TV Prog. Alert: Tume ya Uchaguzi, NEC, Yajibu Hoja za JF Kuhusu Uchaguzi Huru na Wa Haki!

Unakuja hapa kutaka kutuaminisha kwamba huyu mteule wa Rais ataongea kweli tupu kwamba uchaguzi ule haukuwa wa haki. Kama utakumbuka kuna kura zilikamatwa katika baadhi ya mikoa nchini na nyingine ziliokotwa kule Kagera. Serikali ilituzuia kusema chochote kuhusu kura zilizokamatwa na kuokotwa na kama utakumbuka kura zote zilikuwa zimeshapigwa kwa wagombea wa CCM tu.

Hebu itendee haki akili yako ya kumhoji mtu ambaye tungependa kumsikia badala ya huyu mteule wa Rais. Muhoji Mwenyekiti wa Tume ya maadili kuhusu uchunguzi wake ulipofikia wa wale waliopokea rushwa toka kwa Rugemarila na pesa za wizi za Escrow. Pamoja naye kuwa ni mteule wa Rais hili tunataka sana kulisikia.
 
Njaa mbaya sana Mkuu, bado yuko busy huyu kuuwania ukuu wa Wilaya.

as a matter of fact huyuhuyu Pascal Mayalla alikuwa anatuhumiwa kuinfluence uongozi wa JF kufuta threads ambazo zilikuwa critical kwa mabosi wake

he has no moral authority kutuambia kitu humu.
 
Kwa sisi wengine ndio 'tunarudi Duniani' hatukuona hicho kipindi. Je, aliulizwa chaguzi zijazo tume itatumia watu gani baada ya wakurugenzi wote wa halmashauri, miji na majiji kuwa ni makada wa ccm tu?
 
Paskali embu tuache tupumzike bwana. Hivi unataka tume iseme uchaguzi haukua huru na haki wakati wao ndio wasimamizi na waliyemsimamia walimtangaza mshindi? Subiri wanaemsimamia ashindwe ndo watakwambia haukua huru na haki kama ilivyotokea kwa jecha
 
Usingetaja TBC na STAR TV ningeiangalia hiyo video, naomba tusichoshane hapa...kama hata wewe hujui maana ya tume HURU ya uchaguzi basi kazi ipo. Mama Juma niongezee maharage nimalizie wali hapa.
 

Yaani huyo dogo Paskali huwa namuangalia nachoka kabisa, nimemuangalia asubuhi Star TV anasema tume ni huru lakini sio shirikishi, na huwa anasema hivyo kila mara hapa jukwaani! Lakini hajawahi kusema hiyo tume huru kuwa shirikishi inakuwaje. Anasema mahakama na bunge pia zipo huru na tumekubali, sasa sijui amekubali yeye na nani kuwa bunge na mahakama ni taasisi huru.
Mkuu Tindo, find time msikilize Kailima toka dakika ya 26
P
 
Pascal Mayalla .
Tukiachilia mbali bunge na mahakama, hebu tuambie wewe unatumia kigezo kipi kusema kwamba NEC ipo huru Hali ya kuwa the presiding personnel anateuliwa na mwenyekiti wa chama tawala?
Mkuu Mohammed Khatibu, Mwenyekiti wa NEC hateuliwi na Mwenyekiti wa CCM, anateuliwa na Rais wa JMT.
Tanzania ina mihimili mitatu huru na vyombo huru vifuatavyo, huru kwa maana ya independent kutokana na sheria inavyoviunda
Serikali
Bunge
Mahakama
Tume ya Uchaguzi
Tume ya Haki za Binaadam
Tume ya Tabia za Viongozi
Tume ya Kuzuia Rushwa
Tume ya Madawa ya Kulevya
Ofisi ya CAG
Ofisi ya DPP
Etc
Wakuu wa vyombo vyote hivyo wanateuliwa na rais wa JMT, Spika wa Bunge ndie Mkuu wa Mhimili lakini mtendaji Mkuu wa Bunge ni Katibu wa Bunge.
Kama Bunge ni huru, mahakama ni huru na NEC pia ni huru, ila sio Shirikishi.
P
 
Pascal Mayalla acha kupindisha Mambo!
In maana we hufahamu nafasi ya Magu katika uongozi wa ccm au unataka kurefueha Mambo hapa.

Technically ni kwamba NEC ipo chini ya uongozi wa ccm that's all!

Mkuu Mohammed Khatibu, Mwenyekiti wa NEC hateuliwi na Mwenyekiti wa CCM, anateuliwa na Rais wa JMT.
Tanzania ina mihimili mitatu huru na vyombo huru vifuatavyo, huru kwa maana ya independent kutokana na sheria inavyoviunda
Serikali
Bunge
Mahakama
Tume ya Uchaguzi
Tume ya Haki za Binaadam
Tume ya Tabia za Viongozi
Tume ya Kuzuia Rushwa
Tume ya Madawa ya Kulevya
Ofisi ya CAG
Ofisi ya DPP
Etc
Wakuu wa vyombo vyote hivyo wanateuliwa na rais wa JMT, Spika wa Bunge ndie Mkuu wa Mhimili lakini mtendaji Mkuu wa Bunge ni Katibu wa Bunge.
Kama Bunge ni huru, mahakama ni huru na NEC pia ni huru, ila sio Shirikishi.
P
 
Pascal Mayalla acha kupindisha Mambo!
In maana we hufahamu nafasi ya Magu katika uongozi wa ccm au unataka kurefueha Mambo hapa.

Technically ni kwamba NEC ipo chini ya uongozi wa ccm that's all!
Uteuzi wa nafasi mbalimbali ni kwa mujibu wa katiba zinafanywa na rais wa JMT. Hata inapotokea rais wa JMT ndiye huyo huyo Mwenyekiti wa CCM, uteuzi anateua kwa mujibu wa katiba ya JMT na sio katiba ya CCM. Kwa vile the dividing line between rais Magufuli as rais wa JMT and Magufuli as Mwenyekiti wa CCM is very thin, hivyo you can think whatever you think if it makes you happy, be Happy!.
P
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom