TWAWEZA: Tunaomba mtusaidie kuwauliza Uhamiaji wanataka nini?

Kurzweil

JF-Expert Member
May 25, 2011
6,622
8,397
HATIMA ya hati ya kusafiria ya Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti ya Twaweza, Aidan Eyakuze, bado haijafahamika, baada ya Idara ya Uhamiaji kusisitiza kuwa itaendelea kuishikilia kwa muda usiojulikana.

Idara hiyo imesema kuwa ingawa bado wanaendelea kuishikilia hati hiyo, Mkurugenzi huyo anaweza kufuata masharti aliyopewa kama anataka kusafiri nje ya nchi kikazi.

“Tunaendelea kuishikilia hiyo hati, lakini kama anataka kusafiri yapo maelekezo ya ofisi ambayo tumempa ya nini anatakiwa kufanya, akitimiza anaweza kuruhusiwa kusafiri,” alisema Msemaji wa Idara hiyo, Ali Mtanda.

Mmoja wa maofisa wa Twaweza ambaye aliomba jina lake lisitajwe, aliliambia Nipashe hivi karibuni kuwa wamejitahidi kuifuatilia hati hiyo kwa muda mrefu, lakini wameshindwa kuipata na majibu ni kwamba uchunguzi unaendelea.

Alisema wamekuwa wakiandika barua mbalimbali wakiomba kupatiwa hati hiyo, lakini Idara hiyo imekuwa ikiwajibu kuwa inaendelea na uchunguzi ingawa hawasemi watakamilisha lini.

Ofisa huyo alisema Mkurugenzi huyo hajasafiri nje ya nchi tangu hati yake ishikiliwe Julai 24, mwaka huu hivyo amekuwa akikosa mikutano mbalimbali muhimu ya kimataifa na kikanda.

“Sisi tuna ofisi zingine Kenya na Uganda ambako alipaswa kwenda mara kwa mara kwaajili ya shughuli za kiofisi, lakini amekwama kutokana na hati hiyo kuendelea kushikiliwa na Uhamiaji,” alisema.

“Tunaomba mtusaidie kuwauliza Uhamiaji wanachotaka nini kwasababu miezi minne yote hawajachunguza na kupata taarifa wanazotaka au ni kumkomoa mtu jamani,” alisema ofisa huyo.

Alipozungumza na waandishi wa habari baada ya hati yake kushikiliwa Agosti, mwaka huu, Eyakuze alisema hakuelezwa sababu za kushikiliwa kwa hati hiyo ambayo alinyang’anywa Julai 24, mwaka huu.

Alisema alipokea wito kutoka Uhamiaji kwamba anatakiwa na baada ya kufika, aliambiwa aandike maelezo na siku ya pili alitakiwa kuwasilisha hati yake ya kusafiria.

Alisema Agosti Mosi, alizuiwa kusafiri kwa kutumia shahada ya dharura iliyotolewa kwa utaratibu uliopo ili aweze kushiriki mikutano ya kikazi kwenye ofisi ya Twaweza jijini Nairobi na Kampala, Uganda.

Chanzo: Nipashe
 
Huyu ndiye Aliyetabiliwa na marehemu mzee kingunge Kuwa alistahili Kuwa mnyampala wa barabara na si vinginevyo sasa yametimia
Hahahaha si angekuja na utafiti Kichaa anakubalika kwa asilimia 1000% maana anajenga situgilazi joji kwa Hela za ndani, Standard geji, miradi mingi Sana, bajeti ya dawa imeongezwa, yaani Jiwe kafanya mengi kwa miezi mitatu tuu
 
Hivi unaenda kuomba hati huku excuse ikiwa ni unakosa mikutano?? Unajua rais kakosa mikutano mingapi?

Na kama tumekubaliana kuishi kama mashetani unataka kutumia ndege ya nini? Shetani wewe hauna mabawa?
 
Yule kilaza asiyejua Kiingereza licha ya kusoma karibu miaka 18 kwa kutumia lugha ya Kiingereza wanamwabudu sana. Ukimwambia hajui Kiingereza anaanza kucharuka oooohhhooo mara Mbona Wachina wapo ambao hawajui Kiingereza licha ya kwamba ni wasomi na wataalamu, huku anajifanya kusahau kuwa hao wachina walijifunza kwa lugha yao ya Kichina.
Mungu wako ni kile kitu unachokipa kipaumbele na kukihofia au kukitukuza ndani kabisa ya moyo wako na si yule anayetajwa kwenye majengo ya ibada, anaweza akawa yule unayemtaja kanisani au msikitini au kwenye hekalu endapo tu na moyo wako utakuwa unafanya kama Yale unayoyafanya kwenye haya majengo ya ibada.
 
HATIMA ya hati ya kusafiria ya Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti ya Twaweza, Aidan Eyakuze, bado haijafahamika, baada ya Idara ya Uhamiaji kusisitiza kuwa itaendelea kuishikilia kwa muda usiojulikana.

Idara hiyo imesema kuwa ingawa bado wanaendelea kuishikilia hati hiyo, Mkurugenzi huyo anaweza kufuata masharti aliyopewa kama anataka kusafiri nje ya nchi kikazi.

“Tunaendelea kuishikilia hiyo hati, lakini kama anataka kusafiri yapo maelekezo ya ofisi ambayo tumempa ya nini anatakiwa kufanya, akitimiza anaweza kuruhusiwa kusafiri,” alisema Msemaji wa Idara hiyo, Ali Mtanda.

Mmoja wa maofisa wa Twaweza ambaye aliomba jina lake lisitajwe, aliliambia Nipashe hivi karibuni kuwa wamejitahidi kuifuatilia hati hiyo kwa muda mrefu, lakini wameshindwa kuipata na majibu ni kwamba uchunguzi unaendelea.

Alisema wamekuwa wakiandika barua mbalimbali wakiomba kupatiwa hati hiyo, lakini Idara hiyo imekuwa ikiwajibu kuwa inaendelea na uchunguzi ingawa hawasemi watakamilisha lini.

Ofisa huyo alisema Mkurugenzi huyo hajasafiri nje ya nchi tangu hati yake ishikiliwe Julai 24, mwaka huu hivyo amekuwa akikosa mikutano mbalimbali muhimu ya kimataifa na kikanda.

“Sisi tuna ofisi zingine Kenya na Uganda ambako alipaswa kwenda mara kwa mara kwaajili ya shughuli za kiofisi, lakini amekwama kutokana na hati hiyo kuendelea kushikiliwa na Uhamiaji,” alisema.

“Tunaomba mtusaidie kuwauliza Uhamiaji wanachotaka nini kwasababu miezi minne yote hawajachunguza na kupata taarifa wanazotaka au ni kumkomoa mtu jamani,” alisema ofisa huyo.

Alipozungumza na waandishi wa habari baada ya hati yake kushikiliwa Agosti, mwaka huu, Eyakuze alisema hakuelezwa sababu za kushikiliwa kwa hati hiyo ambayo alinyang’anywa Julai 24, mwaka huu.

Alisema alipokea wito kutoka Uhamiaji kwamba anatakiwa na baada ya kufika, aliambiwa aandike maelezo na siku ya pili alitakiwa kuwasilisha hati yake ya kusafiria.

Alisema Agosti Mosi, alizuiwa kusafiri kwa kutumia shahada ya dharura iliyotolewa kwa utaratibu uliopo ili aweze kushiriki mikutano ya kikazi kwenye ofisi ya Twaweza jijini Nairobi na Kampala, Uganda.

Chanzo: Nipashe
Mahakama hazipo hadi muombe magazet
 
Mimi naona wamrudishie huyo mkurugenzi passport yake kwa kipindi cha miezi miwili halafu waichukue tena kwa uchunguzi zaidi, kama bado wanaendelea kufanya uchunguzi.

Kwenye huo utafiti wa Sauti za Wananchi wawa ambie Twaweza kwamba sample ya utafiti iwe representative also at the regional level na sio only at the national level, due to sensitivity ya presidential opinion polls in under developed countries like Tanzania.

Of course, Twaweza wanaweza kusema itakua expensive kuwa na sample ya hivyo, na kwamba sample ya national level ya around watu 2,000 inatosha.

Lakini mimi naona kwenye mambo ya umaarufu wa Rais au umaarufu wa wagombea urais watumie sample ambayo ni representative at the regional level as hii ita aminika zaidi na pande zote. Na pia haita yumbisha mambo ya peace, stability, national unity na national security. COSTECH na NBS nadhani ndo huwa wanasimamia mambo ya vibali vya utafiti.

Ita kuwa vizuri Twaweza wa compromise na ku accept hii sampling level kama ita saidia wa aminike zaidi na watu mbali mbali including upinzani na serikali.
 
Hivi unaenda kuomba hati huku excuse ikiwa ni unakosa mikutano?? Unajua rais kakosa mikutano mingapi?

Na kama tumekubaliana kuishi kama mashetani unataka kutumia ndege ya nini? Shetani wewe hauna mabawa?
Sasa Raisi anahusikaje hapa au ndo uwezi mdogo wa kujenga hoja
 
TOA UTAFITI UNAOSEMA JIWE ANAKUBALIKA ASILIMIA MIA MOJA,NI BORA KULIKO NYERERE NA HATOKAA KAMWE ATOKEE RAIS KAMA YEYE,SEMA ASILIMIA 98 WANAMLILIA ABAKI IKULU HADI 2050 UTAPATA PASSPORT YAKO
 
Back
Top Bottom