Ishaka
Member
- Nov 1, 2011
- 74
- 12
Wana JF, jana usiku ITV walionyesha kipindi maalum kikiripoti matukio ya askari wanyama poli kuua raia na ng'ombe wao kwa risasi za moto kupokea rushwa, viongozi wa serikali za vijiji wilaya za Ngara na Biharamulo kutumia vibaya madaraka, kuuza maeneo ya wafugaji kwa wahamiaji haramu toka nchi jirani za Rwanda na Burundi, uharibifu mkubwa wa mazingira (misitu na tembo).....na mengi mengineyo ya kutisha!
Kipindi hiki kimebainisha kuhusika moja kwa moja kwa uongozi wa juu wa Wilaya husika ambao wamekuwa wakinufaika na janga hili la kitaifa. Katika mahojiano baina ya wananchi (waathirika) na mwandishi wa habari, inaonyesha wazi migogoro hii imeanza kitambo sana na hakuna hatua za makusudi zilizowahi kuchukuliwa kumaliza tatizo hili la wafugaji na askari wa misitu ya hifadhi, na wavamizi haramu wenye ng'ombe wengi toka nchi jirani sababu viongozi wanaonufaika na kashfa hii wamekuwa wakitumia nafasi zao kuzuia, kuwatisha na hata kuwabambikia kesi waandishi wa habari ili isijulikane kinachoendelea huku watu wakiteseka.
Je, amani na utulivu inayoimbwa katika majukwaa ya siasa ni ipi au mkoa wa Kagera si sehemu ya Tanzania? serikali iko wapi na kama si ustaarabu wa watu wa mkoa huu kuheshimu sheria za nchi hali ingekuwaje kule! Inawezekanaje mgeni auziwe pori la malisho ya mifugo ya wanavijiji na kusababisha migogoro baina ya wakulima na wafugaji - wauwane wenyewe kwa wenyewe kisha alindwe na mamlaka za serikali ya kijiji.
Mkoa wa kagera umekumbwa na maafa mengi sana kihistoria; Kwanza ukimwi, pili ajali ya meli ( MV Bukoba), tatu mnyauko (ugonjwa wa migomba), nne mzigo wa wakimbizi toka nchi za Rwanda na Burundi, tano Ujambazi wa kuteka mabasi kuua na kuiba mali kwa kutumia silaha nzito za kivita, sita Wimbi la watoto yatima vijijini na mjini, saba Umaskini uliokithiri tokana na yote yaliyotajwaa hapo juu
Kipindi hiki kimebainisha kuhusika moja kwa moja kwa uongozi wa juu wa Wilaya husika ambao wamekuwa wakinufaika na janga hili la kitaifa. Katika mahojiano baina ya wananchi (waathirika) na mwandishi wa habari, inaonyesha wazi migogoro hii imeanza kitambo sana na hakuna hatua za makusudi zilizowahi kuchukuliwa kumaliza tatizo hili la wafugaji na askari wa misitu ya hifadhi, na wavamizi haramu wenye ng'ombe wengi toka nchi jirani sababu viongozi wanaonufaika na kashfa hii wamekuwa wakitumia nafasi zao kuzuia, kuwatisha na hata kuwabambikia kesi waandishi wa habari ili isijulikane kinachoendelea huku watu wakiteseka.
Je, amani na utulivu inayoimbwa katika majukwaa ya siasa ni ipi au mkoa wa Kagera si sehemu ya Tanzania? serikali iko wapi na kama si ustaarabu wa watu wa mkoa huu kuheshimu sheria za nchi hali ingekuwaje kule! Inawezekanaje mgeni auziwe pori la malisho ya mifugo ya wanavijiji na kusababisha migogoro baina ya wakulima na wafugaji - wauwane wenyewe kwa wenyewe kisha alindwe na mamlaka za serikali ya kijiji.
Mkoa wa kagera umekumbwa na maafa mengi sana kihistoria; Kwanza ukimwi, pili ajali ya meli ( MV Bukoba), tatu mnyauko (ugonjwa wa migomba), nne mzigo wa wakimbizi toka nchi za Rwanda na Burundi, tano Ujambazi wa kuteka mabasi kuua na kuiba mali kwa kutumia silaha nzito za kivita, sita Wimbi la watoto yatima vijijini na mjini, saba Umaskini uliokithiri tokana na yote yaliyotajwaa hapo juu