Two Medical Doctors Drown in Sanje Water Falls

Tupendane

New Member
Apr 22, 2008
3
0
Kuna madaktari wawili walizama katika bwawa lililopo katika maporomoko ya maji pale Sanje Water falls- Kilombero siku ya Jumamosi (April 11th, 2009). Madaktari hao ni walimu katika chuo cha Tanzania Training Centre for International Health (TTCIH) kilichopo Ifakara. Madaktari hao (marehemu Dr Alute na Dr Mujuni) walikwenda sehemu hiyo ya kitalii wakiwa na wenzao wawili lakini mmoja wao alishindwa kufika katika kilima hicho na hivyo kumuomba Guide amsindikize arudi na wenzake watatu wakaenda bila ya Guide. Walipofika kwenye bwawa lililopo kwenye maporomoko hayo mmoja alienda kwenye maji na kutaka apigwe picha na baada ya kupigwa picha mpiga picha alimuambia kuwa picha yake ilikuwa nzuri sana hivyo kwa hamasa wakati anataka kukimbilia kuiona picha yake akateleza na kusombwa na maji kuelekea sehemu ambako kuna maji yenye pressure kali yanayoelekea kwenye mapango. Mwenzake aliyekuwa anampiga picha alipotaka kwenda kumuokoa naye akasombwa na maji na yule wa tatu akakimbia kurudi walikotoka kuomba msaada.

Jitihada za kupata miili ya marehemu hazikufanikiwa hadi leo baada ya wanajeshi wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania kikosi cha Navy kuwasili na kufanikiwa kuyatoa maiti baada ya kukaa majini kwa muda wa takriban siku nne. Miili yao imeletwa St. Francis Designated District Hospital around saa kumi jioni hii.

Tukio hili linatoa fundisho kuwa ni muhimu kuchukua tahadhari tunapokwenda sehemu za hatari kama hizo. Ni muhimu pia kuwa na Guide na kufuata maelekezo yao.

Mungu aziweke roho za marehemu mahala pema peponi
AMEN
 
Ajali bwana haina Kinga....Poleni wafiwa ndugu na wazazi wa Drs Alute na Mujuni...roho za marehemu zipumzike kwa amani...na jina la bwana lihimidiwe maana kazi yake haina makosa!
 
Ni vyema miongozo ya safari za maeneo ya kitalii zikatolewa na pengine hata kuweka alama kama vile za barabarani katika maeneo hayo.
 
Inasikitisha kupoteza wananchi hawa, kifo mahala popote kwa mtu yeyote ni kitu cha huzuni kubwa.

Inasikitisha, walikuwa katika upeo mkubwa wa maisha yao, walikuwa na mchango mkubwa sana ukizingatia ni madaktari walimu katika nchi masikini ambayo uwiano wa madaktari na watu wengine (Tanzania) ni watu 260000 kwa kila daktari.

Tunatakiwa kujifunza kuwa wangalifu zaidi, kujifunza kuweka alama za tahadhari, kujifunza kuthamini hawa viongozi wa hii misafara ya kitalii. Ajali haina kinga lakini matukio ya ajali yanaweza kupunguzwa na tahadhari.

Wapumzike kwa amani ya milele.
 
Last edited:
Jamani kwa kweli ni huzuni kubwa sana hasa ukizingatia kua ni vijana wadogo sana. Nitamkumbuka daima dokta Alute kwa busara, upole na upendo wake. Bwana ametoa na bwana ametwaa. Mungu azilaze roho za marehemu pema peponi. Amen
 
:(:(:( Baadhi ya Picha za Maporomoko hayo nilizozipiga X-mas ya Mwaka jana 2008 nilipoenda na familia yangu Udzungwa Mountains especially Sanje Falls... :(:(:(

Kuna alama za kutosha ila kwa sababu hawakuwa na Guide ndipo walikumbwa na dhahama RIP:(:(:(
 
Binafsi nilishindwa kuamini kwani kama wiki moja kabla ya tukio hili tulipoteza a very young pharmacist,kabla habari hii ya kifo cha pharmacist haijatulia,nikahabarishwa kuhusi vifo vya madaktari hawa wawili.walikuwa bado wadogo kiumri na kiprofession,any way hatuna jinsi inabidi tukubali matukio.
 
:(:(:( Baadhi ya Picha za Maporomoko hayo nilizozipiga X-mas ya Mwaka jana 2008 nilipoenda na familia yangu Udzungwa Mountains especially Sanje Falls... :(:(:( Kuna alama za kutosha ila kwa sababu hawakuwa na Guide ndipo walikumbwa na dhahama RIP:(:(:(

Mkuu hukwenda kwa bibi Kalembwana kunyoa kweli.....!!
 
Mkuu hukwenda kwa bibi Kalembwana kunyoa kweli.....!!



Hapana Mkuu si unajua tena utalii wa ndani:)... Ila siku hiyo ya Xmas tukiwa ndani ya msitu huo radi zilikuwa zinapiga na mvua kubwa kunyesha tulikuwa kama sita hivi... Na tour guide mmoja,pale kwenye view point kuna kibanda wife wangu akadai haendelei kwani kulikuwa kuna upepo na kiza :oops: japo ilikuwa saa 9 za mchana tulimshawishi ndipo tukaendelea... kurudi kwenye starting point tukambiwa zile radi zilizokuwa zinapiga moja imeua mtoto mmoja aliyekuwa akipopoa maembe:(:(
 
Mkuu si unajua tena utalii wa ndani

Safi sana kuendeleza utalii wetu!! Mlifika hadi kule juu kabisa kwenye vyanzo vya maporomoko? Kuna siku nilipanda kule pia na washikaji, mvua ikatukuta, tulikuwa tunapiga mieleka ile mbaya....ni pazuri sana, na guide tuliyekuwa naye alikuwa anajua kila aina ya mti, sijui kama alikuwa anatupiga kamba! ilituchukua masaa 3 kupanda na lisaa 1 kushuka chini....baada ya hapo tulienda kwenye ile bar iliyo karibu na kuingilia ofisini tukashushia Tusker Bariiiidi's kabla ya kupiga misele pale kijijini Mkamba na kurudi zetu Dar taratibu!
 
Nilikuwa na dk mujuni mutabuzi wakati tuko o-level forodhani sec school alikuwa na akili sana darasani na alikuwa mcheshi sana na mwenye masihara lakini ana adabu nzuri kwa watu wote mungu ailaze roho yake mahari pema peponi
 
Hapana kule juu hatukwenda,tuliishia kwenye Base ya Sanje Falls maana tulikuwa pia na Watoto,Kufika hadi kwenye base ilituchukua masaa matatu. Kwa Sh.1000 si vibaya watu waende kutalii huko ila lazima usindikizwe na Guide...
 
Nilikuwa na dk mujuni mutabuzi wakati tuko o-level forodhani sec school alikuwa na akili sana darasani na alikuwa mcheshi sana na mwenye masihara lakini ana adabu nzuri kwa watu wote mungu ailaze roho yake mahari pema peponi

Kaka/dada you are spot on abt Mujuni..Last saw him at Mabibo Hostel...Was very Shocked Chunga Misonge aliponitaarifu
Lusekelo
RIP
 
Last edited:
Mh! Hilo ni swali gumu kwangu. Ila naamini kua ni mipango ya Mungu. Na kunapotokea dharura, akili ya binadamu hufanya kazi kwa haraka sana. Kwa nini umeniuliza swali kama hilo?
 

Tunatakiwa kujifunza kuwa wangalifu zaidi, kujifunza kuweka alama za tahadhari, kujifunza kuthamini hawa viongozi wa hii misafara ya kitalii. Ajali haina kinga lakini matukio ya ajali yanaweza kupunguzwa na tahadhari.

Methali na Misemo na Nahau na Wahenga Walisema, na Busara za Wote, na Convetional Wisdom.

Kama ni kweli ajali haina kinga basi tahadhari haiwezi kupunguza ajali kwa kuzikinga maana ajali haina kinga.

Na kama unasihi tujifunze kuwa waangalifu zaidi na kuchukua tahadhari basi tahadhari zetu zitasaidia kupunguza ajali kwa kukinga zile ambazo zingetokea bila tahadhari; kinga ya ajali.

Ajali haina kinga. Lakini tuchukue tahadhari. Kukinga ajali.

Ungeweza kutoa pole zako ukabonyea.
 
Back
Top Bottom