Tuzo za muziki za Kili

Paul S.S

JF-Expert Member
Aug 27, 2009
6,402
3,242
Wadau jana ilikua ni siku ya kukabidhi tuzo za muziki za kilimanjaro. naomba mtu mwenye matokeo yalikuaje ayaweke humu tuyajadili
 
Zahir Ally Zoro....Hall of Fame

Banana Zorro ....Mwimbaji bora wa kiume

Twanga pepeta...Wimbo bora na Albamu bora ya bendi

Khalidi Chokoraa...Rapa bora

Bwana Misosi....Wimbo bora wa Ragga

Mrisho Mpoto....Wimbo bora wa asili

Mzee Yusuf....Albamu bora ya taarab

Lady JD....Mwanamziki bora wa kike

Diamond....Msanii bora anaechipukia, Wimbo bora wa R&B

AY....Wimbo bora wa Reggae

Marlaw....Wimbo bora wa Afro Pop

CPwaa...Video bora

AT....Wimbo bora wa kolabo ''Nipigie''
 
hii ragga na reggae hapa napata tabu saana, nikiona au kusikia nyimbo hizo, ma man tuko wapi!

Enh mwakani ntajitosa maana naona bado sijaguswa vilivyo katika anga hiyo ya midundo ya hisia na mikito ya kufa, mwagito mwagalinoma muko wapi? Nganyagwa, jhiko man, jet man, slim
daddy, na wengineo......................hapa kuna watu wanaonekana kulala.....................
 
Lady JD Mwanamuziki Bora wa Kike........Ndizi Zoro Muimbaji bora wa kiume.Nadhani ipo tofauti hapo
 
DSC_5662.jpg

Michuzi akitoa tuzo ya Hall of Fame kwa mkongwe Zahir Ally Zorro huku akishuhudiwa na wanawe Banana (kulia) na Maunda pamoja na mzee mzima Kassim Mapili (shoto)

DSC_5687.jpg

Baba na mwana na familia wakifurahia tuzo zao ambapo baba kapata ya Hall of Fame na mwana kaibuka mwimbaji bora wa kiume kwa mara ya pili mfululizo

DSC07701.jpg

Mwenyekiti wa African Stars entertainment Baraka Msiilwa akiwa ameshikilia tuzo tatu ambazo Twanga Pepeta wamepata, ikiwa ni pamoja na wimbo bora, albamu bora ya bendi na rapa bora iliyoenda kwa Khalidi Chokoraa

DSC_5539.jpg

Bwana Misosi akishangilia tuzo ya wimbo bora wa Ragga aliyopewa na Sean Kingston

IMG_5802-1.jpg

Mrisho Mpoto (shoto) aliondoka na tuzo ya wimbo bora wa asili na 'Mjomba'


DSC_5565.jpg

Mzee Yusuf Alikomba tuzo za albamu bora ya taarab na ya mtunzi bora

DSC_5674.jpg

Gadna G. Habash akipokea toka kwa Tajiri Mpoki tuzo ya mwanamuziki bora wa kike ya Lady JD aliyopokea kwa niaba ya mai waifu wake Jide

DSC_5582.jpg

Khalid Chokoraa akipokea tuzo ya Twanga pepeta wa Bendi bora

IMG_5918.jpg

King Kikii akimkabidhi kwa Twanga Pepeta tuzo ya wimbo bora wa bendi

IMG_5928.jpg

Lwiza Mbutu akisogea kutoa shukrani baada ya kupokea tuzo ya albamu bora ya bendi iliyoenda kwa Twanga Pepeta

IMG_5924.jpg

Prodyuza bora wa mwaka akipokea tuzo


DSC_5645.jpg

Diamond akisherehekea moja ya tuzo zake ikiwa ni pamoja na msanii bora anayechipukia, wimbo bora wa R& B toka kwa mwenyekiti wa Yanga Imani Madega

DSC_5521.jpg

AY akisherehekea tuzo yake ya wimbo bora reggae

DSC07766.jpg

Lady JD akipozi na mai hazbendi wake na tuzo yake ya mwanamuziki bora wa kike

DSC07662.jpg

Marlaw akitamba na tuzo yake ya wimbo bora wa afro pop

DSC_5629.jpg

Mwana FA na wenzake wakimtuza Diamond kwa kuwa msanii bora chipukizi

DSC_5616.jpg

Hasheem Thabeet akimkabidhi C-Pwaaa tuzo ya video bora

DSC07740.jpg

Mwamvita Makamba na Ephraim Mafuru wakimkabidhi Banana Ally Zorro tuzo ya msanii bora wa kiume


DSC07687.jpg

Ras Inno Nganyagwa akimkabidhi AT tuzo ya wimbo bora wa kolabo aliofanya na Stara Thomas wa 'Nipigie'

Kwa msaada wa Michuzi Blog
 
Kuna wasanii kama AY,Lady Jay Dee,Banana kila mwaka lazima wapewe tuzo hata kama nyimbo zao mbovu
 
Michuzi nilikuwa nakusikia kwenye vyanzo mbalimbali vya habali ila kwa hayo mapicha ya KILI music Award nimekukubali! big up mkubwa.
 
Lilsun asante kwa habari hiyo,usikose leo diamond utupe majamboz kesho!
 
Back
Top Bottom