Bramo
JF-Expert Member
- Oct 21, 2009
- 13,160
- 10,007
Unajua Kiingereza ?Kulikuwa na mabishano ya muda mrefu ndani ya wadau wa vyama vyote vya siasa kuhusu chama cha siasa cha CHADEMA.
Baadhi ya wadau, walifikia hatua ya kusema CHADEMA siyo chama cha siasa tena baada ya kuondokewa na viongozi wake nguli kama Dkt. W. Slaa na team yake.
Baadhi ya watanzania walifikia hatua ya kukifananisha CHADEMA sawa na SACCOS ya mtu, Chama cha mtu au kikundi cha watu, nk.
Kubwa zaidi CHADEMA ilikuja kuitwa nichama cha KIUANAHARAKATI, hii kulingana na siasa ilizokuja kuanza kuzifanya hivi karibuni.
Ndani ya CHADEMA, viongozi,na wanachama, pamoja na washabiki , wamekuwa wakilipinga hilo kwa nguvu zote.
Juzi hapa jamii ya watanzania na Dunia kwa ujumla , wameshuhudia MAKAMU MWENYEKITI WA CHADEMA na aliyekuwa mgombea Urais tanzania ndg Tundu A. Lissu akipokea TUZO YA MWANAHARAKATI BORA.
Hii tuzo ambayo Tundu Lissu alikuwa akiifrahia pamoja na wadau wake ambao waliweka mpaka uzi humu nadhani hawakujua kama lilikuwa nijibu la ubishani wa muda mrefu.
Hii haina ubishi kuwa, CHADEMA SIYO CHAMA CHA SIASA TENA, BALI NICHAMA CHA WANAHARAKATI .
Nawasilisha tafadhali.
Enzi na enzi.
Dar es salaam.