hii ragga na reggae hapa napata tabu saana, nikiona au kusikia nyimbo hizo, ma man tuko wapi!
Enh mwakani ntajitosa maana naona bado sijaguswa vilivyo katika anga hiyo ya midundo ya hisia na mikito ya kufa, mwagito mwagalinoma muko wapi? Nganyagwa, jhiko man, jet man, slimdaddy, na wengineo......................hapa kuna watu wanaonekana kulala.....................
Michuzi akitoa tuzo ya Hall of Fame kwa mkongwe Zahir Ally Zorro huku akishuhudiwa na wanawe Banana (kulia) na Maunda pamoja na mzee mzima Kassim Mapili (shoto)
Baba na mwana na familia wakifurahia tuzo zao ambapo baba kapata ya Hall of Fame na mwana kaibuka mwimbaji bora wa kiume kwa mara ya pili mfululizo
Mwenyekiti wa African Stars entertainment Baraka Msiilwa akiwa ameshikilia tuzo tatu ambazo Twanga Pepeta wamepata, ikiwa ni pamoja na wimbo bora, albamu bora ya bendi na rapa bora iliyoenda kwa Khalidi Chokoraa
Bwana Misosi akishangilia tuzo ya wimbo bora wa Ragga aliyopewa na Sean Kingston
Mrisho Mpoto (shoto) aliondoka na tuzo ya wimbo bora wa asili na 'Mjomba'
Mzee Yusuf Alikomba tuzo za albamu bora ya taarab na ya mtunzi bora
Gadna G. Habash akipokea toka kwa Tajiri Mpoki tuzo ya mwanamuziki bora wa kike ya Lady JD aliyopokea kwa niaba ya mai waifu wake Jide
Khalid Chokoraa akipokea tuzo ya Twanga pepeta wa Bendi bora
King Kikii akimkabidhi kwa Twanga Pepeta tuzo ya wimbo bora wa bendi
Lwiza Mbutu akisogea kutoa shukrani baada ya kupokea tuzo ya albamu bora ya bendi iliyoenda kwa Twanga Pepeta
Prodyuza bora wa mwaka akipokea tuzo
Diamond akisherehekea moja ya tuzo zake ikiwa ni pamoja na msanii bora anayechipukia, wimbo bora wa R& B toka kwa mwenyekiti wa Yanga Imani Madega
AY akisherehekea tuzo yake ya wimbo bora reggae
Lady JD akipozi na mai hazbendi wake na tuzo yake ya mwanamuziki bora wa kike
Marlaw akitamba na tuzo yake ya wimbo bora wa afro pop
Mwana FA na wenzake wakimtuza Diamond kwa kuwa msanii bora chipukizi
Hasheem Thabeet akimkabidhi C-Pwaaa tuzo ya video bora
Mwamvita Makamba na Ephraim Mafuru wakimkabidhi Banana Ally Zorro tuzo ya msanii bora wa kiume
Ras Inno Nganyagwa akimkabidhi AT tuzo ya wimbo bora wa kolabo aliofanya na Stara Thomas wa 'Nipigie'
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.