Tuzungumzie maendeleo ya nchi na watu wake na sio ushindani wa kisiasa.

moonred

Member
Nov 19, 2012
5
0
Hivi sasa karibu kila chombo cha habari yaani magazeti,radio,television,mitandao ya kijamii n.k inazungumzia malumbano ya kisiasa ama baina ya vyama au makundi ya urais 2015 n.k kila kukicha vichwa vya habari ni malumbano tu.jamani hebu tubadilike.turipoti mambo ya maendeleo,kuhamasisha wananchi kushiriki katika mambo mbalimbali yanayohusu mustakbali wao na ya watoto wao,kutoa tahadhari ili kuepukana na magonjwa hatari kama ukimwi,malaria,kutoharibu mazingira n.k. Kama mambo ya kushika dola basi tusuburi 2015.nchi inateketea.kwa kutambua hali hii ndiyo maana hata majirani zetu wanatumia mwanya huu kutaka kutuangamiza.mfano mgogoro wa mpaka na malawi.wao wamegundua kuwa nchi yetu ni malumbano na kukashifiana tu.naomba tubadilike.
 
Naheshimu sana wazo hili. WaTanzania tusipgawe na siasa za CHADEMA kutaka kushika madaraka ya nchi hii. Tujadiliane masuala ya kujenga nchi yetu kwa kuwa Mungu ni mwaminifu ha
tatuacha tuangamizwe na CHADEMA.
 
Utawezezaje kujadili kufika mbinguni ama kuacha dhambi bila kumtaja Mungu na Shetani ?
 
mtoa mada nakushukuru saana kwangu mimi wewe ni miongoni mwa ma-great thinker. nimewafuatilia saana wanasiasa wetu, nashawishika saana kuwasifia , mh LOWASSA NA MH ZITO mara nyingi watu hawa nimefuatilia saana mazungumzo yao juu ya taifa letu, daima hawako ktk malumbano, wanazungumzia taifa letu linamatatizo gani? nini kifanyike ili tuweze kufanikiwa, lkn baadhi ya watu wamekaa kusikiliza leo huyu atasema nini? nimpinge vipi? MWL NYERERE anasema kuwa yeye alitawala nchi hii kwa miaka 27, kuna mazuri na mabaya aliyoyafanya tatizo sasa watu hawaendelezi yale mazuri wamekalia kushutumu tuu .miaka inakwenda. tubadilike tujenge taifa.
 
Back
Top Bottom