TV Program Alert: Vipindi vya Wajibu wa AZAKI Kuelekea Katiba Mpya

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,337
113,178
Wanabodi,

Nawakaribisha kutazama vipindi maalum vya Wajibu wa Asasi za Kijamii kuelekea kwenye Katiba Mpya.

Vipindi hivyo vinaanza leo Alhamisi na Kesho Ijumaa kwenye ITV saa 1:00-1:30 jioni. Kwa TBC, Vipindi hivi vitarushwa kila siku Saa 1:30-2:00 usiku.

Katika kipindi cha Kwanza, Prof. Shivji, atatoa mada ya mchakato wa kupata katiba bora na halali.

Prof. Shivji, ameuponda mchakato wa kukusanya maoni unaendelea kuwa hauwezi kutupatia katiba bora na yenye uhalali wa kikatiba "The constitutionalism of the constitutional"

Fuatilia vipindi hivi mjifunze mengi.

Asanteni.

Pascal.

Mada ni kama zifuatazo.

TV PROGRAMS ZA TAMASHA LA AZAKI 2012
Wajibu wa Asasi za Kiraia Katika Mchakato wa Kuandaa Katiba Mpya

Program 1
Dur: 30 min
Program 2
Dur: 30 min
Program 3
Dur: 30 min
Program 4
Dur: 30 min
Kukaribisha Wadau na Utambulisho-Mkurugenzi FCS

Neno la ukaribisho na Maudhui ya Tamasha – Mwenyekiti wa Bodi ya FCS


Uwasilishaji wa mada : Masuala ya Msingi ya kuzingatia katika mchakato wa kuandaa katiba ya kidemokrasia :
Prof. Issa Shivji


Ufunguzi
Kumkaribisha Mgeni Rasmi –Raisi FCS

Hotuba ya Ufunguzi-Joseph Butiku Mkurugenzi Mwalimu Nyerere Foundation
Neno la shukrani- Mwakilishi kutoka Azaki

Jopo: Wajibu wa Asasi za kiraia katika Mchakato wa kuandaa katiba

FCS Members




Warsha za Kisekta : Mtazamo kutoka kwa :

  1. Wakulima/ Wavuvi (MVIWATA/ Mtandao wa Wavuvi)/Wafugaji/Wawindaji/wakusanyamatunda/(PINGOs Forum)
  2. Elimu - Haki elimu/ Ten Met
  3. Afya - Sikika
  4. Wajibu wa Serikali za Mitaa- MARCOSSY ALBANIE
  5. Uhuru wa kupata habari na Uhuru wa kutoa maoni –MCT, MOAT- Henry Muhanika
Mjadala wa pamoja : Maadili ya Uongozi katika Katiba Mpya;

  1. Moses Kulaba
  2. Gema Akilimali
  3. Kamishna wa Tume ya maadali


Program 4
Dur: 30 min
Program 5
Dur: 30 min
Program 6
Dur: 30 min
Program 7
Dur: 30 min
Mihimili ya Dola na Madaraka yake katika katiba mpya

  1. Chama cha majaji Wastaafu
  2. Francis Stolla
  3. Marcossy Albanie
  4. Harold Sungusia

Masuala ya Muungano katika Katiba Mpya

  1. Ismael Jusa
  2. Ibrahim Mzee Ibrahim
  3. Dr. Mohamed Bakari
  4. Francis Kiwanga

Warsha: Masuala Mtambuka

  1. Jinsia (TGNP/TAWLA/TAMWA)
  2. Walemavu (SHIVYAWATA/DOLASED)
  3. Vijana (YPC/TAYODEA/MARK OKELO)
  4. Mafuta na Gesi-POLICY FORUM/SALAS OLANG
  5. Maliasili –TNRF/KAMA
  6. Haki za Binadamu na Hati ya Haki za Binadamu katika katiba Mpya LHRC/SAHRINGO
Itikadi Ipi tunayoifuata : Ujamaa au Ubepari?

  1. Prof. Marjorie Mbilinyi
  2. Felix Mosha
  3. Prof. Wangwe

Program 8
Dur: 30 min
Program 9
Dur: 30 min
Program 10
Dur: 30 min
Program 11
Dur: 30 min
Mjadala wa pamoja kuhusu Ardhi katika katiba Mpya



  1. HAKIARDHI (Yefred Myenzi


  1. Dr. Rugemeleza Nshala

Huduma zinazotolewa na FCS: Maswali na Majibu

Mkurugenzi FCS

Nini kifanyike: Uwasilishaji wa Masuala ya Msingi yaliyoibulliwa na AZAKi ya kuzingatia katika
K atiba Mpya

Mjadala wa pamoja kuhusu Masuala ya msingi yaliyojitokeza katika mada zote


  1. Hamphrey Polepole
Kufunga

  • Kutoa Tuzo
  • Maelezo ya kufunga Tamasha – Bi. Salama Kombo
  • Neno la Shukrani – Mwenyekiti Bodi ya FCS
Program 12
Dur: 30 min
Program 13
Dur: 30 min
Program 14
Dur: 30 min
PRODUCTION
Maoni ya Wadau Kuhusu Tamasha la 10 la AZAKI kwa Mwaka huu 2012 (Done)

AZAKI zilizo shinda Tuzo, zimeshinda kwa vigezo gani, na zimefanya nini kustahili tuzo hizo (Done)
Ijue The Foundation for Civil Society, malengo, viongozi, utendaji.
PPR PRODUCTION
 
Mkuu Pascal

Mda wa Dk 30 naona kama ni mfupi sana walau DK 45 ungefaa zaid,. ni mtazamo wangu mkuu

Hata hivyo shukran sana mkuu.
Hakuna TV inayouza muda zaidi ya 30 min. Ukiona kipindi chochote ambacho ni cha zaidi ya 30min, ujue ni cha wenye TV station wenyewe!. Ndio maana vipindi viko vingi.
 
Najua hapo patamu na panashibisha.

Pascal you are a true qualified JF member (Great Thinker). Nitajitahidi kufuatilia.

Nashauri na wewe utu"engage" kwa mjadala wenye maudhui hayo humu kwenye JF nina hakika utakuwa na manufaa. Mods can help.
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom