwenda NCCR-Mageuzi, kufutwa matokeo ya Bunda kwa Wasira ilikuwa personal dhihaka ya Tume ya Rushwa iliyoongzwa na Warioba mwenyewe baada ya kushindwa uchaguzi huo na Wassira .Hivi sasa ndani ya CCM, Tyson, ni mjumbe wa NEC kupitia lile kundi la kifo (Super 20).

Katika enzi za challenge za ethics,rushwa, mafisadi wa BOT,Buzwagi,etc, si shangai kwa nini jina la Tyson likitajwa kuwa nafasi hiyo...Ni that No non-sense,experienced guy asiyeogopa mtu, wala mapambano na mtu..

Ahsante Serengeti kwa kutufahamisha yale ambayo wengi wa wachangiaji hapa JF hawatendi hata kama wanajua ukweli ulivyo.
 
madai yaliyomhusisha na utoroshwaji wa majora ya vitenge vya MUTEX"

Tanzania huwezi kupendwa na kila mtu, hilo tunajua..Ila ukweli skendo za awamu ya Nyerere compared na sasa ni kama kufananisha kuondoka kazini na penseli za ofisi uki compare na ufisadi wa sasa..

Siamini majora ya vitenge MUTEX, sio MWATEX ni skendo serious sana!..? tena akiwa RC miaka 30 iliyopita..Anyway, kila mtu ana haki na maoni yake...Opinion ni opinion, Facts are Facts..

Facts nimepata, nimeona ni share..

Tyson aliwahi kugombana na kumpiga konde mwandishi, hii ilikuwa (1999)..Hii Haikuwa mwanzo wa jina la Tyson

Alitumia pambano la Ndondi la Tyson, Tyson akiwa bado maarafu (1996) kuelezea kesi ya Uchaguzi na kuwa hata wakirudia uchaguzi Jimboni Bunda, atamwangusha tena Waryoba, yeye kama Tyson, ilikuwa baada tu ya Pambano la Tyson vs Seldon,na kifo cha Tupac (1996).Anayekumbuka hilo pambano jamaa Seldon alikuwa kichekesho sababu alijirusha tu bila kupigwa na Tyson...

Hii ni Typical swagger ya watu wa Mara kujisifu, Wassira akajiita Tyson kumkebehi Waryoba kisiasa. Baadae Kesi ikamfungia Ubunge 1997, jina lilishakuwepo.

Kichuguu yuko sahahi, kesi yake na Mwandishi ilikuwa solved nje ya Mahakama, hii ni baadae kabisa baada ya kesi zake za uchaguzi wa 1995,akiwa hayuko tena upinzani na amefungiwa kugombea ubunge na Mahakama..ilikuwa ni (1999), tayari jina lilikuwepo

Umaarufu na jina la Tyson ilikuwa juu wakati wa Uchaguzi na kesi ya uchaguzi kati ya 1996-1997, issue ya huyo mwandishi Jina lilishakuwepo na of-course ni rahisi watu ku-relate makonde na jina lenyewe boxer Tyson..ila Mike Tyson alishaisha 1999 na huwezi wakati huo kujiita Jina la Bondia mfu kujisifi..Mara hii It doesnt make sense. Mara people know this stori well...
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom