Tuwekeze watoto ktk elimu

kangamema

New Member
Oct 4, 2011
1
0
watanzania wenzangu tujifunze kutoka kwa wenzetu wachaga. Shule za kata huko Kilmanjaro zilianza miaka mingi. Leo viongozi wetu wetu wanatusambazia urithi huu wa elimu tunawabeza. Mmeona faida ya elimu k wa wenzetu? Karibu kila mchaga ana kazi ya maana na wala sio ukabila ni elimu.
 
Ulipoanza na "watanzania wenzangu" nilidhani unatoa mfano wa nchi nyingine. Kumbe unazungumzia watanzania wenzetu. lakini nadhani unahitaji kwenda mbele na kujiuliza hizo shule za uchagani zinamilikiwa na nani au zilijengwa na nani, badala ya kutoa sifa tu bila kujua hilo limefikaje hapo. Ukisikiliza hotuba ya Mwalimu Nyerere katika miaka ya 60 utaelewa ni kwa nini wachagga, wahaya na wanyakyusa wamesoma kuliko makabila mengine. Hizi zilikuwa ni juhudi za wamisionari na siyo wakoloni wala serikali ya baada ya Uhuru. Ndiyo maana baadae Mwalimu aliamua kutaifisha shule ili kuruhusu wale wa imani na madhehebu tofauti kujiunga nazo na kupanua wigo. Hata hivyo wanafunzi wa kutoka maeneo zilizpo shule hizo waliendelea kuwa wanufaika wa kwanza.
 
Back
Top Bottom