TV Imaan Hewani, Hongera

Status
Not open for further replies.

FaizaFoxy

Platinum Member
Apr 13, 2011
92,823
109,109
Hongera kwa wote walioshiriki kufanikisha hilo.

Naitazama TV Imaan sasa hivi ikifanya "Test Signal" ikirushwa na Startimes.

Natoa pongezi za dhati kwa wote waliojitahid kwa hali na mali katika kufanikisha hilo.

Najuwa wamepitia mengi sana mpaka kufikia hapa walipo na malipo yao wote yapo yanawangoja wala wasikate tamaa.

Nimefurahishwa sana kuona mmeleta kipindi cha mahojiano na mambo muhimu yanayotuhusu kila siku kwa kumleta mtaalaam wa SUMATRA, ametoa darsa la maana kuhusu usafiri wa abiria na kipindi kimekidhi matarajio na ziyada.

Tunawatakia kila la kheri na mafanikio na urushaji mwema wa vipindi vyenu.

Nawaomba Waislam na wasio Waislam waingie na kujifunza mengi kuhusu maisha na fikra za Kiislam, wengi huwa wanapata habari za Waislam kutoka katika vyanzo ambavyo si vya Kiislam na huwa wanapotoshwa sana, sasa kitumieni chombo hicho kupata habari na kuujuwa Uislam kutoka kwa Waislam wenyewe.

Wa bi Llahi Tawfiq.
 
...cc : ﺣﺮﻛﺔ ﺍﻟﺸﺒﺎﺏ ﺍﻟﻤﺠﺎﻫﺪﻳﻦ ; Ḥ
 
nitakaribia lakini naomba isianze kama redio imaan kabla ya kufungiwa.je nayo itakuwa elimu bila mipaka?
maana nijuavyo elimu yoyote lazma iwe na mipaka,kama ni chekechea utaweka ukomo wa umri kama ni jando na nyagi vivyo hivyo na kama ji jihad utawaondoa walemavu na watoto.
 
Hongera kwa lipi? Kitu gani cha maana walichofanya mpaka wapewe hongera au ndiyo yaleyale ya Radio Imaan tutaanza kuyashuhudia Live kwenye TV yao.

TCRA ifanye monitoring ya kutosha isije ikawa kama yaleyale ya Radio yao waliyoifungia kwa kueneza chuki.

Watanzania hatutaki kufika huko.
 
nitakaribia lakini naomba isianze kama redio imaan kabla ya kufungiwa.je nayo itakuwa elimu bila mipaka?
maana nijuavyo elimu yoyote lazma iwe na mipaka,kama ni chekechea utaweka ukomo wa umri kama ni jando na nyagi vivyo hivyo na kama ji jihad utawaondoa walemavu na watoto.

Naam, Elimu Bila Mipaka.

Karibu sana ujionee mwenyewe, "usiandikie mate na wino upo", tena naona sasa hivi kuna kipindi "live", nawe unaweza kupiga simu ukachangia au ukauliza swali kuhusu mada iliyopo.
 
Hongera kwa lipi? Kitu gani cha maana walichofanya mpaka wapewe hongera au ndiyo yaleyale ya Radio Imaan tutaanza kuyashuhudia Live kwenye TV yao.

TCRA ifanye monitoring ya kutosha isije ikawa kama yaleyale ya Radio yao waliyoifungia kwa kueneza chuki.

Watanzania hatutaki kufika huko.

Wacha uoga, pitia upate ilmu.
 
Kwenye taarifa ya habati( kama itakuwepo wewe wanatuwekea yanayojiri katika mahakama za kadhi za Pakistani na Sudan ili tuone idadi ya wanawake wanaouliwa kwa kupigwa mawe kwa sababu ya kuolewa na wasiotakiwa na jamaa zao
 
Kwenye taarifa ya habati( kama itakuwepo wewe wanatuwekea yanayojiri katika mahakama za kadhi za Pakistani na Sudan ili tuone idadi ya wanawake wanaouliwa kwa kupigwa mawe kwa sababu ya kuolewa na wasiotakiwa na jamaa zao

Yanahusu nini?
 
TV Imani iwe kichocheo cha upendo na mshikamano kwa taifa kinyume chake itakula ban.

Ikiwa ban, wala hazitustui tumekula ban ya habari kwa nyezo tulizokuwa nazo kwa wakati kwa miaka mingi tu.

Malariasugu yuko wapi?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom