PingPong
JF-Expert Member
- Dec 21, 2008
- 926
- 160
Timu ya taifa ya soka ya wanawake ya Tanzania, Twiga Stars imeifunga timu ya taifa ya Ethiopia kwa mabao matatu kwa moja.
Mchezo huo umefanyika mjini Addis Ababa.
Mwenyekiti wa chama cha soka cha wanawake nchini Tanzania, Lina Mhando amekiambia kipindi cha Michezo na Wachezaji cha BBC kuwa goli la kwanza limefungwa na Esther Chamburuma.
Amesema bao la pili limefungwa na Mwanahamisi Omari la tatu kufungwa na Asha Rashid.
Timu hizo zitakutana tena wiki mbili zijazo, katika mechi itakayochezwa mjini Dar es Salaam.
Atakayeibuka mshindi baada ya mechi hizo mbili atacheza na Eritrea, kufuatia timu ya Kenya kuamua kujiondoa katika mechi hizo za kufuzu.
source: BBCswahili.com
Mchezo huo umefanyika mjini Addis Ababa.
Mwenyekiti wa chama cha soka cha wanawake nchini Tanzania, Lina Mhando amekiambia kipindi cha Michezo na Wachezaji cha BBC kuwa goli la kwanza limefungwa na Esther Chamburuma.
Amesema bao la pili limefungwa na Mwanahamisi Omari la tatu kufungwa na Asha Rashid.
Timu hizo zitakutana tena wiki mbili zijazo, katika mechi itakayochezwa mjini Dar es Salaam.
Atakayeibuka mshindi baada ya mechi hizo mbili atacheza na Eritrea, kufuatia timu ya Kenya kuamua kujiondoa katika mechi hizo za kufuzu.
source: BBCswahili.com