tanga kwetu
JF-Expert Member
- May 12, 2010
- 2,194
- 1,434
...huwa nafuatilia sana taarifa za habari za hapa bongo na vituo vya nje kama CNN, BBC na SANBC. Vituo vya nje vinapotangaza matokeo ya mechi fulani ya soka huwa lazima virushe clip za mabao. Mathalani kama mechi imeisha 3-2, lazima utaonyeshwa mabao yote matano yalivyopatikana. Lakini TV zetu za Bongo mara nyingi sana (almost 95%) hawaonyeshi mabao hata kama mechi ilikuwa na mabao kadhaa. Afadhali kama hawana record ya hiyo mechi lakini wanakuwa nayo na mbaya zaidi wanaonyesha vipande vya matukio mengine katika hiyo mechi kama vile chenga, kona na move za ajabuajabu. Inanikera sana! Naomba wabadilike katika hili